Wakuu, ni sahihi kujenga juu ya ‘beacon’ ya Serikali?

Wakuu kama kichwa Cha habari kinavyosema ni sahihi kujenga juu ya beacon ya halmashauribiliyowekwa Kwa ajili ya barabara ya mtaa maana Kuna jirani yangu anajenga hivi maana naona kama anatafuta ugomvi na serikali
Unauliza kama ni sahihi halafu unahitimisha kwamba anatafuta ugomvi na Serikali.

Hizi Shule sijui kama zinatusaidia au zinatuangamiza
 
Wakuu kama kichwa Cha habari kinavyosema ni sahihi kujenga juu ya beacon ya halmashauribiliyowekwa Kwa ajili ya barabara ya mtaa maana Kuna jirani yangu anajenga hivi maana naona kama anatafuta ugomvi na serikali.

View attachment 3173116
Logically wote mkijenga kwa kuikwepa beacon means mtazalisha vichochoro vya kufuga wezi na gesti bubu pia vijiwe vya bangi.
 
Kutoka kwenye bicon lazima muachiane Mita1 kila mmoja, Iwepo chochoro katikati kwaajili ya kupitisha miundombinu [Maji, umeme, Networkcables] huko mbeleni.
Hakuna hiyo sheria... hizo ni setbacks za namna ya kujenga nyumba sio ukuta au uzio

Kasome tena sheria ya mipango miji mkuu
 
Sehemiu yeyote iliyopimwa ina sehemu ya kupitisha miundombinu ipo maana kuna barabara za mitaa zenye urefu wa mita 15 hadi 25.

Hapo cha msingi ili jiwe asiliong'oe wakati wa ujenzi ,anaweza akaweka curve kulipisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…