Wakenya watawala mbio za Boston marathon

Kenyan

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2012
Posts
414
Reaction score
314
Mkenya Hellen Obiri ameshinda mbio za masafa marefu za Boston Marathon baada ya kuandikisha muda wa 2:21:38.

Bingwa huyo wa olimpiki katika mbio za mita 5000 alishiriki marathon kwa mara kwanza mwaka uliopita jijini New York na kushika nafasi ya sita.

Kwa upande wa wanaume, Evans Chebet ameteta taji lake la mbio hizo za Boston kwa kuandikisha muda wa 2:05:54 huku Gabriel Gaey kutoka Tanzania akimaliza wa pili kwa kutumia saa 2:06:04

Washindi watapenda kitita cha pesa kama ifuatavyo pesa za Kenya:

1. 20,157,000

2. 10,078,500

3. 5,375,200

4. 3,359,500

5. 2,418,450
 
Tunamshukuru Mama Samia kwa huu ushindi wa mwanariadha Geay. CCM iliahidi sasa inatenda.
 
Ksh au usd?
 
Wakenya kuweni makini, Marathon ndio mchezo pekee uliobaki mikononi mwenu, hata huko tumeanza kampeni ya kuwatawala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…