Wali wa sausage na mboga

Wali wa sausage na mboga

Elizabeth Dominic

Platinum Member
Joined
Dec 7, 2007
Posts
4,555
Reaction score
3,655
[h=3]JIFUNZE KUPIKA WALI WA SAUSAGE NA MBOGA MAJANI MCHANGANYIKO[/h]


JIFUNZE KUPIKA MBOGA MAJANI NA MCHANGAKO WA WALI NA SAUSAGE
MAHITAJI

3 vipande vya sausage
1 fungu la majani ya vitunguu
1 kitunguu kikubwa
100 gram njegere
500 gram chele basmati
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
JINSI YA KUANDAA FATIKLIA PICHA NA MAELEZO

Muda wa mapishi dakika 45
Muda wa maandalizii dakika 15


Huu ndio muonekano wa majani machanga ya vitunguu​


Kaanga vitunguu maji katika kikaango kwa kuweka mafuta ya kupikia kiasi​


Kisha ongezea majani mabichi ya vitunguu kama inavyoonekana katika picha​


Baada ya kukaanga kwa dakika mbili vitunguu pamoja na majani vitoe tu harufu na sio kuungua kubadilika rangi kisha weka mchele na endelea kukaanga​


Kaanga mchele kwa dakika 3 mpaka 4 kisha weka maji ya wastani yazidi mchele wako kiasi na uendelee kukoroga ili maji yachanganyike na mchele wako​


Kisha funikia na weka moto wa wastani ili wali wako uive taratibu​


Kisha chukua sausage zako na kata kata vipande vidogo​


Huu ndio muonekano wa vipande vya sausage baada ya kukata​


Kisha tupia juu ya wali wako njegere zilizochemshwa pamoja na vipande vyoote vya sausage​


Kumbuka kuendelea kukoroga ili kila kitu kichanganyike, pia kama mpenzi wa blue band au samli unaweza weka kiasi ili kuongeza ladha na harufu safiu sana katika wali wako​


Safi sana hapa kila kitu kimechanganyika na ninaimani baada ya dakika 45 wakli wako utakua umiva kama haujaiva basi ongezea maji kidogo na endelea kupika katika moto mdogo​


Ukimaliza pakua na mpatie mlaji chakula hiki kikiwa chamoto​

​

waandalie famili au hotelini kila atakae kula atafurahia sana

Kwa hisani ya Activechefblog
 
Leo mimi napika pishi hili. Muongozo wangu ni hii thread. Ahsante JF na members wote wa jukwaa hili la mapishi
 
Hapo kwenye kuweka maji vipi kama nitaweka tui nitakuwa nimekosea?
 
Back
Top Bottom