Wale backbenchers darasani tukutane hapa!

Wale backbenchers darasani tukutane hapa!

Curtis De Mi Amor

Senior Member
Joined
Jan 9, 2022
Posts
136
Reaction score
514
Habari za wakati! Natumai muwazima wa afya backbenchers wenzangu, kwakweli life mtaani limekuwa gumu mnoo imefikia hatua hata mtu akikusalimia unahisi ndio mchawi wako.

Vipi mabackbenchers wenzangu mmetoboa kimaisha? Maana nilikuwa mkorofi darasani sisikilizi walimu, mtoro mimi sasa najuta huku mtaani. Vipi nyie wenzangu mnateseka kama mimi au mnamaisha poa?

Screenshot_20220829-090709.jpg
 
Shule nyingi tz huwa wale wanaoongozaga darasan hukaa mbele au wale viongozi,wenye nidhamu hukaaga mbele,mimi nilipendelea zaidi kukaa nyuma ila karibu na katikati mwa darasa, yaani ni mtu wa nne au wa tano mbele ya wakaa nyuma kabisa,pale mbele kabisa kulia,kushoto na katikat au katikat mwa darasa hukaa wale wanaojiweza na wenye usongo na wale wambea wambea na wanoko...kwanza shule zote nilizosoma fimbo zilianziaga mbele pale,hadi mwalimu akifika kwangu tayari kashachoka,ilinisaidia kujiweka tayari na kujua idadi ya fimbo kabisaaaa ili nijiandae na mziki,sikupenda fimbo za mikono niliona fimbo za wadada hz,always maswali mengi huanza pale mbele Kama yale ya kufanya hesabu sasa ole wako ushindwe kufanya hesabu ubaoni utakiona,ngove popote ulipo jua kabisa watu walifel hesabu kwa sababu ya fimbo zako zisizo na maana(hili funzo kwa walimu wote fanyeni wanafunzi wawe marafiki zenu na siyo maadui,Mambo ya kupigana mayai viza na kuwekewa vinyes kwenye meza zenu mnayataka wenyew)...nyuma huko kulikuwa na mijbaba yenye ndevu hayo ndiyo mafaza wa backbencha,hawa jamaa walitulinda sana mtaani(njia za shule) na uwanjani, wengne sisi tulkuwa na miili ya kawaida ya utoto silaha zetu ni maandaz ya mungu tu(mawe)...sijui kwa sasa ila kipind kile watu bakibencha wengi wahun wa shule tu,watu wenye makosa mengi na wasiojiamin kwa kuwa wengi vichwani weupe,watu wanaokaa katikati tulikuwa tunawapa majibu ya uongo na kweli watu wa bakibencha, siku moja liliibiwa daftar la mahudhurio,likakutwa bakibencha limeandikwa matusi matupu,walitukanwa walimu wote hadi mlinz, mwenyekt wa wazazi pale skuli, ukapigwa mstari Yani kuanza pale kati nilipo hadi bakibencha tutoke tuende ofisini kuu ya walimu wote, kukaribia ofisini huko tulskia vilio tu ndani uwiiii Mara mama nakufaa,Yani pale mlangon kulkua na harufu ya miti ya mipera,mijohoro na mianzi mmmmhh,tuliingia mle ndani hali ilitisha maana tulikuta walimu wa kiume ndo wanakunja mashati na kufunga kamba za viatu,popote ulipo pale mwl.mapunda jua kabisa Kuna watu wanakudai bado wanakuapiza viapo hadi leo...
 
Back
Top Bottom