Wakuu naombeni ushauri

Wakuu naombeni ushauri

Jstar1

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2019
Posts
1,391
Reaction score
1,347
Kama kawaida binadamu hatuchoki kutafuta, ila baada ya kuwaza walau angalau niweze kupata kipato cha elfu 15 kwa siku namaanisha 450K kwa mwezi nkaamua niingie kwenye ufugaji wa kuku...

Natamani nifuge kuku wa mayai nichanganye na kuku wa kawaida, nina wasu wasi na eneo maana ni 42m*42M kwa makadri kama 1700SQM hapa dar es salsaam lipo sehemu yenye huduma zote ikiwemo umeme makazi na maji, ninao mda wa kutosha wa kuwahudumia.

wakuu kwa ilo eneo nipate kuku wangapi kwa kunipa hio faida... sina wasi wasi na mtaji nitapambana.
 
Kila la kheri, mkuu kwenye chakula cha kuku ukiitaji unaweza nicheki
 
Hongera mkuu. Eneo ulilonalo linatosha Sana kwa kuanzia. Hapo angalia Mambo ya bajeti ya:
1.banda (kulingana na mtaji wako).
2. Idadi ya kuku wa kuanza nao. Sikushauri Sana kwa layers wa kisasa maana wako delicate Sana na ni gharama kuwanunua na kuwatunza pia. Mavuno ni kuanzia miezi 5 na kuendelea.
3. Aina ya kuku wa kuanza nao. Iwe pure kienyeji, chotara, etc.
4. Ulinzi
5. Huduma za maji na umeme.
 
Back
Top Bottom