Pre GE2025 Wakili Mwanaisha Mndeme atangaza kugombea Ubunge jimbo la Kigamboni kupitia ACT Wazalendo. Ataweza kumrithi Ndugulile?

Pre GE2025 Wakili Mwanaisha Mndeme atangaza kugombea Ubunge jimbo la Kigamboni kupitia ACT Wazalendo. Ataweza kumrithi Ndugulile?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakili Mwanaisha Mndeme ambaye ni Katibu wa Idara ya Mambo ya Nje ya ACT Wazalendo, na Waziri Kivuli Viwanda na Biashara wa chama hicho, leo tarehe 6 Februari 2025 ametangaza nia ya kugombea ubunge wa Jimbo la Kigamboni mkoani Dar es Salaam katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Wakili Mndeme amesema atahakikisha changamoto zote za Wanakigamboni zinatatuliwa hasa suala la barabara na usafiri lakini pia kama mwanasheria, atahakikisha suala la ardhi kwa Wanakigamboni analishikia bango kwa kuwa ndilo tatizo kubwa kwao.

Soma pia: Waziri Kivuli wa ACT Wazalendo Ndolezi Petro atangaza nia ya kugombea Ubunge jimbo la Kigoma Kusini

Wakili mndeme.png

Source: Jambo TV
 
Huyu dada alipambana sana 2020 sema hakuna resources na chama hakikuwa na fedha. Cha msingi sana kati ya sasa na Oktoba upinzani uraise funds za kutosha maana kampeni ni hela kingine waungane ili waachiane majimbo ikiwezekana waweke efforts kwenye majimbo tofauti sio ambapo ACT anasimama na chadema naye asimame.

Otherwise reforms zikifanyika kwa pressure ya upinzani basi nina hakika ccm itapiteza majimbo mengi sana otkoba
 
Namshauri aende Chadema atafanikiwa.

Act hawezi kufanikiwa.
Chama cha kinafki chenye viongozi mapandikizi ya CCM.
 
Back
Top Bottom