Waliojinadi kuwa Serikali Sikivu wamethibika kuwa Viziwi

Waliojinadi kuwa Serikali Sikivu wamethibika kuwa Viziwi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kuna mwenye masikio mazima ambaye hajayasikia manung'uniko ya wananchi? Au basi hata yupo mwenye kutokujua ni nini kinachohitajika kufanywa hadi sasa?

Si tulidhani labda wanasikia nusu nusu? Tukashauriana kuongeza sauti?

"Serikali 'sikivu' Inaposikia nusu nusu"

Kwani lipi wamesikia hata?

Hawa si wamedhamiria tu kufanya yao na kinyume cha utaratibu?

Muda wa kufanya maamuzi magumu ni sasa:

"Tunataka haki? Hatutaki tozo? Tukutane Tahrir."

Anasema J.J. Rawlings (RIP):

"Ni lazima ifikie pale ambapo hata kama shweitani atakuwa ndiye mtawala (rais), itakuwa ni lazima afanye kile ambacho Waghana (wananchi) wanataka na wala siyo kile ambacho yeye shweitani na genge lake wanataka."

Yote yako mikononi mwetu. Yote yanawezekana.

Mola na ukatubariki waja wako.
 
Tuandamane au?

Mbona huku nasikia vigelegele & chereko za ANAUPIGA MWINGI?
 
Lazima awepo kiongozi wa kufanikisha haya unayoandika, kama ni hawa waliopo au wengine tofauti, muhimu wawepo viongozi, kujiendea wenyewe ninsawa na kutokujua dira.
 
Back
Top Bottom