Wakenya wakati umefika wakuwa wazalendo, adui yetu sasa ni alshabaab na serikali

Wakenya wakati umefika wakuwa wazalendo, adui yetu sasa ni alshabaab na serikali

flyingcrane

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2014
Posts
241
Reaction score
88

Serikali yetu inataka kupitisha sheria takriban 24 za usalama dhidi ya ugaidi. ikiwa zitapita mambo haya hatatokea:

Tutakosa uhuru wa kuchat fb, twitter na hapa JF kwa kisingizio cha usalama. tutakamatwa na NIS na kupigwa faini ya millioni 5 au kifungo cha miaka mitatu, tusikubali kupimiwa uhuru wetu wa kuwasiliana

NIS itachunguza kukamata washukiwa wa ugaidi na kuwazuia kwa mda wa mwaka mmoja unavyojuwa hawa jamaa walivyokuwa wakatili..

Serikali itanyima vyombo vya habari uwezo wa kutujuza matukio ya kigaidi nchini na udhaifu dhidi ya serikali kama lilivyotokea westigate wanajeshi kuiba

Wakenya tunavyopenda kuandamana serikali inapotukosea na kubeba nguruwe, punda na kumwaga damu chafu mlangoni bungeni kuwaonyesha kutoridhishwa kwetu, haya yote tutanyimwa.

TUTAKUWA KAMA WATUMWA, WANYONGE WASIOKUWA NA HAKI, TUTATESEKA KWA MIAKA MINGI

Serikali itaiba mabilioni bila sisi kuwa na uwezo wa kuikashifu, ukitoa mdomo tu unapotezwa.
Wakenya kenya haiko katika enzi za moi, wala kama utawala wa museveni au mugabe..Kenya ni nchi huru na tupiganie haki zetu kwa lolote lile.

Uhuru ametumia kigezo cha magaidi kupitisha sheria hii ya kidhulma na kikatili. Tunaunga mkono vita dhidi ya Alshabaab, tunaunga mkono pia vipengele vingi katika mabadiliko hayo lakini wakenya tuwe waangalifu sana kupitisha sheria ambazo zitatuumiza kama wananchi

WAKATI WA MAANDAMANO NA KUPINGA SHERIA HIZI NI SASA NA KAMA SI SASA NI SASA HIVI, TUWE TAYARI KUIKOMBOA NCHI KWA LOLOTE LILE
 
..sasa mmejitambua kuwa adui yenu ni Al-Shabaab na siyo Tanzania.

..for quite sometime you were busy hating on Tanzania, badala ya kutafuta mbinu za kuondokana na Al-Shabaab.
 
Ume data ndugu yaan aduiwenu awe serikali yenu,halafu sula la wewe kuwa na mashaka fb twtt,jf nk, kwani unahusika ktk ugaid mpaka uogope? wacha zako kama hufanyi kosa wasiwasi wako nn.Tanzania sis tupohuru kufanya tutakavyo irimladi usikiuke sheria za nchi,nawe kama utakiuk sheria za nchiyenu Kenya wacha upate ustahilicho
 
Back
Top Bottom