Craig
JF-Expert Member
- Feb 9, 2013
- 1,512
- 2,712
Habari za majukumu wadau, ni matumaini yangu kuwa wote tumeonesha uzalendo kwa kushiriki vizuri zoezi la sensa 2022.
Dodoso za sensa zimenifanya nikumbuke visa nilivyowahi kukutana navyo kwenye mahusiano. Ilikuwa mwaka 2010 enzi hizo nilikuwa naishi Masaki, Haille Selassie Road(nyumbani). Nyumba ya jirani yetu ilipangishwa, kutokana na ujirani mwema nilikuwa na mazoea na wakazi wa nyumba hiyo ambayo walipanga wachina, akiishi mkurugenzi wa mradi mkubwa wa barabara.
Sasa walikuwa na pisi moja kali ya kihaya(Kokunyumisa) kama chief cooker. Toto jeusii tii, bonge la guu, msambwanda upo, limepanda hewani, linaongea kichina na kingereza kizurii. Basi mzee mzima nikajipendekeza pisi ikanizoea nikatema sumu likanielewa tukaanzaa mahusiano.
Sasaa mpenzi wangu huyo hakuwahi kunitumia sms hata siku moja yeye ni kupiga tu, hata nikituma sms nipo bize job nitext yeye ni kupiga tuu. Chale zikanicheza baada ya mwezi huyu atakuwa illiterate?! Siku moja moja nikashika simu yakee kuingia kwa sms hakuna hata sms moja zaidi ya zile za networks provider na promotions.
Nikaendelea kuuchuna kadri anavyonizoea akawa ananiambia nimsomee sms zake kimasikhara mimi nikawa nimeshang'amua huyu demu ni ngumbaruu. Tuliendelea na mahusiano nikajifanya sijui. Basi nilikuwa kama sekretari wake maana hata kufanya miamala yake ya banking na simu nilifanya mimi, na demu alikuwa akiwapiga wachina dollars zao walizoshinda kwenye kamali.
Tulikuja kuachana mkataba wa Wachina ulipoisha akarudi kwao Kagera, nilimpenda sana. Kama na wewe uliwahi kukutana na kisa kama hiki tiririka.
Craig kwa sasa Kigoma.
Dodoso za sensa zimenifanya nikumbuke visa nilivyowahi kukutana navyo kwenye mahusiano. Ilikuwa mwaka 2010 enzi hizo nilikuwa naishi Masaki, Haille Selassie Road(nyumbani). Nyumba ya jirani yetu ilipangishwa, kutokana na ujirani mwema nilikuwa na mazoea na wakazi wa nyumba hiyo ambayo walipanga wachina, akiishi mkurugenzi wa mradi mkubwa wa barabara.
Sasa walikuwa na pisi moja kali ya kihaya(Kokunyumisa) kama chief cooker. Toto jeusii tii, bonge la guu, msambwanda upo, limepanda hewani, linaongea kichina na kingereza kizurii. Basi mzee mzima nikajipendekeza pisi ikanizoea nikatema sumu likanielewa tukaanzaa mahusiano.
Sasaa mpenzi wangu huyo hakuwahi kunitumia sms hata siku moja yeye ni kupiga tu, hata nikituma sms nipo bize job nitext yeye ni kupiga tuu. Chale zikanicheza baada ya mwezi huyu atakuwa illiterate?! Siku moja moja nikashika simu yakee kuingia kwa sms hakuna hata sms moja zaidi ya zile za networks provider na promotions.
Nikaendelea kuuchuna kadri anavyonizoea akawa ananiambia nimsomee sms zake kimasikhara mimi nikawa nimeshang'amua huyu demu ni ngumbaruu. Tuliendelea na mahusiano nikajifanya sijui. Basi nilikuwa kama sekretari wake maana hata kufanya miamala yake ya banking na simu nilifanya mimi, na demu alikuwa akiwapiga wachina dollars zao walizoshinda kwenye kamali.
Tulikuja kuachana mkataba wa Wachina ulipoisha akarudi kwao Kagera, nilimpenda sana. Kama na wewe uliwahi kukutana na kisa kama hiki tiririka.
Craig kwa sasa Kigoma.