Sifa za "msingi" za uongozi wa elimu:
1. Msingi- Diploma
2. Sek. - Bachelor
3. Chuo Ualimu- Masters
Taasisi mojawapo inayoongozwa na asiye na sifa hizo ni ama UTEUZI wake ulifanywa kukiwa na upungufu wa wenye sifa stahiki kitaaluma ama sifa ya uzoefu wa angalau miaka mitatu kikazi...
Kadhalika, ni mara chache kutengua uteuzi wa mtu...kinachofanyika ni kumpa muda mteule huyu kujiendeleza kitaaluma ili afikie kiwango stahiki, muda huo ukipita ni rahisi kutengua kwa kuwa muhusika alishindwa kukidhi haja ya mwajiri wake...
Kuanzia Julai 2014, kuna waraka unaelekeza kuhusu posho:
HT(dip.holder) -200,000/=
HoS(b/masters)-250,000/=
MEK(b/masters)-250,000/=
Principle -300,000/=*
DSEO & DEO -300,000/=
Tanbihi:
1) Kiongozi wa taasisi asiye na sifa hizo za kitaaluma hatapata posho hiyo mpaka atakapofikia kiwango husika cha taaluma- Kwa mujibu wa waraka...
2) Kwa mfumo wetu wa elimu Tz...Kiwango cha juu kinachotambuliwa kwa ngazi ya msingi na sekondari (O&A Levels) ni BACHELOR DEGREE...!! MASTERS ni ADDED QUALIFICATION
Hivyo, panapotokea uwingi wa wenye sifa ya msingi, sifa ya ziada inatafutwa ili kuongoza taasisi-Kwa mujibu wa uelewa na uzoefu wangu katika taasisi za serikali...
Nawasilisha taarifa ya awali
Tafakari...