Wakenya hamuwezi kupata mabadiliko bila ninyi wenyewe kubadilika

Wakenya hamuwezi kupata mabadiliko bila ninyi wenyewe kubadilika

joto la jiwe

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2017
Posts
26,117
Reaction score
46,617
Ni wazi kwamba wagombea wakuu wa kiti cha urais Kenya katika uchaguzi wa 2022 wameshajulikana, 1)Raila, 2)Rutto.

Hawa wote sio wageni katika siasa za Kenya, wakenya wanawajua vizuri sana kwasababu walishashika nafasi nyingi tena nafasi za juu sana katika serikali ya Kenya kwa muda mrefu sana, kwahiyo uwezo wao unajulikana ndani na nje ya Kenya.

Ni wazi kwamba nchi ya Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo mwelekeo wake wa kisiasa, kijamii na kiuchumi haupo vizuri kabisa, rushwa, malumbano ya kikabila na ukanda, mzigo wa madeni, upungufu wa ajira na gharama za maisha vimekua ni matatizo yanayozidi kuwaumiza wakenya siku hadi siku.

Raila na Rutto wamekua ni sehemu ya viongozi walioifikisha Kenya hapa ilipo, katika vipindi vyao vyote vya uongozi, Hakuna hata mmoja anayeweza kujipiga kifua hadharani na kusema kwamba japo amechangia katika kupunguza kero moja wapo kati ya hizo nilizozitaja, kwa ufupi hakuna hata mmoja mwenye rekodi ya kutukuka katika uongozi wao, karibu wote wanashindwa na Matiang'i kwa mbali sana.

Magufuli alipokua waziri, aliweka rekodi nzuri kuwashinda mawaziri wote akiwemo waziri mkuu aliyekuwepo na wale wastaafu, japo hakuwa na wafuasi wengi ukilinganisha Lowasa na Membe ambao walikuwa wakitajwa Sana kama wanavyotajwa Raila na Rutto, lakini watanzania tuliamua kumchagua Magufuli kutokana na rekodi yake ya uchapakazi bora.

Swali la kujiuliza, Kenya wanatumia vigezo gani vya kuwashabikia Raila na Rutto na kumuacha Matiang'i?, je wakenya wanategemea kupata mabadiliko chanya endapo Rutto au Raila atakua rais, au ni yale yale ya kuchagua viongozi kwa misingi ya ukabila na mara tu baada ya uchaguzi wakenya wote wanaungana kulalamikia rushwa, ukabila, deni la Taifa, mauaji, ukosefu wa ajira na ugumu wa maisha?

Ukweli lazima tuuseme, kwa sisi ambao tupo nje ya Kenya tupo katika nafasi nzuri zaidi ya kutoa mawazo ambayo hayapendelei mtu au kabila lolote.

Kwa hali ya Kenya ilipofikia, hakutatokea mabadiliko yoyote endapo Raila au Rutto atakua rais. Wakenya ambao hawatumii vigezo vya ukabila, uchama, au maeneo walikotoka wanajua wazi kabisa kwamba ukilinganisha uchapaji kazi wa Raila na Rutto, hawawezi kumkaribia Matiang'i.
 
Nenda kambie hayo ndugu zako miccm mijinga
Huyo amewambia au ameshauri hivyo maana sisi ka watz tumepitia hapo mlipo au umesahau mpaka tukawa tunaitwa shamba la bibi. Kikubwa nyie pigeni ruto na huyo mzee chini halafu muangalie katika mawaziri nani anafanya kazi toka moyoni na lazma atakuwepo lazima. Bt hata ka ushauri nyie mnaona ugomvi basi sawa wawekeni huyo ruto au huyo mzee afu tuone.
 
Huyo amewambia au ameshauri hivyo maana sisi ka watz tumepitia hapo mlipo au umesahau mpaka tukawa tunaitwa shamba la bibi... Kikubwa nyie pigeni ruto na huyo mzee chini halafu muangalie katika mawaziri nani anafanya kazi toka moyoni na lazma atakuwepo lazima.. Bt hata ka ushauri nyie mnaona ugomvi basi sawa wawekeni huyo ruto au huyo mzee afu tuone
Wakenya wapo tayari kufa kuliko kukubali mawazi ya mtanzania. Hivi sasa 90% ya viongozi na raia wa Kenya wanakubali kwamba njia bora ya kupambana na Corona ni aliyotumia Magufuli, lakini hawapotayari kuja kuomba ushauri, kwao ni bora waendelee kuhesabu maiti za wakenya kuliko kuja kuomba ushauri kwa Magufuli.

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
 
Wakenya wapo tayari kufa kuliko kukubali mawazi ya mtanzania. Hivi sasa 90% ya viongozi na raia wa Kenya wanakubali kwamba njia bora ya kupambana na Corona ni aliyotumia Magufuli, lakini hawapotayari kuja kuomba ushauri, kwao ni bora waendelee kuhesabu maiti za wakenya kuliko kuja kuomba ushauri kwa Magufuli.

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
Wenye busara walishawai sema njia ya kwanza ya kusolve kosa ni kukubali kwamba umekosea then ndio utaona good solution.
Hawa Kenyans wacha wakaze shingo tusipoona wanarudi tulipokua sisi (LDC)
 
Yaani leo hii wakenya tunapewa mawaidha kuhusu mabadiliko na watu ambao wametafunwa kweli kweli na chama kimoja kwa miongo kadhaa. [emoji1] Watu ambao hadi kwenye milenia mpya hii bado wanajivunia utawala wa kidikteta na kumuimbia mzee mtakatifu mapambio na sifia sifia za kiboya. Tena ambao badao wanaona sifa kutumia katiba ambayo waliachiwa na mkoloni. Ha!
 
Yaani leo hii wakenya tunapewa mawaidha kuhusu mabadiliko na watu ambao wametafunwa kweli kweli na chama kimoja kwa miongo kadhaa. [emoji1] Watu ambao hadi kwenye milenia mpya hii bado wanajivunia utawala wa kidikteta na kumuimbia mzee mtakatifu mapambio na sifia sifia za kiboya. Tena ambao badao wanaona sifa kutumia katiba ambayo waliachiwa na mkoloni. Ha!
Ndo mana nmeshangaa WaTz kina joto la jiwe kuwapa ushauri mzuri hv wakati inabd kuwaacha muingie mkenge ili tuzd kuwatawala [emoji3][emoji3]
 
Yaani leo hii wakenya tunapewa mawaidha kuhusu mabadiliko na watu ambao wametafunwa kweli kweli na chama kimoja kwa miongo kadhaa. [emoji1] Watu ambao hadi kwenye milenia mpya hii bado wanajivunia utawala wa kidikteta na kumuimbia mzee mtakatifu mapambio na sifia sifia za kiboya. Tena ambao badao wanaona sifa kutumia katiba ambayo waliachiwa na mkoloni. Ha!
Nimetoa ushauri nikiwa na nia njema kabisa, kila mkenya mwenye busara akisoma huu uzi atagundua ukweli na nia njema niliyonayo kwasababu hakuna tofauti na waliyosema wakenya wasomi siku mbili baada ya kufungua huu uzi
Raila na Ruto wataifaa Kenya? – Taifa Leo

It is up to Kenyans to decide, either to get new Kenya the way Tanzania did, or to continue with chest thumbing and continue with sufferings like what is happening with current administration., the choice is yours our brothers and sisters.

Only one thing to remind you is that Koffi Annan and Benjamin Mkapa are not around any more.
 
Nimetoa ushauri nikiwa na nia njema kabisa, kila mkenya mwenye busara akisoma huu uzi atagundua ukweli na nia njema niliyonayo kwasababu hakuna tofauti na waliyosema wakenya wasomi siku mbili baada ya kufungua huu uzi
Raila na Ruto wataifaa Kenya? – Taifa Leo

It is up to Kenyans to decide, either to get new Kenya the way Tanzania did, or to continue with chest thumbing and continue with sufferings like what is happening with current administration., the choice is yours our brothers and sisters.

Only one thing to remind you is that Koffi Annan and Benjamin Mkapa are not around any more.
Mwishoni wakamalizia kuwakumbusha kwamba Koffi Annan na Mkapa hawapo so wakichinjana wasitegemee msaada.
 
Back
Top Bottom