Wakenya Wakinukisha tena, Waimba "RUTO MUST GO" Katika Kituo cha Bomas ya Kenya katika Sakata la Kufukuzwa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua

Wakenya Wakinukisha tena, Waimba "RUTO MUST GO" Katika Kituo cha Bomas ya Kenya katika Sakata la Kufukuzwa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakenya walikusanyika kwa wingi na kuanza kuimba kwa nguvu "RUTO MUST GO." Mkutano huo ulilenga kujadili kufukuzwa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, na umeshuhudia wananchi wakionesha hasira na kutoridhishwa na uongozi wa sasa.
Cheche kali za kisiasa na wakati mwingine vurugu zilishuhudiwa huku Wakenya katika kaunti zote 47 wakitoa maoni kuhusiana na hoja maalum inayolenga kumfurusha Naibu Rais Rigathi Gachagua madarakani.

Katika ukumbi wa Bomas, kaunti ya Nairobi, kikao cha utoaji maoni kilisitishwa baada ya vurugu kuzuka ukumbini.

Hii ni baada ya mwanaharakati Morara Kebaso kubebwa kwa nguvu na kufukuzwa eneo hilo punde alipowasili kutoa maoni yake.

Pia, Soma: Rigathi Gachagua adinda kujiuzulu, asema bila yeye Ruto asingeingia Ikulu

Raia walilalamika vikali, wakidai waandaji walikataza wapinzani wa Gachagua kutoa maoni. Katika kaunti ya Nakuru, kikao cha utoaji maoni kilisitishwa baada ya kudaiwa kuwa hojaji zilikuwa nakala na si halisi. Wafuasi wa Gachagua walidaiwa kuzuiwa kuingia ukumbini, hali iliyosababisha watu kuingia mitaani kulalamikia hali hiyo.

Hoja maalum ya kutaka Gachagua afurushwe iliwasilishwa bungeni na mbunge wa Kibwezi Magharibi, Eckomas Mwengi Mutuse, ikiwa na mashtaka 11, ikiwemo ukabila na ubadhirifu wa mali ya umma. Wakenya wameruhusiwa kutoa maoni kwa mujibu wa kifungu 118 cha katiba.

Jaribio la Naibu Rais kuzuia zoezi la ukusanyaji maoni lilishindikana, na kesi hiyo itatajwa Oktoba 9. Wakati huo, wabunge wamesubiri kusikiliza hoja ya Mutuse na kuamua kama kumtimua au kumweka Gachagua madarakani. Ili hoja ipite, wabunge 233 wanahitajika kuiunga mkono, huku wabunge 291 tayari wamesaini kutaka Gachagua afukuzwe.

Soma:
--> Gachagua akana kudai Ksh.8B ili akubali kuachia nafasi ya Naibu Rais wa Kenya
--> Gachagua awaonya Wabunge: Mmekula hadi mmevimbiwa sasa mnawatapikia Wananchi, kuweni na Heshima basi!
 
Wametumwa na Gachagua hao. Aliendekeza watu wa Murima Kenya sasa kimewaka
 
Leo mchana fujo zimetokea katika ukumbi wa Bomas of Kenya wakati wa zoezi
la kuwashirisha wananchi zoezi la kumkong'oa naibu wa Rais Rigadhi Gachagua

Wakili na Mwanaharakati Kebaso ameshambuliwa na wafu wame
rushiana vitu.
 
Hivi Kenya hakunaga POLICE na FFU wanaomwagwa mtaani kama siafu mpaka kuwafanya waandamanaji wafike sehemu nyeti kama Bungeni.?
 
Wakenya walikusanyika kwa wingi na kuanza kuimba kwa nguvu "RUTO MUST GO." Mkutano huo ulilenga kujadili kufukuzwa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, na umeshuhudia wananchi wakionesha hasira na kutoridhishwa na uongozi wa sasa.
Cheche kali za kisiasa na wakati mwingine vurugu zilishuhudiwa huku Wakenya katika kaunti zote 47 wakitoa maoni kuhusiana na hoja maalum inayolenga kumfurusha Naibu Rais Rigathi Gachagua madarakani.

Katika ukumbi wa Bomas, kaunti ya Nairobi, kikao cha utoaji maoni kilisitishwa baada ya vurugu kuzuka ukumbini.

Hii ni baada ya mwanaharakati Morara Kebaso kubebwa kwa nguvu na kufukuzwa eneo hilo punde alipowasili kutoa maoni yake.

Pia, Soma: Rigathi Gachagua adinda kujiuzulu, asema bila yeye Ruto asingeingia Ikulu

Raia walilalamika vikali, wakidai waandaji walikataza wapinzani wa Gachagua kutoa maoni. Katika kaunti ya Nakuru, kikao cha utoaji maoni kilisitishwa baada ya kudaiwa kuwa hojaji zilikuwa nakala na si halisi. Wafuasi wa Gachagua walidaiwa kuzuiwa kuingia ukumbini, hali iliyosababisha watu kuingia mitaani kulalamikia hali hiyo.

Hoja maalum ya kutaka Gachagua afurushwe iliwasilishwa bungeni na mbunge wa Kibwezi Magharibi, Eckomas Mwengi Mutuse, ikiwa na mashtaka 11, ikiwemo ukabila na ubadhirifu wa mali ya umma. Wakenya wameruhusiwa kutoa maoni kwa mujibu wa kifungu 118 cha katiba.

Jaribio la Naibu Rais kuzuia zoezi la ukusanyaji maoni lilishindikana, na kesi hiyo itatajwa Oktoba 9. Wakati huo, wabunge wamesubiri kusikiliza hoja ya Mutuse na kuamua kama kumtimua au kumweka Gachagua madarakani. Ili hoja ipite, wabunge 233 wanahitajika kuiunga mkono, huku wabunge 291 tayari wamesaini kutaka Gachagua afukuzwe.

Soma:
--> Gachagua akana kudai Ksh.8B ili akubali kuachia nafasi ya Naibu Rais wa Kenya
--> Gachagua awaonya Wabunge: Mmekula hadi mmevimbiwa sasa mnawatapikia Wananchi, kuweni na Heshima basi!
Kenya inaingia kwenye machafuko ya kikabila very soon.

Game of Thrones
 
Tumewachoka sasa na drama zao,waivamie ikuku ndio tutajua wako serias
 
Back
Top Bottom