Wake wa wanajeshi wa FARDC huko Goma walilia maisha magumu

Wake wa wanajeshi wa FARDC huko Goma walilia maisha magumu

MBOKA NA NGAI

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2025
Posts
350
Reaction score
576
Baadhi ya wanawake ambao waume zao walikuwa wanajeshi wa FRDC(jeshi la DRC), wanahangaika sana baada ya waume zao kufia vitani, wengine wapo kambini ilipo MONUSCO, wengine wamekimbilia nchi jirani ya Rwanda.

Wanawake hao walibaki na watoto. Wanachokiongelea ni kwamba wamefukuzwa kambini walikokuwa wakiishi, na kwamba mpaka sasa wapo wapo tu.

Kwa sasa, walikuwa wamepata hifadhi katika shule mbali mbali, lakini uongozi wa M23, ulitangaza kuwa shule zifunguliwe, na wao wanasema ingelikuwa kambi bado zipo wangeenda kambini.

Uongozi wa kundi la M23 haujatangaza chochote kuhusu hawa watu.

 
Ili ujue haya mambo magumu utashangaa nao wanapewa hifadhi na m23 na mirathi wanapewa
Hii inatosha kabisa kuwavunja morali askari waliokua mbele ,

Kwamba kumbe hata sisi tukifia nchi familia zetu zitakumbwa na haya?

Waziri wa ulinzi nae kaenda " kukagua" mstari wa mbele maelezo mengii mara mfie Nchi haya ufie nchi familia ifukuzwe kota ?
Tatizo la Congo hata Uongozi wao unahusika kweli kabisa
 
Back
Top Bottom