Pre GE2025 Wakili Mpanju: Wanawake mjitokeze kugombea nafasi za uongozi kwenye Uchaguzi Mkuu

Pre GE2025 Wakili Mpanju: Wanawake mjitokeze kugombea nafasi za uongozi kwenye Uchaguzi Mkuu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kwenda kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi mkuu utakafoanyika mwaka huu.

Akizungumza katika Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Kanda ya Kusini linalofanyika wilaya ya Nachingwea, Mkoa wa Lindi, Mpanju amesema kuna umuhimu wa nafasi kujiamini na kuchukua hatua za kuwania nafasi za uongozi.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

"Wanawake ni chachu ya maendeleo wamekuwa mhimhili na chachu ya maendeleo ya taifa naomba mjitokeze mara kipyenga kitakapolia jitokezeni nendeni mkachukue fomu gombeeni nafasi za udiwani gombeeni nafasi za ubunge" amesema Mpanju

Aidha amewataka kujiamini kwani tayari kuna mifano ya viongozi walioshika nyadhifa na kuonyesha mafanikio makubwa.

"Na mfano mzuri ni Mheshimwa Rasi Dkt. Samia Suluhu Hassan, Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson na Msajili mkuu wa Mahakama Eva Nkya chukueni fomu mshiriki kwenye kuamua na kupanga mstakabali wa taifa letu"

 
Back
Top Bottom