Waliokatwa vizimba soko la Kariakoo waandamana kwenda ofisi za CCM Lumumba!

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hii ndio Taarifa ya sasa kutoka Dar es Salaam.

Kwamba Wale waliokuwa wafanyabiashara wa soko hilo kabla halijaungua na ambao majina yao hayapo kwenye mkeka mpya, wameandamana kuelekea CCM Lumumba!

Pia soma: Mgomo wa Wafanyabiashara: Biashara zafungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024

Sasa sijajua kama ni wajinga au la, Maana hawakupaswa kuelekea huko badala yake walipaswa kwenda kwenye mamlaka husika.

Nani kawachuuza kirahisi hivi? Tangu lini ccm ilikuwa na msaada kwenye mambo haya?

Your browser is not able to display this video.

Pia soma: DC Ilala awatuliza wafanyabiashara Kariakoo, kukutana na Chalamila kesho
 
Mimi sijaelewa walikuwa wanapanua nini hapo kkoo...nilitegemea zitangazwe nafas wazi ili wengine wapate
 
Washagawana makada wa CCMl tayari!🤣🤣🤣
 
Watu wenye hela zao washabeba nafasi zao. But wamewafanyia vibaya ni ajali ya moto ilitokea. Wangewarudisha wote, washindwe wenyewe kodi au ushuru. Machinga complex walifanya hayahaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…