Wale waliokuwa vikojozi na kutembezwa na magodoro yao mtaani

google helper

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2013
Posts
9,623
Reaction score
13,759
Wanajamvi, poleni sana na hali ya uhaba wa sukari maana hata ukiumwa hiyo corona mgonjwa wake uji, sasa uji bila sukari mgonjwa anaweza kufa kwa kweli.

Maisha yanakwenda kasi hatari kuliko kasi ya covid 19 wazeiya, ni vizuri kukumbushana mambo yaliyoteka uwanja tukiwa wadogo. Japo sijawahi kubebeshwa kidogoro kwa kuyamwaga ya haja, lakini mara nyingi nimeshuhudia waliobebeshwa.

Kama na wewe umewahi kubebeshwa kigodoro au ndugu yako wa karibu tupe mkasa, alivyoanza kuyamwaga, kuzoea kuyamwaga mpaka kumtoa nje na videbe huku kabeba heshima zake juu juu. Je, ilikuwa ni suluhu kwako au kwake?

Karibuni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa kikojozi lakini hizo anga za kimataifa sikuwahi kuzifikia kusema kweli 😂😂
 
Nilikuwa nashangaa na wimbo wa kikojozii na nguo kaitia moto na ndani kuna viroboto huyoooooo.

Sijui kama nimeupatia wimbo wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ha ha ha! Mkuu kufikia hatua ya kukariri huo wimbo ni dhahiri wewe ulishawahi bebeshwa godoro na kutembezwa na hapa unafanya vetting ya kuwatambua wenzako ili muunde chama😂
 
Ha ha ha! Mkuu kufikia hatua ya kukariri huo wimbo ni dhahiri wewe ulishawahi bebeshwa godoro na kutembezwa na hapa unafanya vetting ya kuwatambua wenzako ili muunde chama[emoji23]
Kuujua haina maana na mimi nilikuwa wa kimataifa na hapa sina haja ya kuficha kitu. Sijawahi imbiwa hivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mdogo wangu alikuwa anajikojolea mpaka akiamka anakuwa kama katoka kuogelea.
 
Hii ni tabia mbaya sana. Utotoni kila baada ya sherehe ilikuwa lazima nifanye mambo enzi zile nilikuwa mdhaifu wa soda lakini lazima nilale na ndugu yangu yoyote ili nimtegeshe. Samahani ndugu zangu mliobeba lawama kwa niaba yangu.
 
Nilikuwa nashangaa na wimbo wa kikojozii na nguo kaitia moto na ndani kuna viroboto huyoooooo.

Sijui kama nimeupatia wimbo wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app

Umepatia, ila unaanza na ile " kindumbwe ndumbwe afu wengine wanaitikia chaaliaa" inarudiwa na wanaitikia tena, then ndio inaendelea na hiyo extension yako.
Sema enzi hizo mtu mpaka apigiwe hilo songi ni lazima uwe legend afu kidizaini maskani wawe washaichoka tabia yako...


Alexander
 
alexander the great nimecheka sana kumbe kuna kindumbwe ndumbwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…