Wakili Sungusia: Haki Jinai haina utaratibu wa mtu aliyewekwa muda mrefu Mahabusu kudai FIDIA pindi anapoachiwa huru au DPP kutoendelea na kesi

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Wakili msomi Halord Sungusia amesema sheria za Tanzania hazijaweka utaratibu wa mtu aliyewekwa mahabusu kwa muda mrefu kudai fidia pindi itakapobainika aliwekwa mahabusu kimakosa, akishinda kesi au DPP akiamua kutoendelea na kesi.

Hii imeumiza watu wengi sana lakini ndivyo utaratibu wa sheria za Tanzania ulivyo kwasasa, amesema Sungusia.

Chanzo: BBC Dira ya Dunia!
 
Nafikiri hili suala linahitaji watu matata kama Marehemu Mtikila kulifikisha mahakamani.
 

Ndio maana kila siku upelelezi haujakamilika... wangekuwa wanalipa faini, huu ujinga ungeisha...
 
Mpaka hapo mbowe anaachiwa wameanza kutengeneza mazingira ya kujinasulia
 
Hizi sheria za kishetani ndizo zilitakiwa kubadilishwa haraka lakini watawala kwa sababu wanafurahia ushetani, na kuna wakati ikulu anakuwepo shetani (maneno ya Askofu Mwingira), wanaona ni sahihi kuiweka nchi nzima chini ya ushetani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…