AbaMukulu
JF-Expert Member
- Jan 1, 2018
- 2,053
- 3,586
Msemo wa Hakuna Matata ni maarufu sana ukanda huu wa Afrika Mashriki hasa zile sehemu ambazo zinatembelewa sana na watalii.
Msemo huu ulipata umaarufu kwa ngazi za kimataifa kupitia filamu ya Lion King ambapo kulikuwa kuna wimbo maalumu kabisa uitwao hakuna matata.
Kampuni ya kutengeneza filamu iitwayo Walt Disney karibuni imesajili Hatimiliki ya msemo wa HAKUNA MATATA. Kampuni hii imetengeneza filamu ya Iion King.
Hali hii imesababisha mtifuano kwenye mitandao ya kijamii nchini Kenya kuhusu hasa nani anastahiki kupata Hatimiliki kwenye msemo huo.
Historia fupi ya "Hakuna Matata"
Msemo ulipata umaarufu kwenye eneo la Afrika Mashariki baada ya bendi ya Them Mushrooms kutoa kibao matata kilichoenda kwa jina la 'Jambo Bwana'. Hiyo ilikuwa ni mnamo 1982.
Jambo Bwana ya Them Mushrooms
Ndani ya kibao hicho msemo wa Hakuna Matata umetumika sana.
Ndani ya 1983, bendi maarufu ya Bony M ilitengeneza kibao hicho kwa mahadhi ya lugha ya kiingereza lakini sehemu halisi ya kiitikio ilibakizwa kwa lugha ya Kiswahili.
Jambo Bwana ya Bony M
Mwaka 1994, ulitengenezwa wimbo wa HAKUNA MATATA ambao ulitumika kwenye filamu ya Lion king.
Hakuna Matata kwenye Lion King
2018,Walt Disney walijiandikisha kama wamiliki wa msemo huu wakati wakiwa kwenye mchakato wa kuirudia filamu ya Lion King.
Wazungu walituibia rasilimali sasa wameamua kujimilikisha misemo yetu lakini HAKUNA MATATA
Msemo huu ulipata umaarufu kwa ngazi za kimataifa kupitia filamu ya Lion King ambapo kulikuwa kuna wimbo maalumu kabisa uitwao hakuna matata.
Kampuni ya kutengeneza filamu iitwayo Walt Disney karibuni imesajili Hatimiliki ya msemo wa HAKUNA MATATA. Kampuni hii imetengeneza filamu ya Iion King.
Hali hii imesababisha mtifuano kwenye mitandao ya kijamii nchini Kenya kuhusu hasa nani anastahiki kupata Hatimiliki kwenye msemo huo.
Historia fupi ya "Hakuna Matata"
Msemo ulipata umaarufu kwenye eneo la Afrika Mashariki baada ya bendi ya Them Mushrooms kutoa kibao matata kilichoenda kwa jina la 'Jambo Bwana'. Hiyo ilikuwa ni mnamo 1982.
Jambo Bwana ya Them Mushrooms
Ndani ya kibao hicho msemo wa Hakuna Matata umetumika sana.
Ndani ya 1983, bendi maarufu ya Bony M ilitengeneza kibao hicho kwa mahadhi ya lugha ya kiingereza lakini sehemu halisi ya kiitikio ilibakizwa kwa lugha ya Kiswahili.
Jambo Bwana ya Bony M
Mwaka 1994, ulitengenezwa wimbo wa HAKUNA MATATA ambao ulitumika kwenye filamu ya Lion king.
Hakuna Matata kwenye Lion King
2018,Walt Disney walijiandikisha kama wamiliki wa msemo huu wakati wakiwa kwenye mchakato wa kuirudia filamu ya Lion King.
Wazungu walituibia rasilimali sasa wameamua kujimilikisha misemo yetu lakini HAKUNA MATATA