Nyakijooga
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 276
- 473
Wakili Paul Kisabo ameeleza kuwa amemuandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) kutaka majibu ya utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuhusu upelelezi wa walipo Deus Soka, Jacob Mlay, Frank Mbise.
View: https://youtu.be/vEgMlh8IoFI?si=ytSt2Uo8IZ_rnAVx
Wakili huyo ambaye alifungua Kesi ambayo ilitolewa uamuzi na Mahakama ameeleza "Februari 07, 2025 nilimuandikia barua IGP wa Tanzania kutaka majibu ya utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuhusu upelelezi wa walipo Deus Soka , Jacob Mlay, Frank Mbise. Barua hiyo ameipokea Feb 10, 2025."
"Ikumbukwe kwamba Agosti 22, 2024 nikiwa wakili wa Soka, nilifungua shauri la jinai namba 23998 kudai Deus Soka , Jacob Mlay, Frank Mbise waachiliwe huru baada ya kutekwa. Agosti 28, 2024 Mahakama Kuu ya Tanzania masijala ya Dar es Salaam iliwaagiza Jeshi la Polisi kufanya upelelezi wa kuwatafuta walipo hawa ndugu zetu, sasa ni zaidi ya miezi 5 hakuna taarifa rasmi kuhusu utekelezaji wa hukumu hiyo."
Amesisitiza kwamba "Maamuzi ya Mahakama Kuu ni lazima yatekelezwe na yanapaswa kutekelezwa kikamilifu. Kwa mujibu wa Sheria za Tanzania ni kosa kutokutekeleza maamuzi ya Mahakama Kuu ya Tanzania." amesema Wakili Paul Kisabo
View: https://youtu.be/vEgMlh8IoFI?si=ytSt2Uo8IZ_rnAVx
Wakili huyo ambaye alifungua Kesi ambayo ilitolewa uamuzi na Mahakama ameeleza "Februari 07, 2025 nilimuandikia barua IGP wa Tanzania kutaka majibu ya utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuhusu upelelezi wa walipo Deus Soka , Jacob Mlay, Frank Mbise. Barua hiyo ameipokea Feb 10, 2025."
"Ikumbukwe kwamba Agosti 22, 2024 nikiwa wakili wa Soka, nilifungua shauri la jinai namba 23998 kudai Deus Soka , Jacob Mlay, Frank Mbise waachiliwe huru baada ya kutekwa. Agosti 28, 2024 Mahakama Kuu ya Tanzania masijala ya Dar es Salaam iliwaagiza Jeshi la Polisi kufanya upelelezi wa kuwatafuta walipo hawa ndugu zetu, sasa ni zaidi ya miezi 5 hakuna taarifa rasmi kuhusu utekelezaji wa hukumu hiyo."
Amesisitiza kwamba "Maamuzi ya Mahakama Kuu ni lazima yatekelezwe na yanapaswa kutekelezwa kikamilifu. Kwa mujibu wa Sheria za Tanzania ni kosa kutokutekeleza maamuzi ya Mahakama Kuu ya Tanzania." amesema Wakili Paul Kisabo