Walifikaje tarehe 7 Julai 1954 kuunda TANU na tunawaadhimishaje Wazalendo hawa?

Walifikaje tarehe 7 Julai 1954 kuunda TANU na tunawaadhimishaje Wazalendo hawa?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
WALIFIKAJE TAREHE 7 JULAI 1954 NA KUUNDA TANU NA TUNAWAADHIMISHAJE WAZALENDO HAWA?

Kuna mtaa Dar es Salaam sisi tulimezaliwa tumeukuta ukiitwa Stanley Street.

Baada ya kupatikana uhuru mtaa huu ukabadilishwa jina ukaitwa Aggrey Street kisha baadae wakati marehemu Kitwana Kondo alipokuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ukabadilishwa tena jina ukaitwa Mtaa wa Max Mbwana.

Mtaa huu umepewa majina ya watu maarufu watatu ambao wote wamekuwa na uhusiano wa kihistoria kuanzia Tanganyika hadi kufika Tanzania.

Henry Morton Stanley ndiye aliyetumwa kuja Tanganyika kumtafuta David Livingstone na akamkuta Ujiji. Dr. Aggrey alikuwa Mwafrika kutoka Ghana.

Umaarufu wake unatokana na kuwa yeye alikuja Tanganyika mwaka wa 1924 akiwa mmoja wa wajumbe wa kamisheni iliyokuja Tanganyika kuja kuchunguza elimu ya Waafrika.

Wajumbe wengine wote waliobakia katika kamisheni hii walikuwa Wazungu.

Kleist Sykes anaeleza katika mswada wa maisha yake alioandika kabala ya kifo chake mwaka wa 1949 kuwa alikuwa Dr. Aggrey ndiye aliyemtia hima aunde African Association.

Dr. Aggrey alimpa Kleist ushauri huu baada ya kutambua kuwa Waafrika wa Tanganyika hawakuwa na umoja wao, wakati Wazungu, Waasia na Waarabu wote tayari walikuwa na jumuia zao.

Katika mswada wake ule Kleist anasema kuwa Waafrika waliwakiishwa na Father Gibbons kutoka Misheni ya Minaki ambae yeye anastaajabu kwa kuwa hakuwa na uhusiano wala muiingiliano wowote na Waafrika wa Tanganyika.

Father Gibbons ni huyo wa kwanza waliosimama kushoto kwenye picha.

Kwa sifa hii ya Aggrey kuja Tanganyika akiwa Mwafrika msomi Jiji la Dar es Salaam wakabadili jina la Stanley na kuliweka jina la Dr. Aggrey.
Kitwana Kondo akiwa Meya wa Dar es Salaam akabadili tena jina la mtaa kutoka Aggrey ukaitwa Mtaa wa Max Mbwana.

Mzee Max Mbwana alikuwa mmoja wa wazee maarufu wa Dar es Salaam waliounga mkono harakati za kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Baraza la Wazee wa TANU 1955 katika picha hapo chini:

1. Abdallah Shomari (Tandamti Street No. 3)
2. Nassoro Kalumbanya (Simba str.)
3. Said Chamwenyewe (Aggrey/Congo Street)
4. Mtoro Ally (Muhonda Street.)
5. John Rupia (Misheni Kota)
6. Julius Nyerere( Pugu Sekondari)
7. Said Chaurembo (Congo/Mkunguni Street.)
8. Jumbe Tambaza( Upanga)
9. Sheikh Suleiman Takadir (Mafia /Swahili)
10. Dossa Aziz ( Mbaruku /Somali Kipande Street )
11. Mshume Kiyate (Tandamti Street)
12. Juma Sultan (Kitchwele karibu na kanisa dogo )
13. Maalim Shubeti (Masasi/Likoma Street)
14. Rajab Simba (Kiungani Street)
15. Waziri Mtonga (Kilosa no. 18, Ilala)
16. Mwinjuma Mwinyikambi (Mwananyamala)
17. Maxi Mbwana ( Aggrey /Kongo Street)
18. Usia Omari (Sungwi ,Kisarawe)
19. Sheikh Issa Nasir (Bagamoyo)
Kulia wa pili waliokaa Sheikh Suleilan Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU 1954 - 1958) (Swahili/Kariakoo Street)
Muhimu kufahamika ni kuwa Jiji la Dar es Salaam lilipotoa jina la mtaa wa huu kwa Dr. Aggrey hawakutoa kwa kuenzi ile fikra yake ya kuwataka Waafrika waunde African Association.

La hasha, jina la mtaa lilitolewa kwa ile sifa yake ya yeye kuwa Mwafrika msomi aliyefika Tanganyika wakati ule wa ukoloni.
Max Mbwana alipewa mtaa kwa mchango wake katika kuunga mkono TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Historia ya TANU inaanza hapa alipofika Dr. Aggrey Tanganyika na kumshauri Kleist na wenzake kuanzisha umoja wa Waafrika wa Tanganyika.

Hata hivyo ilimchukua Kleist miaka mitano hadi 1929 kuasisi African Association akiwa katibu muasisi na rais muasisi akiwa Cecil Matola.
Mkutano wa kuunda African Association ulifanyika nyumbani kwa Cecil Matola Mtaa wa Ndanda na Masasi.

Nyumba hii baadae ikaja kununuliwa na John Rupia na ipo hadi leo.

Waliokusanyika pale kuasisi African Association walikuwa Kleist Sykes, Cecil Matola, Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamis, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima, Suleiman Majisu, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Hili lilikuwa kundi la wazalendo tisa walioanza kufunga safari ngumu ya kuelekea New Street kuja kuunda TANU tarehe 7 Julai 1954.
Bahati mbaya sana ni kuwa wazalendo hawa hawafahamiki katika historia ya Tanganyika na kwa hakika historia hii isingelijulikana kama Kleist asingeandika historia ya maisha yake.

Mswada wake huu ulichukua miaka 24 hadi 1973 kufikia kuchapwa na kama si juhudi za John Iliffe mswada ungebaki kama ulivyoandikwa na mwishowe kutoweka kama zilivyotoweka nyaraka nyingi katika historia ya Waafrika wa Tanganyika.

Mswada huu ulichapwa katika kitabu alichohariri Iliffe, ‘’Modern Tanzanians,’’ kilichopigwa chapa na Tanzania Publishing House.
Nyaraka hizi za Sykes zimesaidia sana katika kuhifadhi si historia hii ya African Association bali hata historia ya TANU.

Abdul Sykes alimpa mswada huu pamoja na nyaraka nyingine binti yake Daisy, wakati ule mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na kupitia nyaraka hizi mwalimu wake wa historia, John Ilife aliweza kujua mengi ambayo yalimsaidia katika kuiandika kwa uhakika historia ya African Association.

Nyaraka hizi ndizo nyaraka pekee zilizoweza kuhifadhiwa kutoka kwa waasisi wa African Association waliokuwapo kati ya mwaka wa 1929 hadi 1954 ilipokuja kuasisiwa TANU.

Kushoto katika picha hapo chini: Mwinjuma Mwinyikambi, Max Mbwana Julius Nyerere na Mshume Kiyate, 1962.



Ufunguzi wa ofisi ya African Association New Street akiwapo Gavana Donald Cameron wa nne kushoto mstari wa kati, mstari wa nyuma kutoka kushoto wa sita ni Kleist Sykes, mstari wa mbele suti nyeusi ni Mwalimu Mdachi Shariff na mbele waliokaa kitako wa pili kushoto ni Ramadhani Mashado Plantan 1933.


 
Asante kwa kuendelea kuweka ukweli wazi, baada ya Nyerere na genge lake kufuta historia za wengine aliowakuta katika harakati toka Nineteen kweusi, na yeye 'wakuja' kujifanya ndo amefanya kila kitu katika Tanganyika hii..kiasi kwamba wajinga wengi wanadhani yeye ndo mwanzo na mwisho wa harakati za kudai uhuru
 
Kwenye hiyo picha ya waanzilishi wa TANU mbona hazungumziwi Kambona miongoni mwa waasisi. Au yeye alikuja baadae?
 
Kwenye hiyo picha ya waanzilishi wa TANU mbona hazungumziwi Kambona miongoni mwa waasisi. Au yeye alikuja baadae?
Last...
Oscar Kambona hakuwako Dar es Salaam wakati TANU inaundwa.

Waliokuwako na wakawa wanachama wa mwanzo ni Julius Nyerere kadi no. 1, Ally Sykes kadi no. 2, Abdul Sykes kadi no. 3, Dossa Aziz kadi no. 4, Denis Phombeah kadi no 5, Dome Okochi Budohi kadi no. 6, Abbas Sykes kadi no 7.

Utaona hapo kuna ndugu baba moja mama mmoja, Abdul, Ally na Abbas katika wanachama wa mwanzo wa TANU.

Sababu ni kuwa hawa baba yao Kleist Sykes ni mmoja wa waasisi wa African Association mwaka wa 1929 na hawa walikuwa ndani ya chama hicho.

Phombeah Mnyasa kutoka Nyasaland na Budohi Mluya kutoka Kenya hawa waliingia katika uongozi wa TAA pamoja na Nyerere katika uchaguzi ulifanyika Ukumbi wa Arnautoglo April 1953.

Kambona alipofika Dar es Salaam akitokea Dodoma alijiunga na TANU na aliongeza nguvu katika TANU na hakuchukua muda akawa mmoja wa viongozi wakubwa akishika nafasi ya Katibu nafasi ambayoo kwa siku za mwanzo ilizunguka sana kuanzia kwa Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafungo, Oscar Kambona na Elias Kissenge.

TAA Executive Committee: President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer and Ally K. Sykes Assistant Treasurer.

Committee members: Dr. Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo and Patrick Aoko ( Tanganyika Standard, 19 th June 1953).

Hawa ndiyo waliounda TANU mwaka wa 1954 na wako wengine kama Iddi Tosiri na ndugu yake Iddi Faiz Mafungo, nk. nk. hawa ni kutoka Dar es Salaam.

Katika waasisi 17 wa TANU wapo wale waliotoka majimboni kama Saadan Abdu Kandoro kutoka Kanda ya Ziwa, Joseph Kimalando na Japhaet Kirilo kutoka Jimbo la Kaskazini kwa kuwataja wachache hawa wote waliingiza wanachama wengi katika TANU baada ya kupelekewa kadi huko waliko mikoani.

Halikadhalika kuna wazalendo kama Haruna Taratibu na Omar Suleiman kutoka Dodoma, Suleiman Masudi Mnoji na Salum Mpunga kutoka Lindi hawa walifanya juhudi zao kufungua matawi ya TANU na kutuma watu kuja Dar es Salaam kufata kadi.

Lakini ukiwatoa hawa wanachama wa Dar es Salaam ambao walichukua kadi kabla ya chama hakijapata tasjila, kuna kundi kubwa la wanachama waliingia TANU kutoka Rufiji ambako walikwenda kupewa kadi na Mzee Said Chamwenyewe na sababu ni kuwa Msajili alidai aonyeshwe rejesta ya wanachama wa TANU kabla hajakisajii chama.

Hapo ndipo Abdul Sykes akamtuma Mzee Chamwenyewe kwenda Rufiji akalete wanachama.

Uamuzi huu ulifanywa na watu watatu - Abdul Sykes, Ally Sykes na Julius Nyerere nyumbani kwa Ally Sykes Mtaa wa Kipata (sasa Mtaa wa Kleist).

Mke wa Ally Sykes Bi. Zainab alikuwapo katika kikao hiki kama msikikilizaji kwa kuwa kikao kilikuwa nyumbani kwake.

Kadi 1000 za kwanza za TANU alinunua Ally Sykes kutoka mfukoni kwake na nyingine 2000 alikopa fedha za Tanganyika African Government Servant Association (TAGSA) ambako alikuwa Katibu.

Nimeona nitoe maelezo marefu kidogo na ya ziada kwenu kama zawadi kwa kuwa leo ni Saba Saba siku TANU iliundwa.

1625669037669.png

Kulia: Haruna Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Idd Faiz Mafungo Dodoma Railway Station 1956.

1625670034950.png

Kushoto ni Iddi Tosiri kadi ya TANU No. 25 na Iddi Faiz ni no. 24 hawa ni ndugu na kaka yao mkubwa ni Sheikh Mohamed Ramia na hawa wawili ndiyo walimchukua Nyerere hadi Bagamoyo kumtambuisha kwa Sheikh Ramiya. Safari ya UNO mkusanyaji fedha za safari alikuwa Iddi Faiz kama Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

1625671505325.png


Ally Sykes na Julius Nyerere nyumbani kwa Nyerere Magomeni 1958

1625671621976.png

Abdul Sykes na Julius Nyerere kulia ni Lawi Sijaona na kushoto ni Dossa Aziz hafla ya kumuaga Nyerere safari ya UNO Ukumbi wa Arnautoglo 1957.
 
Last...
Oscar Kambona hakuwako Dar es Salaam wakati TANU inaundwa.

Waliokuwako na wakawa wanachama wa mwanzo ni Julius Nyerere kadi no. 1, Ally Sykes kadi no. 2, Abdul Sykes kadi no. 3, Dossa Aziz kadi no. 4, Denis Phombeah kadi no 5, Dome Okochi Budohi kadi no. 6, Abbas Sykes kadi no 7.

Utaona hapo kuna ndugu baba moja mama mmoja, Abdul, Ally na Abbas katika wanachama wa mwanzo wa TANU.

Sababu ni kuwa hawa baba yao Kleist Sykes ni mmoja wa waasisi wa African Association mwaka wa 1929 na hawa walikuwa ndani ya chama hicho.

Phombeah Mnyasa kutoka Nyasaland na Budohi Mluya kutoka Kenya hawa waliingia katika uongozi wa TAA pamoja na Nyerere katika uchaguzi ulifanyika Ukumbi wa Arnautoglo April 1953.

Kambona alipofika Dar es Salaam akitokea Dodoma alijiunga na TANU na aliongeza nguvu katika TANU na hakuchukua muda akawa mmoja wa viongozi wakubwa akishika nafasi ya Katibu nafasi ambayoo kwa siku za mwanzo ilizunguka sana kuanzia kwa Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafungo, Oscar Kambona na Elias Kissenge.

TAA Executive Committee: President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer and Ally K. Sykes Assistant Treasurer.

Committee members: Dr. Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo and Patrick Aoko ( Tanganyika Standard, 19 th June 1953).

Hawa ndiyo waliounda TANU mwaka wa 1954 na wako wengine kama Iddi Tosiri na ndugu yake Iddi Faiz Mafungo, nk. nk. hawa ni kutoka Dar es Salaam.

Katika waasisi 17 wa TANU wapo wale waliotoka majimboni kama Saadan Abdu Kandoro kutoka Kanda ya Ziwa, Joseph Kimalando na Japhaet Kirilo kutoka Jimbo la Kaskazini kwa kuwataja wachache hawa wote waliingiza wanachama wengi katika TANU baada ya kupelekewa kadi huko waliko mikoani.

Halikadhalika kuna wazalendo kama Haruna Taratibu na Omar Suleiman kutoka Dodoma, Suleiman Masudi Mnoji na Salum Mpunga kutoka Lindi hawa walifanya juhudi zao kufungua matawi ya TANU na kutuma watu kuja Dar es Salaam kufata kadi.

Lakini ukiwatoa hawa wanachama wa Dar es Salaam ambao walichukua kadi kabla ya chama hakijapata tasjila, kuna kundi kubwa la wanachama waliingia TANU kutoka Rufiji ambako walikwenda kupewa kadi na Mzee Said Chamwenyewe na sababu ni kuwa Msajili alidai aonyeshwe rejesta ya wanachama wa TANU kabla hajakisajii chama.

Hapo ndipo Abdul Sykes akamtuma Mzee Chamwenyewe kwenda Rufiji akalete wanachama.

Uamuzi huu ulifanywa na watu watatu - Abdul Sykes, Ally Sykes na Julius Nyerere nyumbani kwa Ally Sykes Mtaa wa Kipata (sasa Mtaa wa Kleist).

Mke wa Ally Sykes Bi. Zainab alikuwapo katika kikao hiki kama msikikilizaji kwa kuwa kikao kilikuwa nyumbani kwake.

Kadi 1000 za kwanza za TANU alinunua Ally Sykes kutoka mfukoni kwake na nyingine 2000 alikopa fedha za Tanganyika African Government Servant Association (TAGSA) ambako alikuwa Katibu.

Nimeona nitoe maelezo marefu kidogo na ya ziada kwenu kama zawadi kwa kuwa leo ni Saba Saba siku TANU iliundwa.

View attachment 1844926
Kulia: Haruna Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Idd Faiz Mafungo Dodoma Railway Station 1956.

View attachment 1844957
Kushoto ni Iddi Tosiri kadi ya TANU No. 25 na Iddi Faiz ni no. 24 hawa ni ndugu na kaka yao mkubwa ni Sheikh Mohamed Ramia na hawa wawili ndiyo walimchukua Nyerere hadi Bagamoyo kumtambuisha kwa Sheikh Ramiya. Safari ya UNO mkusanyaji fedha za safari alikuwa Iddi Faiz kama Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

View attachment 1844986

Ally Sykes na Julius Nyerere nyumbani kwa Nyerere Magomeni 1958

View attachment 1844991
Abdul Sykes na Julius Nyerere kulia ni Lawi Sijaona na kushoto ni Dossa Aziz hafla ya kumuaga Nyerere safari ya UNO Ukumbi wa Arnautoglo 1957.
Nashukuru sana kwa hisani yako ya kunijuza historia ya kweli ya nchi yangu.. lakin bado hujalijibu swali langu..nipo interested more kuhusu Kambona, alijiunga mwaka gani na ana kadi namba ngapi? Na alitokea wapi?
 
Nashukuru sana kwa hisani yako ya kunijuza historia ya kweli ya nchi yangu.. lakin bado hujalijibu swali langu..nipo interested more kuhusu Kambona, alijiunga mwaka gani na ana kadi namba ngapi? Na alitokea wapi?
Nashukuru sana kwa hisani yako ya kunijuza historia ya kweli ya nchi yangu.. lakin bado hujalijibu swali langu..nipo interested more kuhusu Kambona, alijiunga mwaka gani na ana kadi namba ngapi? Na alitokea wapi?
Last...
Kambona katokea Dodoma akifundisha Alliance Secondary School.

Mwaka alijiunga TANU na namba ya kadi yake nasikitika sijui.
 
Asante kwa kuendelea kuweka ukweli wazi, baada ya Nyerere na genge lake kufuta historia za wengine aliowakuta katika harakati toka Nineteen kweusi, na yeye 'wakuja' kujifanya ndo amefanya kila kitu katika Tanganyika hii..kiasi kwamba wajinga wengi wanadhani yeye ndo mwanzo na mwisho wa harakati za kudai uhuru
Last...
Tujadili kistaarabu.
 
Last...
Tujadili kistaarabu.
Ustaarabu unashindikana baada ya kuona kuna watu wanapotosha makusudi kwasababu ya kuweka mbele udini na ukanda. Watu ambao walipigania hasa kwa kutembea kwa miguu ili kuorganise movement, wakatoa hela au 'visent' vyao vya ngama ili kufanikisha mikutano na shuguli za chama na kupigania uhuru wa nchi hii wamepuuzwa, na badala yake amebaki kuimbwa mtu mmoja tu Nyerere kwa mapana na marefu, wakasahaulika 'waasisi' hasa wa mapambano.. inasikitisha sana na haikubaliki
 
Ustaarabu unashindikana baada ya kuona kuna watu wanapotosha makusudi kwasababu ya kuweka mbele udini na ukanda. Watu ambao walipigania hasa kwa kutembea kwa miguu ili kuorganise movement, wakatoa hela au 'visent' vyao vya ngama ili kufanikisha mikutano na shuguli za chama na kupigania uhuru wa nchi hii wamepuuzwa, na badala yake amebaki kuimbwa mtu mmoja tu Nyerere kwa mapana na marefu, wakasahaulika 'waasisi' hasa wa mapambano.. inasikitisha sana na haikubaliki
Last...
Ngoja nikuambie kitu.

Baada ya uhuru kupatikana wakajitokeza watu ndani ya TANU wakaanza kuikashifu TAA na wengine wakamkashifu Abdul Sykes kuwa hakupata kuongoza chama cha siasa ila chama cha starehe.

Abdul hakujibu allikaa kimya hadi anaingia kaburini.
Na hata katika umauti wake magazeti ya TANU Uhuru na Nationalist yalimpuuza hakuwa taarifa ya maana.

Mhariri wa magazeti haya alikuwa Benjamin William Mkapa ambae baadae alikuwa kuwa Rais wa Tanzania.

Hapakuwa na taazia yake.

Waingereza, maadui zake aliowachimba usiku na mchana kuwatoa Tanganyika ndiyo kupitia gazeti lao Tanganyika Standard hawa walichapa taazia yake na kumpa heshima aliyostahili kupewa.

Lakini Abdul Sykes na mdogo wake Ally walitunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa mchango wao katika kupigania uhuru katika kuadhimisha sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.

1625713163125.png
 
Last...
Ngoja nikuambie kitu.

Baada ya uhuru kupatikana wakajitokeza watu ndani ya TANU wakaanza kuikashifu TAA na wengine wakamkashifu Abdul Sykes kuwa hakupata kuongoza chama cha siasa ila chama cha starehe.

Abdul hakujibu allikaa kimya hadi anaingia kaburini.
Na hata katika umauti wake magazeti ya TANU Uhuru na Nationalist yalimpuuza hakuwa taarifa ya maana.

Mhariri wa magazeti haya alikuwa Benjamin William Mkapa ambae baadae alikuwa kuwa Rais wa Tanzania.

Hapakuwa na taazia yake.

Waingereza, maadui zake aliowachimba usiku na mchana kuwatoa Tanganyika ndiyo kupitia gazeti lao Tanganyika Standard hawa walichapa taazia yake na kumpa heshima aliyostahili kupewa.

Lakini Abdul Sykes na mdogo wake Ally walitunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa mchango wao katika kupigania uhuru katika kuadhimisha sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.

View attachment 1845367
Sielewi hizi chuki za kibaguzi misingi yake ni nini
 
Maandiko yako ni mazuri sana.! Unatukumbusha kuijua hostoria ya Nchi yetu
 
Back
Top Bottom