Sisi Wakulima wa Korosho tuliopo Mkunya Wilayani Newala Mkoani Mtwara tulipimishwa korosho tangu Oktoba na wengine Novemba 2024, hapo nikiwa namaanisha wale maafisa wa Serikali walikamilisha taratibu zote za manunuzi wakaondoka na mzigo kwa ahadi kuwa tutalipwa muda sio mrefu.
Kwa kawaida hela huwa inatoka ndani ya wiki mbili mara baada ya mchakato kama huo kufanyika lakini sasa hivi huu unaenda mwezi wa tatu sasa, kila siku danadana, hakuna majibu ya kueleweka kutoka Serikalini.
Wakati wa mchakato wa manunuzi tulikubaliana kuwa gharama ya kilo moja ya korosho ni Shilingi 3,000 lakini muda ulivyopita na wakulima kuanza kulalamika baadhi yetu wakaanza kuingiziwa malipo ambayo kimahesabu yalionesha wamelipwa Sh 2,200 kwa kilo.
Wale waliolipwa walipoona malipo yaliyoingizwa kwenye akaunti ni pungufu ndipo wakahoji kwa wale Maafisa wa Serikali waliopo Ghala Kuu ambao hata hawakusema kuwa malipo yatakuwa pungufu, ndio wakajibu kwa kusema eti kuna unyaufu wa korosho.
Sasa huo unyaufu unatoka wapi wakati mwanzoni tulikubaliana kila kitu kuwa kipo sawa na hadi bei tukapanga pamoja!
Matukio kama hayo huwa yanatokea mara kwa mara, tunachotaka kujua ni kweli hiyo hela iliyolipwa ni kweli imetoka hivyo Serikali Kuu au kuna watu wamecheza nayo hapo Katikati na mbona hawakutoa maelezo mapema?
Tunaomba Serikali pamoja na Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) watupe majibu ya kinachoendelea, je, ni kweli kuna unayufu wa korosho tulizowauzia? Mbona hawakusema awali? Mbona haikuwa hivyo wakati wa makubaliano ya mauzo na je sisi ambao hatujalipwa ‘status’ yetu ipoje?
Kuna wenzetu Wakulima wa Korosho katika Chama Kikuu cha Ushirika TANECU (Tandahimba & Newala cooprative Union) nao wanalia kama sisi
Tumehangaika kutafuta viongozi hususan Waziri mwenye dhamana lakini naye yupo kimya, Mkuu wa Wilaya anajua yupo kimya. Afisa Ushirika nae yupo kimya. kuna harufu isiyo ya kawaida. Tunaomba utupazie sauti tunaenda mwezi wa pili sasa tangu korosho zetu ziuzwe na hatujalipwa.
Wanachelewesha makusudi ili walipe bei pungufu ya ile waliyouza mizigo huo, maana ni madili ya watu haya na wakulima hawana pa kusemea.
Kwa kawaida hela huwa inatoka ndani ya wiki mbili mara baada ya mchakato kama huo kufanyika lakini sasa hivi huu unaenda mwezi wa tatu sasa, kila siku danadana, hakuna majibu ya kueleweka kutoka Serikalini.
Wakati wa mchakato wa manunuzi tulikubaliana kuwa gharama ya kilo moja ya korosho ni Shilingi 3,000 lakini muda ulivyopita na wakulima kuanza kulalamika baadhi yetu wakaanza kuingiziwa malipo ambayo kimahesabu yalionesha wamelipwa Sh 2,200 kwa kilo.
Wale waliolipwa walipoona malipo yaliyoingizwa kwenye akaunti ni pungufu ndipo wakahoji kwa wale Maafisa wa Serikali waliopo Ghala Kuu ambao hata hawakusema kuwa malipo yatakuwa pungufu, ndio wakajibu kwa kusema eti kuna unyaufu wa korosho.
Sasa huo unyaufu unatoka wapi wakati mwanzoni tulikubaliana kila kitu kuwa kipo sawa na hadi bei tukapanga pamoja!
Matukio kama hayo huwa yanatokea mara kwa mara, tunachotaka kujua ni kweli hiyo hela iliyolipwa ni kweli imetoka hivyo Serikali Kuu au kuna watu wamecheza nayo hapo Katikati na mbona hawakutoa maelezo mapema?
Tunaomba Serikali pamoja na Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) watupe majibu ya kinachoendelea, je, ni kweli kuna unayufu wa korosho tulizowauzia? Mbona hawakusema awali? Mbona haikuwa hivyo wakati wa makubaliano ya mauzo na je sisi ambao hatujalipwa ‘status’ yetu ipoje?
Kuna wenzetu Wakulima wa Korosho katika Chama Kikuu cha Ushirika TANECU (Tandahimba & Newala cooprative Union) nao wanalia kama sisi
Tumehangaika kutafuta viongozi hususan Waziri mwenye dhamana lakini naye yupo kimya, Mkuu wa Wilaya anajua yupo kimya. Afisa Ushirika nae yupo kimya. kuna harufu isiyo ya kawaida. Tunaomba utupazie sauti tunaenda mwezi wa pili sasa tangu korosho zetu ziuzwe na hatujalipwa.
Wanachelewesha makusudi ili walipe bei pungufu ya ile waliyouza mizigo huo, maana ni madili ya watu haya na wakulima hawana pa kusemea.