Pre GE2025 Wakuu wa wilaya Tabora: Nyumba tunazoishi haziendani na hadhi yetu

Pre GE2025 Wakuu wa wilaya Tabora: Nyumba tunazoishi haziendani na hadhi yetu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Wakuu wa wilaya za mkoa wa Tabora wameiomba serikali kuwajengea nyumba za kuishi pamoja na ofisi zao, wakieleza kuwa kwa sasa wanatumia majengo chakavu na ya zamani. Baadhi ya majengo hayo hujaa maji pindi mvua zinaponyesha, hali inayodhoofisha mazingira yao ya kazi na kuonyesha kutokuwepo kwa hadhi inayoendana na nyadhifa zao.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Wakuu hao wa wilaya, wakiwemo Mohamed Mtulyakwaku wa Wilaya ya Uyui, Mhandisi Deusdedith Katwale wa Wilaya ya Tabora, na Bi. Sauda Mtondoo wa Wilaya ya Igunga, walitoa hoja hiyo wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichojadili na kupitisha mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.

 
Kazi iendelee hata mkilala nje chapeni kazi!!

Unashindwaje kupanga nyumba classic ufanyekazi za serikali ipasavyo Hadi ulie lie!!?mbona walim,maaskari n.k wanapanga!!
 
Si wajenge nyumba zao au waendelee mtaani wakapange
Ikishindikana warekebishe zisivuje kwa gharama na faida zao.Washukuru hata wanakaa nyumba za bure zilizojengwa kwa kodi zetu wavuja jasho
 
🤣🤣🤣 mnavyolia hivyo ndivyo watumishi kama walimu wasio na hatia kabisa wameendelea kulia hivyo hivyo miaka dahari. Punguzeni siasa.
 
Back
Top Bottom