KERO Wakazi wa Msasani Mikoroshini tunateseka maji taka yanatiririshwa Mtaani makusudi, tumeripoti NEMC ila wametuacha tupambane wenyewe

KERO Wakazi wa Msasani Mikoroshini tunateseka maji taka yanatiririshwa Mtaani makusudi, tumeripoti NEMC ila wametuacha tupambane wenyewe

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

informer 06

Member
Joined
May 11, 2024
Posts
66
Reaction score
49
WhatsApp Image 2025-02-03 at 16.15.15_1bacb44f.jpg

Hapa mtaani kwetu kuna changamoto ya kimazingira inaendelea huu ni Mwaka wa tatu sasa maeneo ya Msasani Mikoroshini yanaathiriwa na maji taka yanayotoka kwenye makazi ya mtu mmoja ambaye ni kama imeshindikana kumdhibiti kwa kile kinachoonekana yeye ana nguvu kuliko wengine.

Kwa ufupi ni kuwa kuna maji taka ambayo yanatoka kwenye majengo ya mtu huyo na kutiririka mitaani siku zote, ikifika muda wa mvua ndio kabisa hali inakuwa mbaya kwa wahusika hao kutiririsha au kufungulia maji machafu ili yaungane na yale ya mvua na kuingia mtaani.

Wananchi tumesharipoti mara kibao kwa Serikali za Mtaa lakini hatuoni jitihada za wahusika kuleta suluhu badala yake tunaendelea kuteseka bila msaada wowote, tukienda kuripoti katika ofisi za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaishia kusema “Hayo ni mambo ya Serikali za Mtaa karipotini huko”.

Viongozi wa Serikali za Mtaa wenyewe tukiripoti kwao wakienda hapo kwenye hiyo nyumba ambapo maji machafu yanatoka, wanatoka wakitabasamu na hakuna kinachoendelea.

Katika hali ya kusikitisha zipo chemba ambazo zipo karibia na makazi zinafanya harufu kuwa kali kutokana na kutiririsha maji machafu ambayo kuna muda yanakuwa na funza, yanaingia mitaani, inauma sana.

Changamoto hiyo imedumu kwa muda mrefu lakini hatuoni mabadiliko badala yake hali inazidi kuwa mbaya zaidi na inaongeza wasiwasi wa kupata magonjwa.

Kwakuwa yapo majukwaa huru kama JF tunaomba mamlaka za juu kufuatilia suala hili kwa kina ili ambapo kuna uzembe wahusika wawajibike iwe ni kuanzia Serikali za Mtaa pamoja na baadhi ya maafisa wa NEMC ambao tumeripoti kwao na hawajachukua hatua mpaka sasa.

WhatsApp Image 2025-02-03 at 16.24.03_76e96274.jpg

WhatsApp Image 2025-02-03 at 16.24.03_e905866a.jpg

WhatsApp Image 2025-02-03 at 16.24.03_e9156ee0.jpg
 
Hiyo NEMC tangu aondoke heche ilijifia yenyewe bora heche alikua anachukua hatua na kufanya maamuzi
 
Msasani!! Huko si kwa ma boss? Hivyo vivanda vipi tena? Lol
 
Hao NEMC Na wafike Shule ya ST.PARICK MISSION HIGH SCHOOL.
Sita andika mengi wafike ajionee, waongee na watendaji serikali ya mtaa, wajumbe, nk
Wazazi wa wanafunzi hawajui watoto wao wako mazingira hatarishi sana
 
Hapa mtaani kwetu kuna changamoto ya kimazingira inaendelea huu ni Mwaka wa tatu sasa maeneo ya Msasani Mikoroshini yanaathiriwa na maji taka yanayotoka kwenye makazi ya mtu mmoja ambaye ni kama imeshindikana kumdhibiti kwa kile kinachoonekana yeye ana nguvu kuliko wengine.

Kwa ufupi ni kuwa kuna maji taka ambayo yanatoka kwenye majengo ya mtu huyo na kutiririka mitaani siku zote, ikifika muda wa mvua ndio kabisa hali inakuwa mbaya kwa wahusika hao kutiririsha au kufungulia maji machafu ili yaungane na yale ya mvua na kuingia mtaani.

Wananchi tumesharipoti mara kibao kwa Serikali za Mtaa lakini hatuoni jitihada za wahusika kuleta suluhu badala yake tunaendelea kuteseka bila msaada wowote, tukienda kuripoti katika ofisi za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaishia kusema “Hayo ni mambo ya Serikali za Mtaa karipotini huko”.

Viongozi wa Serikali za Mtaa wenyewe tukiripoti kwao wakienda hapo kwenye hiyo nyumba ambapo maji machafu yanatoka, wanatoka wakitabasamu na hakuna kinachoendelea.

Katika hali ya kusikitisha zipo chemba ambazo zipo karibia na makazi zinafanya harufu kuwa kali kutokana na kutiririsha maji machafu ambayo kuna muda yanakuwa na funza, yanaingia mitaani, inauma sana.

Changamoto hiyo imedumu kwa muda mrefu lakini hatuoni mabadiliko badala yake hali inazidi kuwa mbaya zaidi na inaongeza wasiwasi wa kupata magonjwa.

Kwakuwa yapo majukwaa huru kama JF tunaomba mamlaka za juu kufuatilia suala hili kwa kina ili ambapo kuna uzembe wahusika wawajibike iwe ni kuanzia Serikali za Mtaa pamoja na baadhi ya maafisa wa NEMC ambao tumeripoti kwao na hawajachukua hatua mpaka sasa.

Mkuu hapo Msasani Mikoroshini upande gani?
 
NEMC imekuwa ni porojo tu na hawafuatilii na kutatua changamoto za wananchi, au mpaka yatokee majanga?
 
Hili ni janga jipya kwa sehemu kubwa ya Dar es salaam. Unakuta mtu kajenga nyumba yake ya makazi yeye na familia yake huku kachimba shimo la majitaka la kawaida kulingana na ukubwa wa familia yake. Sasa ghafla anaifanyia matenegenzo anaibadili kuwa nyumba ya kupanga. Shida inaanzia hapo idadi ya watu inaongezeka halafu shimo la majitaka linabaki lile. Matokeo yake shimo linajaa baada ya muda mfupi na hapo mwenye nyumba kuleta gari la majitaka kunyonya hayo maji kila siku anaona hasara na hapo ndio mwanzo wa kutiririsha majitaka mitaani.

Ushauri wa bure kwa wenye nyumba mnapofikiria kubadilisha matumizi ya nyumba zenu msiaangalie tu kuongeza vyumba andaeni pia nafasi ya kuongeza shimo la majitaka na miundo mbinu mingine ili kuweza kuendana na ongezeko la idadi ya watu watakao kuja kuishi kwenye hiyo nyumba. Hii itawasaidia nyinyi wenyewe na majirani zenu.

Ni mtizamo tu.
 
Back
Top Bottom