Walimu watuhumiwa kupora vichongeo, ufutio vya wahitimu wa Darasa la Saba

Walimu watuhumiwa kupora vichongeo, ufutio vya wahitimu wa Darasa la Saba

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Walimu wa Shule ya Msingi za Kishinda na Isebya zilizoko kata ya Kishinda wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza wanatuhumiwa kupora vifaa vya wanafunzi baada ya kumaliza mtihani wa kitaifa wa darasa la saba. Malalamiko ya wahitimu hao yaliwasilishwa na Diwani wa Kata ya Kishinda, Shokolo Visent kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo kilichofanyika Oktoba 28 na kuwaamuru walimu hao kulejesha vifaa.

Walianisha vifaa hivyo kuwa kilamu za wino, peseli, vichongeo pamoja na vifutio ambavyo vilinunuliwa na wazazi wa wanafunzi hao na siyo mali ya shule. "Ingekuwa mali ya shule vingebaki shuleni lakini kwa sasa siyo mali za shule vifaa hivyo vinatakiwa walejeshewe wanafunzi, amesema Shokolo.

Kutoka na malalamiko hayo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Sengerema, Yanga Makaga amesema walimu hawana mamlaka ya kuwanyang’anya wanafunzi vifaa vyao baada ya kumaliza mitihani yao, hivyo ameamuru vifaa hivyo vilejeshwe.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sengerema, Binuru Shekidele amesema atafuatilia suala hilo ili abaini ukweli wake na kuwataka walimu waliochukua vifaa hivyo wavilejeshe kwa wenyewe. Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kishinda, Raymondo Alex amesema ni kweli vifaa hivyo vilikuwa vimekusanywa na ilitokana na makubaliano kati ya wahitimu hao na mwalimu wa darasa lao.

Lakini kutokana na maagizo hayo vifaa hivyo vimerejeshwa kwa wahitimu hao ili kuondoa mkanganyiko huo.

MWANANCHI
 
Hii nayo eti ni habari? Vichongeo, penseli ndiyo vitu vya kumtuhumu mwalimu mpaka kwenda kwenye Baraza la madiwani? Diwani kabisa anakomaa na penseli badala ya kutatua kero za maendeleo! Wanasiasa wanachangia sana kuharibu jamii yetu!
 
Tulimnunulia vifaa vyipya hajarudi hata na penseli, tukamuuliza vipi? Akasema ticha katunyang'anya kasema tuviache.

Kufanya uchunguzi wameuziwa darasa la nne walivyofanya mtihani juzi[emoji16]

Nikajisemea tu hiiiiiiiii[emoji16]
 
Hii nayo eti ni habari?? Vichongeo, penseli ndiyo vitu vya kumtuhumu mwalimu mpaka kwenda kwenye Baraza la madiwani?? Diwani kabisa anakomaa na penseli badala ya kutatua kero za maendeleo! Wanasiasa wanachangia sana kuharibu jamii yetu!
Badala ya kuwalaumu waalimu kwa kupora vitu vidogovidogo unalaumu anayekataza huo ujinga! Lazima wewe mwalimu ni mmoja wa waliopora hivyo vichongeo na penseli.
 
Badala ya kuwalaumu waalimu kwa kupora vitu vidogovidogo unalaumu anayekataza huo ujinga! Lazima wewe mwalimu ni mmoja wa waliopora hivyo vichongeo na penseli.
Hakuna sehemu nimetetea waalimu mh. Diwani, hoja yangu kuu ni kuacha kushughulikia mambo ya msingi kuhusu kero za wananchi , eti diwani anasimama kuongelea vichongeo! Hiyo ni level ya kikao cha madiwani kweli??
 
Kuna mada za hovyo sana sikuhizi JF. Sio bure CCM inawafanya watanzania mtaji kwa ujinga wao.
Mnaelezwa jinsi taaluma ya ualimu inavyochafuliwa na "walimu" waliokosa maadili.Kwa nini wawapore watoto vitu vyao halali hata kama vimenunuliwa kwa shili gi ishirini?
 
Hakuna sehemu nimetetea waalimu mh. Diwani, hoja yangu kuu ni kuacha kushughulikia mambo ya msingi kuhusu kero za wananchi , eti diwani anasimama kuongelea vichongeo! Hiyo ni level ya kikao cha madiwani kweli??
Umejibu vema.Hata watoto nao wametoa kero.Wamenyanyaswa,kuporwa na kuumizwa kisaikolojia.Hiyo kero imemfikia diwani kwa usahihi.Walimu wamewaonea watoto na kuonesha mfano mbaya kwenye mambo madogo.Siku nyingine watafanya jambo kubwa kwa uzao wa jambo dogo.Hakuna dogo katika haki.
 
Tulimnunulia vifaa vyipya hajarudi hata na penseli, tukamuuliza vipi? Akasema ticha katunyang'anya kasema tuviache.

Kufanya uchunguzi wameuziwa darasa la nne walivyofanya mtihani juzi[emoji16]

Nikajisemea tu hiiiiiiiii[emoji16]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mbona ilikuwa inshu ndogo tu,diwani angefika kwenye hzo shule na kutatua tatzo,mbona huku kwetu diwani anaogopwa sana na watumishi wa serikali,halikupaswa kufika kwenye baraza la madiwani
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Halafu ni private school[emoji16][emoji16]

Last born nae alikuwa ana mtihani class 4 tulitegemea vifaa vya dada atavitumia yeye,[emoji23]

i[emoji23],mkebe,lura,penseli vinawachafulia jina[emoji16]
 
Huko ndiko kwenye uwanja wa siasa credit ataipta wapi
Mbona ilikuwa inshu ndogo tu,diwani angefika kwenye hzo shule na kutatua tatzo,mbona huku kwetu diwani anaogopwa sana na watumishi wa serikali,halikupaswa kufika kwenye baraza la madiwani
 
Back
Top Bottom