TANZIA Wakili msomi Judith Mushumbusi hatunae tena

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
R.I.P Wakili Msomi Judith Mushumbusi

Raha ya milele umpe Ee Bwana na mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa amani tukaonane tena katika asubuhi ile iliyo njema na Kuu.

NOTE: Tuendelee kujikinga na Corona! Maisha sio mali ya serikali unayoishabikia, sio mali ya Kanisa unaloabudu, sio mali ya Kiongozi wako wa kidini wala sio mali ya chama chako. Maisha ni mali yako!

Niwarai tu tena kwamba kama hujaumizwa na Corona basi mshukuru Mungu jiepushe kutoa matamko yanayowaumiza walioumizwa na Corona.

 
Aise bado kabint kabichi kabisa,daa,! kifo ni njia ya kila mmoja,ila kinapotokea kinaumiza sana.rip wakili.pole kwa wanafamilia
 
RIP jamani; Mwenyezi Mungu amrehemu. Mahakamani kuna kila aina ya mikusanyiko hatari sana. Tupate Hali halisi ya magerezani pia maana wale ndio kabisa hawana wa kuwasemea.
 
Watanzania fanyeni mazoezi, mwili unatakiwa uchangamshe.

Jitahidini hata utembee km 2 kwa siku.

Huu ugonjwa hauna madhara kwa watu wanaoushughulisha mwili.

Mbona mama ntilie, machinga, wapiga debe, mafundi ujenzi, wanamichezo, dereva bajaji na bodaboda hawafi?

Sababu miili yao haikai kizembe kama hawa wanaokaa kwenye viyoyozi ofisini.

Note:
Tangu Corona ianze hakuna mwanamichezo duniani aliyefariki.

Wanaupata ila hauwadhuru
 
Corona ipo ila tusiiwatie watu hofu

Note tujikinge Corona ipo ila sio kwa ukubwa unaozungumzwa
 
Upepo wa neno "R.I.P" unavuma kama ilivyotabiriwa; ila tusiogope ni kawaida !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…