KERO Wakazi wa Nyarero- Tarime hatuna maji mwezi wa pili sasa, RUWASA wametelekeza Ofisi,

KERO Wakazi wa Nyarero- Tarime hatuna maji mwezi wa pili sasa, RUWASA wametelekeza Ofisi,

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Ruwasaa.jpg

Sisi wakazi wa Kijiji cha Kemakorere, Kata ya Nyarero Wilayani Tarime tuna changamoto ya kukosekana kwa huduma ya maji kwa muda wa zaidi ya miezi miwili sasa.

Wanaohusika wangeweza kusingizia kuwa hakuna umeme, lakini umeme upo, mabomba yapo na miundombinu yote ipo lakini maju hakuna na hakuna kiongozi wala ngazi ya Mamlaka inayotoa taarifa kuhusu kinachoendelea.
Ruwasa.jpg
Hapa kwenye Kijiji kuna Ofisi za RUWASA lakini tangu zimekamilika Ofisi hazijafunguliwa na hakuna anayesema kuna nini kinachoendelea.

Tunaomba ujumbe huu ufike Serikalini na wajue kuwa RUWASA wametelekeza ofisi na Wananchi hatuna huduma yam aji, tunalazimika kwenda kuchota kwenye visima ambavyo vingine maji yake sio salama kwa afya.

Soma Pia:
~ Huduma ya maji yarejea Kijiji cha Kemakorere, andiko la Mwanachama wa JF lawafikia RUWASA
~ DAWASA, watu wa Mbezi Luis Makabe mpaka kwa Robert hatuna maji yapata wiki sasa. Mhandisi hapokei simu, namba ya huduma kwa wateja haipatikani


rUWAS.jpg
 

Sisi wakazi wa Kijiji cha Kemakorere, Kata ya Nyarero Wilayani Tarime tuna changamoto ya kukosekana kwa huduma ya maji kwa muda wa zaidi ya miezi miwili sasa.

Wanaohusika wangeweza kusingizia kuwa hakuna umeme, lakini umeme upo, mabomba yapo na miundombinu yote ipo lakini maju hakuna na hakuna kiongozi wala ngazi ya Mamlaka inayotoa taarifa kuhusu kinachoendelea.
Hapa kwenye Kijiji kuna Ofisi za RUWASA lakini tangu zimekamilika Ofisi hazijafunguliwa na hakuna anayesem kuna nini kinachoendelea.

Tunaomba ujumbe huu ufike Serikalini na wajue kuwa RUWASA wametelekeza ofisi na Wananchi hatuna huduma yam aji, tunalazimika kwenda kuchota kwenye visima ambavyo vingine maji yake sio salama kwa afya.

Bora nyie mna hata hayo matank,mnaishi kwa imani kwamba yatapatikana

Sisi huku kwetu sasa dah!
 
Mimi nipo korotambe hapa kata ya mwema tarime, mabomba ya maji tayari yamekamilika ila wazee wa koo hawataki mabomba hayo yatumike kwa sababu wake zao waendelee kufuata maji mtoni kama walivyokuwa wakifanya hapo mwanzo na wanadai eti ni ukisasa wa kuja kuwavurugia ndoa za vijana wao

Kwa hiyo wana tarime wanachangamoto za kijinga za kujitakia wenyewe, suala linalohusu kumkomboa mwanamke hawaliungi mkono hii ni hatari sana

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom