Wakoloni hawakuwa wanyanyasaji kama inavyosadikika

Wakoloni hawakuwa wanyanyasaji kama inavyosadikika

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
4,580
Reaction score
7,943
Habari wanabodi!
Nimeona niliweke sawa jambo hili lililohusu ukoloni Tanzania (Tanganyika) kuanzia utawala wa Kijerumani miaka ya 1880's- 1918 baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia na kisha utawala wa Mwingereza ulioanza mwaka 1919-1961 (wakati wa uhuru)

Kwa hakika watu huchanganya mafaili mawili, faili la enzi za utunwa na lile linalozungumzia ukoloni.

Enzi za ukoloni East Afrika, Tanganyika ikiwemo wakoloni/wazungu walitawala kwa misingi ya haki za binadamu, huku wakifuata sheria walizozitunga.

Yapo madhaifu madogomadogo yaliyojitokeza katika utawala wao ila hayakuwa makubwa sana, walihesabu nchi kama mali yao.

Kikwazo kikubwa kwa wananchi kilikuwa kodi za kichwa ambazo hata nchi mama kama Uingereza na Ujerumani kwa kipindi hicho ilikuwa ikitozwa kama kawaida; tena kwa kiasi kikubwa kidogo zaidi ya kile kilichotozwa kwa Watanganyika.

Waafrika wachache walioelimika waliwatumia Waafrika wenzao( non- educated persons) kuwashawishi hata wamwage damu zao kuung'oa utawala wa Kizungu ili wao washike nafasi za uongozi.

Nimeongea na vikongwe kadhaa kuwadadisi ikiwa kulikuwa na manyanyaso ya dhahiri kutoka kwa wakoloni wengi walishindwa kuniambia zaidi ya kodi ya kichwa ambayo ilikuwa fedha ya kiasi ambayo kila mtu huweza kuipata kwa wakati huo.
 
Pumba tupu
Mkishawanunulia wazee wenu pombe za machicha,tayari wana Divert story
 
Farao hakuwatesa wayahudi kama mussa alivyowaaminisha, ndo akili zako hizo za kizamani saaaana.
 
Hatuzungumzii utumwa ndugu.
Inaonyesha uelewa wako ni wa kiwango cha vumbi kama si changarawe.
Huoni kitendo cha wao kuja kututawala tayari ilikuwa sio sahihi?ulishawahi kuishi nao hao unawasifu hapa kwetu au kwao?

Hivi our good manners zinatoka kwao?
 
Mkuu mleta mada sijajua kana kuwa wewe ni mkoloni au vip?

Tangu tupate Uhuru mwaka 1961 mpaka Leo ni yapata miaka 57 mtoto aliyezaliwa kipindi hicho ndo umri wake.

Lkn uelewe Tanganyika was under Mandate baada ya vita ya pili vya dunia 1945 ambayo yapata kuwa 73 iliyopita mtoto aliyezaliwa ni miaka hiyo 73 .

Under mandate maana yake wakoloni waliopewa ilikuwa ni kuandaa wazawa wachache ili waje wawe watawala, kuwatawala wenzao ili wao watumie dividing rule ili waendelee kututawala kwa njia ya wenzetu.

Lkn ni wazi kabisa mambo yanayotendeka sasa tunatukanana sisi lkn tujue hizi ni athari za wakoloni kututengea tabaka na kutufanya turndelee kuwa watumwa ndani ya nchi zetu

Napinga kabisa kuwa wakoloni hawakuwa wanatesa kama jinsi historia inavyobaini
 
Dhana ya nchi kupata uhuru na kuweza kujitawala ni nzuri sana, na inathamani ya kupiganiwa kwa jasho na damu. Lakini kwa Africa ni kama laana, wale waliongoza harakati hizo baada ya kupata madaraka wameishia kua kama wakoloni, na wengine wamekua wabaya kuliko hata wakoloni. Wanajiona kama ni wafalme ambao kutawala ni haki yao ya kuzaliwa.
Tanzania bado haijapata uhuru. Kwa bahati mbaya njia ya mkato ya kupata uhuru kamili ni vita na sadaka ya damu za wenye nchi, baada ya kila mtu kuichoka vita basi hapo tutaweza kukaa meza moja na kukubaliana kifungu kwa kifungu nchi yetu iweje. Njia mbadala na ambayo ni sahihi ni kuruhusu demokrasia ya kweli, watu waweze kumchagua wamtakaye bila kundi fulani la manyang'au kuingilia na kuvuruga uchaguzi huku yakijifanya yanajua zaidi kipi ni bora kwa nchi.
 
Back
Top Bottom