Walimu wa leo wana kipi cha kujivunia?

Walimu wa leo wana kipi cha kujivunia?

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Mada inazungumzia kwa upekee uandishi na matamshi ya lugha ya kiswahili. Kingereza si lugha yetu hivyo sitalaumu sana huko. Ukiwasikiliza vijana wengi sasa unagundua hawajui hata hicho kiswahili kinachoongewa kila siku.

Nakumbuka shule ya msingi tulisoma "imla". Kwa kingereza ni dictation. Mwalimu anasoma na sisi tunaandika kwa ufasaha alichokuwa anatamka. Zoezi hilo lilifanyika hadi mwanafunzi aliweza kuandika kwa ufasaha anachotamka.

Kwa vijana wengi wa zamani ni nadra kukuta anakosea matamshi. Kinyume chake leo hii kijana aandike ujumbe kwenye status yake ya simu utaona aibu. Mfano "mwanangu una baya". Au "usimzalau usiemjua. Uyo nitajili wa kesho". Au "mungu (Mungu) si asumani" .... Na ujinga mwingine mwingi sana.

Waathirika wakubwa kwenye hili kundi ni vijana fulani hivi wa kada ya chini. Madereva, mafundi, etc. Wa kada ya juu nao tatizo halijawaacha.

Hawa walimu wanaofundisha hasa elimu ya msingi ndio hao hao waliofeli imla na hawataweza kuwasahihisha wanafunzi. Ni aibu. Inafika wakati unaona kijana wa kada hiyo kaandika kiswahili fasaha, unaanza kumshangaa. Unagundua kuwa huyu ana akili. Akili ya kuweza kuainisha. Walimu mnakwama.
 
Hawa walimu wanaofundisha hasa elimu ya msingi ndio hao hao waliofeli imla
UDSM, SUA, MZUMBE, UDOM, hivi ni vyuo pendwa hapa nchini.Huko kuna kozi za ualimu, hawa wapo huko shule ya msingi, au hufahamu? Vipi nao wanachukua wanafunzi waliofeli imla?

Hoja yako dhaifu sana, umejikita kwenye eneo dogo ambalo nalo ni kasumba uliyojengwa zamani kuwa 'walimu ni watu waliofeli'!
 
Mada inazungumzia kwa upekee uandishi na matamshi ya lugha ya kiswahili. Kingereza si lugha yetu hivyo sitalaumu sana huko. Ukiwasikiliza vijana wengi sasa unagundua hawajui hata hicho kiswahili kinachoongewa kila siku.

Nakumbuka shule ya msingi tulisoma "imla". Kwa kingereza ni dictation. Mwalimu anasoma na sisi tunaandika kwa ufasaha alichokuwa anatamka. Zoezi hilo lilifanyika hadi mwanafunzi aliweza kuandika kwa ufasaha anachotamka.

Kwa vijana wengi wa zamani ni nadra kukuta anakosea matamshi. Kinyume chake leo hii kijana aandike ujumbe kwenye status yake ya simu utaona aibu. Mfano "mwanangu una baya". Au "usimzalau usiemjua. Uyo nitajili wa kesho". Au "mungu (Mungu) si asumani" .... Na ujinga mwingine mwingi sana.

Waathirika wakubwa kwenye hili kundi ni vijana fulani hivi wa kada ya chini. Madereva, mafundi, etc. Wa kada ya juu nao tatizo halijawaacha.

Hawa walimu wanaofundisha hasa elimu ya msingi ndio hao hao waliofeli imla na hawataweza kuwasahihisha wanafunzi. Ni aibu. Inafika wakati unaona kijana wa kada hiyo kaandika kiswahili fasaha, unaanza kumshangaa. Unagundua kuwa huyu ana akili. Akili ya kuweza kuainisha. Walimu mnakwama.
Huku kwetu uswahln kwenye shule zetu za 'elomenopi' wanayo mengi ya kujivunia,kwa mfano:
1.Elfu 1000 ya ubwabwa kila siku.
2.Darasa moja wanakaa wanafunzi 297 tena kwa utulivu wa hali ya juu.
3.Kila jumamosi ni TSH 1000 kwa ajili ya mitihani ya kujipima.
4.Pesa ya masomo ya ziada tsh 200 kila siku.
5.Kusimamia chaguzi mbali mbali.
6.Mikopo ya kausha damu.
7.Mikopo ya bidhaa mbali mbali toka kwa waha.
 
Bila kusahau wale wa:-
. Xaxa = sasa
. Ucku = usiku
. Jomoni = jamani

🤒🤒.
 
UDSM, SUA, MZUMBE, UDOM, hivi ni vyuo pendwa hapa nchini.Huko kuna kozi za ualimu, hawa wapo huko shule ya msingi, au hufahamu? Vipi nao wanachukua wanafunzi waliofeli imla?

Hoja yako dhaifu sana, umejikita kwenye eneo dogo ambalo nalo ni kasumba uliyojengwa zamani kuwa 'walimu ni watu waliofeli'!
Ukweli ndio huo. Matunda yake tunayaona. Na nimejikita hapo kwa sabsbu za msingi sana jjapo ni kaeneo kadogo. Pia hao uliowataja hawaendi kufundisha eneo nililotaja
 
Pia hao uliowataja hawaendi kufundisha eneo nililotaja
Huko shule ya msingi wanaenda kufanya nini?? Serikali ilipoamua kupeleka walimu wenye shahada shule ya msingi, unafikiri hawakwenda kufundisha hiyo 'imla'?


Au huamini, kuwa walimu wenye shahada kutoka vyuo pendwa na wenye G.P.A kali wapo msingi??
 
Mada inazungumzia kwa upekee uandishi na matamshi ya lugha ya kiswahili. Kingereza si lugha yetu hivyo sitalaumu sana huko. Ukiwasikiliza vijana wengi sasa unagundua hawajui hata hicho kiswahili kinachoongewa kila siku.

Nakumbuka shule ya msingi tulisoma "imla". Kwa kingereza ni dictation. Mwalimu anasoma na sisi tunaandika kwa ufasaha alichokuwa anatamka. Zoezi hilo lilifanyika hadi mwanafunzi aliweza kuandika kwa ufasaha anachotamka.

Kwa vijana wengi wa zamani ni nadra kukuta anakosea matamshi. Kinyume chake leo hii kijana aandike ujumbe kwenye status yake ya simu utaona aibu. Mfano "mwanangu una baya". Au "usimzalau usiemjua. Uyo nitajili wa kesho". Au "mungu (Mungu) si asumani" .... Na ujinga mwingine mwingi sana.

Waathirika wakubwa kwenye hili kundi ni vijana fulani hivi wa kada ya chini. Madereva, mafundi, etc. Wa kada ya juu nao tatizo halijawaacha.

Hawa walimu wanaofundisha hasa elimu ya msingi ndio hao hao waliofeli imla na hawataweza kuwasahihisha wanafunzi. Ni aibu. Inafika wakati unaona kijana wa kada hiyo kaandika kiswahili fasaha, unaanza kumshangaa. Unagundua kuwa huyu ana akili. Akili ya kuweza kuainisha. Walimu mnakwama.
wanajivunia zaidi kutimiza ndoto zao za utotoni za kua walimu 🐒
 
Huko shule ya msingi wanaenda kufanya nini?? Serikali ilipoamua kupeleka walimu wenye shahada shule ya msingi, unafikiri hawakwenda kufundisha hiyo 'imla'?


Au huamini, kuwa walimu wenye shahada kutoka vyuo pendwa na wenye G.P.A kali wapo msingi??
Labda kina Bunge, Olyimpio, St. So and so, ila sio St. Kayumba. Sio shule za kata
 
Ili twende sawa utanipatia takwimu ya hao waliotolewa wasi na waziri.
Wapo shule zipi wakifundisha?
Samahani ndugu, unataka kuelekezwa au kubishana??


Uhalisia: Mwaka 2018 walimu wote wa sekondari waliozidi hasa katika masomo ya sanaa katika halmashauri zote za Tanzania hapa nchini walipelekwa kufundisha shule za msingi (nyingi vijijini)


Walimu wengi kwa ngazi ya shahada walipelekwa kufundisha shule za msingi.Mara baada ya zoezi hili kukamilika, serikali katika kuajiri inakuchagua moja kwa moja na shahada yako kwenda msingi .


Takwimu: 1) Tafuta idadi ya halmashauri za hapa nchini, nenda kaulize ni walimu wangapi wa shahada walipelekwa shule za msingi. Piga simu watakuambia.


2) Tafuta ajira za ualimu kuanzia 2019 na kuendelea,halafu tafuta walimu wa shahada ni wangapi wanaopelekwa kufundisha shule za msingi.


Nb 1: Nimejaribu kukuelekeza, kuna vitu ulikuwa huvifahamu, na huo mwaka 2018 sijui ulikuwa wapi!


Nb 2: Kingine, ni kukuondolea dhana ya shahada kuwa ni kitu cha thamani mno! Yaani unashangaa mwalimu wa shahada kutoka UDSM, MZUMBE. UDOM n.k kufundisha msingi tena vijijini, wakati watu washazoea na kusahau!
 
Samahani ndugu, unataka kuelekezwa au kubishana??


Uhalisia: Mwaka 2018 walimu wote wa sekondari waliozidi hasa katika masomo ya sanaa katika halmashauri zote za Tanzania hapa nchini walipelekwa kufundisha shule za msingi (nyingi vijijini)


Walimu wengi kwa ngazi ya shahada walipelekwa kufundisha shule za msingi.Mara baada ya zoezi hili kukamilika, serikali katika kuajiri inakuchagua moja kwa moja na shahada yako kwenda msingi .


Takwimu: 1) Tafuta idadi ya halmashauri za hapa nchini, nenda kaulize ni walimu wangapi wa shahada walipelekwa shule za msingi. Piga simu watakuambia.


2) Tafuta ajira za ualimu kuanzia 2019 na kuendelea,halafu tafuta walimu wa shahada ni wangapi wanaopelekwa kufundisha shule za msingi.


Nb 1: Nimejaribu kukuelekeza, kuna vitu ulikuwa huvifahamu, na huo mwaka 2018 sijui ulikuwa wapi!


Nb 2: Kingine, ni kukuondolea dhana ya shahada kuwa ni kitu cha thamani mno! Yaani unashangaa mwalimu wa shahada kutoka UDSM, MZUMBE. UDOM n.k kufundisha msingi tena vijijini, wakati watu washazoea na kusahau!
Ni jambo jema. Asante pia kwa taarifa. Turudi kwenye hoja. Bado vijana wengi wanaotoka shule za awali hawana uwezo wa kuandika kiswahili fasaha.
 
Mada inazungumzia kwa upekee uandishi na matamshi ya lugha ya kiswahili. Kingereza si lugha yetu hivyo sitalaumu sana huko. Ukiwasikiliza vijana wengi sasa unagundua hawajui hata hicho kiswahili kinachoongewa kila siku.

Nakumbuka shule ya msingi tulisoma "imla". Kwa kingereza ni dictation. Mwalimu anasoma na sisi tunaandika kwa ufasaha alichokuwa anatamka. Zoezi hilo lilifanyika hadi mwanafunzi aliweza kuandika kwa ufasaha anachotamka.

Kwa vijana wengi wa zamani ni nadra kukuta anakosea matamshi. Kinyume chake leo hii kijana aandike ujumbe kwenye status yake ya simu utaona aibu. Mfano "mwanangu una baya". Au "usimzalau usiemjua. Uyo nitajili wa kesho". Au "mungu (Mungu) si asumani" .... Na ujinga mwingine mwingi sana.

Waathirika wakubwa kwenye hili kundi ni vijana fulani hivi wa kada ya chini. Madereva, mafundi, etc. Wa kada ya juu nao tatizo halijawaacha.

Hawa walimu wanaofundisha hasa elimu ya msingi ndio hao hao waliofeli imla na hawataweza kuwasahihisha wanafunzi. Ni aibu. Inafika wakati unaona kijana wa kada hiyo kaandika kiswahili fasaha, unaanza kumshangaa. Unagundua kuwa huyu ana akili. Akili ya kuweza kuainisha. Walimu mnakwama.
tunajivunia kuwa na mwanafunzi kama Mpwayungu Village
 
Back
Top Bottom