Wakulima Songea waililia Serikali kwa kupanda Bei ya mbolea -24/02/2022

Wakulima Songea waililia Serikali kwa kupanda Bei ya mbolea -24/02/2022

nyamwingi

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2016
Posts
944
Reaction score
872
Katika utafiti nilioufanya leo hii tar. 24.02.2022 Bei za mbolea zimepanda Mara dufu lakin kwa bahati mbaya serikali hadi sasa ipo kimya huku ikijua wazi kuwa Ruvuma-Songea ndio mikoa inayozalisha kwa wingi zao la mahindi kiasi Cha kuweza kusaidia Tanzania kuwa na akiba ya chakula. Leo Bei za mbolea za kuzalishia zimefikia Kama ifuatavyo:

1. CAN-86,000(pia hapatikani)
2. SA-70,000 kutoka 64,500 siku wiki moja nyuma
3. NPK-91,500

Kwa bei hizi za mwaka huu zinawasababishia wakulima wa mkoa wa Ruvuma kutumia mbolea za asili ili angalau kupoza maumivu ya gharama.

Kama waziri wa kilimo ndgu Hussein Bashe yupo nchini hajaambatana na MH. Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassan basi kuna haja ya kuchukua hatua za dharuru za haraka katika kuhakikisha Bei ya mbolea ziwe rafiki kwa mkulima hali itayopelekea nchi kuwa na utulivu wa chakula cha kutosha.
 
Mkulima anatumia mavi ya kuku kuzalishia mahindi hii kweli ni mtihani kabisa
 
Unalima mahindi heka 20 hafu hupati pesa nzuri ila mtu anabustani tu ya nyanya heka moja au kabeji anakukimbiza kwa pesa...
 
Na maonyesho ya 8-8, wameyapiga pin, sijui kama yatarudi, sisi wakulima yalikuwa yanatupa contact sana za makampuni mbalimbali, sijui wakulima tunakikosea nini hiki chama kinachoshika haramu!??
 
Na maonyesho ya 8-8, wameyapiga pin, sijui kama yatarudi, sisi wakulima yalikuwa yanatupa contact sana za makampuni mbalimbali, sijui wakulima tunakikosea nini hiki chama kinachoshika haramu!??
Kumbe wamesitisha haya maonesho?
 
Kumbe wamesitisha haya maonesho?
Wameyasitisha.
Maonyesho ya 8-8, hayapo labda kama yatarudi mwaka huu!

Yakirudi wakulima hatutaki viingilio, yamegeuzwa biashara, haya yalitakiwa mapato yakusanywe tokea makampuni yanayodhamini na kushiriki, wakulima thingie bure na familia zetu!

Serikali unajua Sana kuharibu, mahudhurio yamekuwa hafifu Sana siku za karibuni mikoa ya kilimo, Ka Morogoro! Mpaka mabanda mengi huwa yanabakia wazi! Zamani watu walikuwa wanakimbilia kuchukua vibanda,
Hayo matozo hayaboreshi viwanja, vumbi washiriki mpaka kwenye kope, utadhani madereva trekta Au waswaggaa ng'ombe Simiyu! Hela zote zinazokusanywa MATUMBONI! WTF?

Makampuni ya kilimo na wakulima tuanzishe kitu kingine cheti! Umoja wetu, tuachane na maonyesho ya wanasiasa!
 
Back
Top Bottom