Pre GE2025 Wakili Madeleka: Kisutu kuna danadana za kumnyima haki ya dhamana Dkt. Slaa tumeenda Mahakama Kuu

Pre GE2025 Wakili Madeleka: Kisutu kuna danadana za kumnyima haki ya dhamana Dkt. Slaa tumeenda Mahakama Kuu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Jopo la Mawakili wanaomwakilisha Dkt.Wilbrod Slaa kwenye Kesi ya Jinai Namba 993 ya Mwaka 2025 wamewasilisha maombi mawili kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ambapo ombi la kwanza ambalo limesikilizwa leo Januari 23, 2025 walikuwa wanapinga kunyimwa dhamana kwa mteja wao.

Katika ombi la pili ambalo litasikilizwa Januari 24, 2025 kwenye Mahakama hiyo wanapinga uhalali wa kesi ya msingi ambayo ipo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Jopo likiongozwa na Wakili Peter Madeleka pamoja na Wakili Hekima Mwasipu wamewasilisha hoja zao kupinga kunyimwa dhamana kwa mteja wao ambaye alifikishwa kwenye Mahakama ya Kisutu kwa mara ya kwanza January 10, 2025.

Jopo hilo limeeleza Mahakama Kuu kwamba ni haki ya mshtakiwa kupewa dhamana, ambapo wameiomba Mahakama Kuu kufanya mapitio ya kilichofanyika Mahakamani Januari 10,13 na 17, 2025 kwenye kesi ya msingi ili kubaini ukiukwaji wa taratibu uliomfanya mshtakiwa kuendelea kuwekwa ndani bila kupata haki yake ya msingi ya kupewa dhamana.

Hata hivyo, Mawakili wa Jamhuri nao wamewasilisha hoja kindhani juu ya utaratibu uliozingatiwa na kufanya mtuhumiwa kuendelea kuwa ndani bila dhamana.

Kufuatia mawasilisho ya hoja kwa pande zote mbili ambayo yamechua takribani saa nne mbele ya Mh.Jaji Arnold Kirekiano, uamuzi wa ombi hilo umepangwa kutolewa Jumatatu Januari 27, 2025 Saa tatu asubuhi.

Hata hivyo, mshtakiwa Dkt. Slaa amerejeshwa tena rumande huku maombi hayo yakiendelea kusikilizwa.
 
Jopo la Mawakili wanaomwakilisha Dkt.Wilbrod Slaa kwenye Kesi ya Jinai Namba 993 ya Mwaka 2025 wamewasilisha maombi mawili kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ambapo ombi la kwanza ambalo limesikilizwa leo Januari 23, 2025 walikuwa wanapinga kunyimwa dhamana kwa mteja wao.

Katika ombi la pili ambalo litasikilizwa Januari 24, 2025 kwenye Mahakama hiyo wanapinga uhalali wa kesi ya msingi ambayo ipo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Jopo likiongozwa na Wakili Peter Madeleka pamoja na Wakili Hekima Mwasipu wamewasilisha hoja zao kupinga kunyimwa dhamana kwa mteja wao ambaye alifikishwa kwenye Mahakama ya Kisutu kwa mara ya kwanza January 10, 2025.

Jopo hilo limeeleza Mahakama Kuu kwamba ni haki ya mshtakiwa kupewa dhamana, ambapo wameiomba Mahakama Kuu kufanya mapitio ya kilichofanyika Mahakamani Januari 10,13 na 17, 2025 kwenye kesi ya msingi ili kubaini ukiukwaji wa taratibu uliomfanya mshtakiwa kuendelea kuwekwa ndani bila kupata haki yake ya msingi ya kupewa dhamana.

Hata hivyo, Mawakili wa Jamhuri nao wamewasilisha hoja kindhani juu ya utaratibu uliozingatiwa na kufanya mtuhumiwa kuendelea kuwa ndani bila dhamana.

Kufuatia mawasilisho ya hoja kwa pande zote mbili ambayo yamechua takribani saa nne mbele ya Mh.Jaji Arnold Kirekiano, uamuzi wa ombi hilo umepangwa kutolewa Jumatatu Januari 27, 2025 Saa tatu asubuhi.

Hata hivyo, mshtakiwa Dkt. Slaa amerejeshwa tena rumande huku maombi hayo yakiendelea kusikilizwa.
Sema kwa kipindi hiki wangemuachia tu apambane na mzee mwenzie Wasira
 
Wamwachie apambane na wasira shida iko wapi hapo, tunatamani mtifuano wa hoja
 
Back
Top Bottom