Wakenya waliokuwa wakielekea Dubai wakamatwa na vyeti gushi vya corona

Wakenya waliokuwa wakielekea Dubai wakamatwa na vyeti gushi vya corona

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Uwanja wa ndege wa  kimataifa wa Jomo Kenyatta
Maafisa wa uwanja wa ndege nchini Kenya wamewakamata wasafiri 21 ambao waliokuwa wakielekea mjini Dubai, katika Muungano wa falme za kiarabu (UAE), kwa kutumia vyeti gushi vya Covid-19.

Wasafiri waliokamatwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.

Wasafiri hao wamekamatwa wakati wa msako wa vyeti hivyo uliokuwa ukifanyika katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta katika mji mkuu, Nairobi.

Hii inakuja saa kadhaa baada ya UAE kupiga marufuku utoaji wa vibali vya kusafiria (visa) kwa wasafiri wanaotoka nchi kadhaa ikiwa ni pamoja na Kenya.

Vyombo vya habari nchini Kenya vinaripoti kuwa marufuku hiyo iliwekwa baada ya wasafiri kutoka Kenya kupatikana na vyeti gushi vya Covid-19 walippowasili katika taifa hilo la Ghuba.

Kenya imekuwa ikirekodi ongezeko la maambukizi ya Covid-19, huku jumla ya watu wenye maambukizi ikifikia 80,102 vikiwemo vifo vya watu 1,427.
 
Ni wasafiri kutoka kenya au ni Wakenya?

Coz unaweza kua mrundi ila ukaanzia safari ya kwenda uae kutokea Kenya
 
Back
Top Bottom