Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Wakuu wa wilaya za mkoa wa Tabora wameiomba serikali kuwajengea nyumba za kuishi pamoja na ofisi zao, wakieleza kuwa kwa sasa wanatumia majengo chakavu na ya zamani. Baadhi ya majengo hayo hujaa maji pindi mvua zinaponyesha, hali inayodhoofisha mazingira yao ya kazi na kuonyesha kutokuwepo kwa hadhi inayoendana na nyadhifa zao.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Wakuu hao wa wilaya, wakiwemo Mohamed Mtulyakwaku wa Wilaya ya Uyui, Mhandisi Deusdedith Katwale wa Wilaya ya Tabora, na Bi. Sauda Mtondoo wa Wilaya ya Igunga, walitoa hoja hiyo wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichojadili na kupitisha mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Wakuu hao wa wilaya, wakiwemo Mohamed Mtulyakwaku wa Wilaya ya Uyui, Mhandisi Deusdedith Katwale wa Wilaya ya Tabora, na Bi. Sauda Mtondoo wa Wilaya ya Igunga, walitoa hoja hiyo wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichojadili na kupitisha mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.