Kuna mtu anaitwa Nikola Tesla. Kwangu mimi huyu ndie mwanasayansi bora zaidi kuwahi kutokea.
Alikua na kipaji cha ajabu, yani jamaa aliweza kuvuna umeme out of thin air. Na yeye ndie msingi mkuu wa wireless communications tulizo nazo sasa.
Pamoja na kipaji chote hicho, jamaa alikufa akiwa masikini huku wajanja kama Thomas Edison wakipiga hela kutumia gunduzi na tafiti zake!
Sababu ni moja tu, alifeli kujitengeneza as a business brand, akamuuzia Thomas Edison patents za ugunduzi wake!
BACK TO THE TOPIC!
Mtu yeyote anaefuatilia hip hop hawez kuutilia shaka uwezo au kipaji cha Fid Q. He's simply on his own level.
Tatizo ni moja tu, haelewi nguvu ya brand katika biashara. Hapa naweka scenario kadhaa kuthibitisha hoja yangu.
1. Amekua mtu wa teams hapa karibuni.
Unaikumbuka remix ya Fresh akiwa na Diamond na Ray vanny? Unakumbuka vile Diamond aliutumia wimbo huu kumdis Ali kiba?
That was a very stupid move kwa upande wa Fid Q.
Kwa heshima yake hakutakiwa kuruhusu wimbo wake utumike kumdis msanii mwingine ambae yeye hahusiki na ugomvi wao.
Unadhani leo Ali Kiba anaweza kufanya collabo na Fid Q kirahisi baada ya kuisikiliza fresh remix? Mimi sijui, ila pale kaka mkubwa alichafua brand yake.
Kama vile bado haitoshi, sasa hivi kaamua kua team Clouds huku akitupiana maneno na Wasafi. Kulikua na ulazima gani? Kwani asingeweza kupiga show fiesta bila kutupiana maneno na Wasafi?
Je, unadhani anaweza
tena kufanya project na Wasafi? Mimi sijui, ninachojua ni kwamba kaka mkubwa kaharibu kwa Ali Kiba (collabo ya fresh) na sasa kaharibu kwa Diamond kwa sababu ya kupenda u-team usiokua na manufaa!
2. Amekua cheap sana ukimlinganisha na status yake!
More than ten years in the game, bado kaka anapiga show za laki kadhaa au milioni moja. Ni aibu kumuona Fid Q akiwa kwenye coaster anaenda kupiga show Muleba, unafikiri akina Young killer na Dogo janja wanajifunza nini kutoka kwake?
Kwa status yake angeitambua nguvu ya branding, sasa hivi angekua anaandaa shows zake then yeye ndie awaalike vijana akina Young killer waje kussuport.
Badala yake, ameamua kubanana nao kwenye coaster ya Tigo fiesta. PATHETIC!
MWISHO;
Tuko kwenye zama za ubepari. Kua na kipaji pekee haitoshi. Bila kua na mipango mizuri ya kibiashara utabaki kulalamika na kutoa ngoma kali ambazo hazikulipi.
Hebu waangalie Navy Kenzo, wakikutana na Ali kiba wanacheka nae then wanaingia studio wanatoa ngoma. Kesho wakikutana na Diamond wanacheka nae, wanaingia studio wanatoa ngoma. Habari ya teams wamewaachia wenyewe!
Kama Diamond asingeitambua nguvu ya branding pengine asingeweza kupiga mkwara miaka ile kwamba bila milioni kumi sifanyi show, wakati wenzie walikua wanapiga show za laki tatu.
Pengine na yeye angekua kwenye Coaster ya fiesta hivi sasa. Ngoja niishie hapa, maana maneno yanakuja tu kichwani hayaishi.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]