Wakuu Nimeipenda hii gari Toyota Collora Fielder

Ngumu kumeza

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2012
Posts
577
Reaction score
354
Wakuu Heshima Kwenu,

Naomba kufahamishwa kidogo kuhusu hii gari,kwa upande wangu naona ni gari nzuri kwa muonekano ni ndoto zangu kuja kumiliki hii gari, maana naona haizungumzwi sana katika hili jukwaa.

Naomba kufahamishwa machache kuhusu hii gari:

- Changamoto zake
- Ulaji wake mafuta
- Upatikanaji wa vipuri
- Na mengineyo

Naomba kuwasilisha.

 
Hakuna haja ya kujiuliza mara2 hiyo gari iko poa kuanzia body yake, mashine na gear box, pia Corolla Fielder inatumia engine ya 1NZ ni engine zinazohimili Sana pia hiyo gari inafanana na pro box succeed.

Fasta Sana Fanya maamuzi wala haina haja ya kutafuta gari tofauti na hiyo
 
Unapokutana na brand yoyote ya toyota corolla iwe spacio, run x, fielder, axio etc hutakiwi kuuliza mara mbilimbili, we angalia shape tu kama inakupendeza machoni ichukue, hazinaga stress hizo gari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…