Walimu wapya hatuna mishahara

Mkuu uliyekuwa unataka mawasiliano ya Waziri wa Elimu haya hapa. GENERAL Salutation Honourable Member picture First Name: Dr. Shukuru Middle Name : Jumanne Last Name: Kawambwa Member Type: Constituency Member Constituent: Bagamoyo Political Party: CCM Office Location: P.O.Box 9121, Dar es Salaam Office Phone: +255 787 400 700 Ext.: Office Fax: Office E-mail: skawambwa@parliament.go.tz Member Status: Current Member Date of Birth 15 December 1957.

Ahsante Mkuu!
 
Mkuu wangu, ingawaje watu wanamponda sana Mulugo, lakini katika ufuatiliaji naamini Mulugo ni mzuri sana kuliko Kawambwa! Labda kawambwa apigiwe simu kisha amjulishe Mulugo otherwise, hakuna kitu hapo!
 
Ndugu wana JF naomba kwa yeyote anayeweza kusaidia kupatikana mawasiliano ya Waziri wa Elimu anipe.
Huu ni mwezi wa pili sasa mamia ya walimu tulioajiriwa Machi2013 hatuna mishahara.
Mbaya zaidi majibu ya Maafisa Elimu na Wakurugenzi hayana utu.
Nakushauri kama kuwasiliana basi wasiliana na Mulugo kuliko Kawambwa! Kwa mtazamo wangu, namuona Mulugo ni mzuri sana ktk follow up kuliko Kawambwa!
 
Yaani hata ukipata namba za huyo mkubwa wa elimu,naye hakawii kuingia mitini.
 
Yaani hata ukipata namba za huyo mkubwa wa elimu,naye hakawii kuingia mitini.

Naibu Waziri Mwanri anapatikana katika 0754693156
anatoa maelezo mazuri na kama sikuelewa vibaya TATIZO LIKO KTK HALMASHAURI ZETU.
 
halmashauri wilaya ya magu, mkoani mwanza!

ni bagamoyo ambako rais watu wa halmashauri ni corrupt idara zote hii ya elimu sekondari ndo imeoza kabisa hela ya kujikmu wamekatwa na kuambiwa wao wenyewe wamepewa pungufu mwez nusu ya walimu walioajiliwa wapatao 54 hawapo kwenye payrol
 
Walimu wapya wakesha kwa mkurugenzi


na Sitta Tumma, Magu

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, walimu wapya wa shule za sekondari wilayani Magu, mkoani Mwanza, juzi walilazimika kulala nje ya Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Magu, wakishinikiza kulipwa mishahara yao.
Walimu hao wapatao 100 kutoka shule mbalimbali wilayani hapa, walifikia uamuzi huo baada ya kutolipwa mishahara yao na haki zao nyingine stahiki tangu Machi mwaka huu, walipoajiriwa na serikali.Wakizungumza na Tanzania Daima Jumatano nje ya ofisi hiyo, walimu hao walieleza kuchukizwa na kitendo cha serikali kutowalipa mishahara kwa muda wote huo.Walisema kuwa kati ya walimu wapya 154, ni walimu zaidi ya 50 pekee ndio wameingizwa kwenye mpango wa kulipwa mishahara, huku wengine wakiwa hawajui hatima yao.Walifafanua kuwa ofisi ya mkurugenzi imekuwa ikikataa kuzungumza nao na wakati mwingine inawaamuru waende kuomba fedha za kujikimu kwa wakuu wao wa shule, jambo ambalo wakuu hao wanakataa.“Juzi tumekuja hapa kwa mkurugenzi saa 2:00 asubuhi kudai fedha zetu za mishahara. Lakini tulizungushwa na ofisa elimu takwimu wa wilaya, ambaye alitupa vitisho kwamba tunahatarisha ajira zetu iwapo tutaendelea kukaa hapa.“Licha ya kwamba mkurugenzi jana hatukumkuta na kupewa vitisho hivyo, tulilazimika kuweka kambi na kulala hapa. Na leo hatutaondoka hapa mpaka kieleweke,” alisema Deusdedith Millanzi kwa niaba ya wenzake.Walimu hao waliongeza kuwa kutokana na kukosa mishahara yao tangu waajiriwe Machi mosi mwaka huu, kwa sababu majina yao hayajaingizwa kwenye utaratibu wa malipo, wataendelea kuweka kambi na kulala nje ya ofisi hizo.Walisema kuwa wamejionea mkanganyiko dhidi ya majina yao, ambapo baadhi ya majina yaliyopo Ofisi ya Utumishi Wilaya ya Magu yanaonesha hayamo kwenye mpango wa kulipwa.Lakini kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya majina hayo yanaonesha yamo katika mpango huo wa kupata mshahara kama watumishi wengine wa serikali.“Tumechoka kuzunguka. Hivi tumeletwa Magu kuja kuteseka? Na kwa mtindo huu wanatuweka kwenye mazingira magumu sana walimu wengi. Tutaishije hawatulipi?” alihoji mwalimu mwingine ambaye alikataa kutajwa jina lake.Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Wilaya ya Magu (CWT), Boniphace Maghembe, aliiambia Tanzania Daima kuwa madai ya walimu hao yapo sahihi na kuitaka serikali iwalipe mishahara na stahiki zao si vinginevyo.Akizungumzia malalamiko hayo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo ya Magu, Bonaventra Kiswaga, alikiri walimu hao kulala nje ya ofisi ya mkurugenzi wakishinikiza kulipwa mishahara yao.Kiswaga alisema kulingana na unyeti wa madai ya walimu hao, ofisi ya mkurugenzi na Utumishi ya wilaya hiyo zinayafanyia kazi malalamiko ya walimu hao, hivyo kuwataka wavute subira wakati ufumbuzi wa tatizo hilo ukitafutwa.

TANZANIA DAIMA, JUMATANO MEI 1, 2013
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…