Huyo mleta uzi ndio wale wanaodhurura na bahasha mitaani wakitafuta ajira. Anaona kinyongo walimu kupewa ajira ili hali yeye amesugua benchi miaka kadhaa kitaa bila hata kiajira cha kujishikisha. Mleta uzi ikiwa kila mgonjwa akifa au akashindwa kupona dokta anaemuuguza anakatwa mshahara utawakata wa ngapi? Unajua wanafunzi kufeli si kosa la walimu bali ni wazazi na sirikali yenyewe? Kama mtoto anapeleka sekondari akiwa na wastani wa 80 ya 250 wewe unategemea nini? Kama mtoto anawastani wa 20 ya 100 kidato cha pili anaruhusiwa na sirikali aende kidato cha tatu unategemea nini akifika form 4? Kama shule inamwalimu mmoja wa hisabati na ina mikondo 16 unategemea nini? Jaribu kuwa thinkative ndugu sio kuleta chuki kwa walimu, kasome post graduate ya ualimu utaajiriwa pia. Au kasome diploma utapata ajira pia. Maneno hayata kusaidia wenzio ndio wanaingizwa kwenye payroll hivyo.