Mkuu ninachoona walimu waanze kuingiza siasa mashuleni kwa kutoa elimu kwa wale form four au form five na six walio nao nao mashuleni kupigia kura vyama pinzani na kuwashauri wakawaelimishe na wazazi wao vivyo hivyo iwe mjini au vijijini najua kwa sasa vijana ndo wenye nchi na walimu najua mna ushawishi mkubwa mbele za wanafunzi hao ambao wengi wao wana umri wa miaka 18 na kuendelea.
Madai ya waalimu kuidai serikali hayajaanza Leo, ni wimbo ambao umerithishwa toka kipindi kimoja cha uongoz kwenda kingine. Leo hii tunaongelea madai ya mabilioni ya shilingi wanayodai waalim toka vipindi vya uongozi vilivyopita.
Najiuliza serikali hii ambayo inadeni kubwa sio tu kwa waalim bali hata watumishi wengine, inawezaje kuendelea kuajiri waalim au madaktari isiyoweza kulipa madeni ya mwanzo? Uliona wapi unaruhusiwa kukopa ilhali deni la mwanzo bado bichi!!!!!!
Majuzi tuliarifiwa kwamba serikali imepewa onyo na taasisi za fedha za kimataifa kwamba inakoelekea haitakopesheka kutokana na kuongezeka kwa deni; unastaajabishwa na taarifa kama hizo kwa kujiuliza pesa tunakopa lakini mbona matumiz hayaeleweki?
Serikali iachane na matumizi mabaya ya fedha, iwekeze kwenye kuboresha maslahali ya watumishi na miradi ya maendeleo, wakusanye kodi na sio kuruhusu wengine walipe wengine wasilipe,,
Ushauri wako kuhusu waalimu kuhubiri siasa za upinzani kwa mtazamo wangu mm naona bado hauna mashiko; ni kwa sababu serikali bado inadeni kubwa kwa watumishi wake wote, waalim, wanajeshi, madaktari, polisi nk.
Sasa hao wengine ukiondoa waalimu nani atakuwa balozi wao, nadhani watanzania wote kwa sasa inatosha kuburuzwa na serikali isiyojua nini wajibu wake,, mabadiliko ya mfumo wa uongozi kuanzia juu yanahitajika haraka sana.
Nawasilisha.
Sent from my iPhone using JamiiForums app.