Umoja wa Walimu wasio na ajira nchini Tanzania (NETO), umemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan na Serikali, kuwasaidia Walimu hao kupata ajira na kuweka usimamizi madhubuti pamoja na kufuta mfumo wa usaili katika mchakato wa kutoa ajira.
Uongozi wa Umoja huo kupitia kwa Katibu wake Daniel Edgar mbele ya Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam, pia umeeleza kusikitishwa na kauli zilizotolewa na baadhi ya Viongozi wa Serikali kwamba Waalimu waliokaa muda mrefu bila kuajiriwa hawana ubora wa kutosha jambo ambalo wanalipinga na kusema kuwa sio kweli.
Pamoja na hayo, Katibu huyo ameomba Serikali kufuatilia Shule binafsi zilizopo Tanzania kwani wamegundua kuna Waalimu wenye degree wanalipwa mshahara wa shilingi laki moja na nusu huku wale wenye Diploma wakilipwa shilingi laki moja.
“Unakuja Shule ina Watoto 1200 na kila Mtoto analipa ada sh. milioni 1.2 lakini Mwalimu analipwa mshahara laki mbili laki tatu, tunaomba Serikali iingilie kwenye Sekta binafsi”
Sometimes walimu wenyewe Huwa tunafodi king na kukubaliana na masharti. Mfano unaomba kazi wanakuambia hapana uhitaji ila kama utajitolea na ikitokea nafasi upewe kipaumbele utaajiriwa. Katika mazingira kama hayo mtu unaamua kujitolea lakini unakuta muda unaenda miaka inakatika upo kwenye kujitolea na baadae inakua kama umeajiriwa.
Huo ni mshahara wanaolipwa walimu wa kujitolea shule binafsi ni sawa na wafanyakazi wa kujitolea viwandani kwa matumaini ya kupewa kipaumbele ajira ikitokea wapate.
So Pana waajiri viwandani maofisini mashuleni vyuoni nk upata cheap labour kwa kuwatumia wanaojitolea ili kupunguza gharama kuliko kuajiri.
Kujitolea ni aina fulani ya utumwani
Aisee Nchi hii kiboko yaani wanapitisha mishahara hiyo kwa Watanzania wenzao huku wao wakijilipa posho laki tatu kwa kikao kimoja cha masaa kadhaa tu na hakuna kitu cha maana kinajadiliwa zaidi ya kupongezana kushinda ubunge tu.