Wakulima na changamoto / Farmers with challenges?

Wakulima na changamoto / Farmers with challenges?

Samsara

Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
5
Reaction score
1
Greetings,
I often hear how difficult is for Farmers in Tanzania, but what exactly are the really challenges that Farmers are encountering?

Where main problems that they are struggling with?

What could Tanzanians do to somehow contribute and support each other with mutual benefit and to improve the economy system? From Farmers, supply chain, to the end consumers?

I would like to hear views.

Thanks and good day.

----------------------------------------------------------------------------------

Salamu,
Mara nyingi husikia jinsi Wakulima wanyopata ugumu Tanzania na matokeo yake ina zorotesha maelendeleo.
Lakini nini hasa kinacho wakabili Wakulima?

Ni changamoto zipi wanazo kutana na kupambana nazo?

Je Watanzania wanawezaje kusaidiana kwa namna yoyote katika kuchangia na kuboresha uchumi na kwa faida ya wote? Kuanzia Wakulima, usambazaji, mpaka watumiaji wa mwisho?

Ningependa kuelewa zaidi and kusikia maoni yenu.

Asanteni sana na nawatakia siku njema.
 
Kwa hiyo Mkuu unataka tukusaidie kujibu assignment yako ya extension? (natania Mkuu). Ngoja waje wenyewe wakusaidie!!
 
Job K - Umeshindwa kweli kuchangia hata wazo moja? Hapana sikubali Mkuu 🙂
 
Greetings,
I often hear how difficult is for Farmers in Tanzania, but what exactly are the really challenges that Farmers are encountering?

Where main problems that they are struggling with?

What could Tanzanians do to somehow contribute and support each other with mutual benefit and to improve the economy system? From Farmers, supply chain, to the end consumers?

I would like to hear views.

Thanks and good day.

----------------------------------------------------------------------------------

Salamu,
Mara nyingi husikia jinsi Wakulima wanyopata ugumu Tanzania na matokeo yake ina zorotesha maelendeleo.
Lakini nini hasa kinacho wakabili Wakulima?

Ni changamoto zipi wanazo kutana na kupambana nazo?

Je Watanzania wanawezaje kusaidiana kwa namna yoyote katika kuchangia na kuboresha uchumi na kwa faida ya wote? Kuanzia Wakulima, usambazaji, mpaka watumiaji wa mwisho?

Ningependa kuelewa zaidi and kusikia maoni yenu.

Asanteni sana na nawatakia siku njema.
Hili somo ni pana sana. Mawazo yangu yatahusu changamoto zinazowakabili wakulima wadogo wa vijini na si wakulima wakubwa wa kibiashara (ambao hatunao wengi hapa Tanzania). Hizi ni baadhi ya changamoto:

1. Ukosefu wa elimu kuhusu kilimo bora: Zamani (1960s, 70s and somehow 80s) elimu hii ilkuwa inatolewa na vyama vya ushirika ambavyo vilikuwa na extension officers vijijini. Hata serikali ilikuwa inaajiri ma-Bwana Shamba. Sasa hivi kama wapo ni wachache na hawatimizi wajibu wao. Kulikuwa na machapisho na hata vipindi vya redio ambavyo kwa sasa hakuna.

2. Ukosefu na uaghali wa vitendea kazi: Vifaa kama matrekta na pembejeo ni aghali mno kwa mkulima mdogo. Hata mifumo iliyowekwa na serikali kama vocha za bembejeo na kilimo cha mkataba vinamkandamiza mkulima badala ya kumsaidia. Wanaofaidika ni mawakala na walanguzi.

3. Ukosefu na vikwazo vya masoko: Wakati serikali inasema inatekeleza sera za soko huria kwa mkulima mdogo imemuwekea vikwazo kwa kumzuia asiuze kwa uhuru kama wafanyabiashara wengine. Kuna dhana kuwa wakulima wadogo hawazalishi kibiashara lakini hiyo si kweli. Nao wanaingia gharama za uzalishaji na hivyo wanahitaji kurudisha gharama zao na kupata ziada/faida.

4. Ukosefu wa vyanzo vya mitaji: vyombo rasmi vya kifedha haviwakopeshi wakulima moja kwa moja kwa sababu hawana mali za kuweka kama dhamana. Hawana hati za ardhi zao. Mikopo inayochukuliwa na vyama vya ushirika nayo inakuwa mzigo kwa wakulima kwa sababu inafujwa na watendaji lakini mwishowe wakulima wanalazimishwa kulipa kwa kukatwa fedha kwenye mauzo ya mazao yao.

5. Urasimu wa Uendeshai Kilimo wa Kinyonyaji: Kuna ngazi katika uendeshaji hasa unaohusu mazao makuu ya kibiashara ambazo si za lazima ila zimewekwa kwa maslahi ya watu au makundi fulani. Kwa mfano, kwenye zao la Kahawa kuna chama cha msingi cha ushirika, kunafuatia chama kikuku cha ushirika, kunafuatia chama cha kilele (apex) na bila kusahahu Bodi ya Kahawa. Kila ngazi inamega kutoka kwenye bei ya zao kimataifa. Kinachomfikia mkulima ni kidogo mno. Nchi jirani za Kenya na Uganda hazina upuuzi huu. Ndiyo maana katika Mkoa wa Kagera Kahawa nyingi inauzwa kimagendo Uganda kwa sababu bei zao ni nzuri.

6. Ushuru Katili kwa Mkulima: Sehemu nyingi katika nchi hii mkulima analipishwa ushuru hata akiwa anapeleka mkungu mmoja wa ndizi kwenye gulio la kijiji kwa ajili ya kujikimu. Lakini mawakala/walanguzi wa mazao vijijini hawalipi au wanalipa kidogo sana.

Zipo nyingi ila kwa leo naishia hapa.
 
Back
Top Bottom