Waliomaliza form iv mwaka 2007 kushuka v/s waliomaliza form four 2008-2013.

Makuku Rey

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2013
Posts
3,497
Reaction score
3,823
Nimegundua ubora wa elimu hapa TZ,ulianza kushuka miaka ya 2008, kama tunakumbuka kipndi hiki(kikwetism) mitihani ya taifa form 2 na form 4 ilivuja mno, Madogo wengi walitusua kwa kwenda shule za vipaji maalum. Miaka ya hapa kati 2009,2010,....,...2012 elimu yetu bado ilikuwa ikilegalega. Matokeo ya mtihani form iv 2013,SERIKALI imeamua kuwabeba wanafunzi na kujiriDHIsha kuwa inatekeleza sera ya BRN. Kwa maelezo haya mi naona msomi wa mwisho kumaliza form IV nchini TANZANIA ni yule aliyemaliza miaka ya 2007,2006,2005....... Hawa wa miaka ya 2008,2009,........ ni wasomi wa kupewa maksi na serikali! Au ninyi mnaonaje wakuu?
 
Mwaka 2007 ulikuwa ni highest peak kwa ufaulu na baada ya hapo mambo yalianza kuvurugika sana, mambo mengi yanachangia.

1. Walio maliza 2008 kama mnakumbuka walivurugwa na Mungai (hawa ni watu wa physics with chemistry.
2. Watu wa 2009 hawa hawakuwa na mtihani wa form two, wasiojiweza wengi walifika form four.
3. 2010 kulikuwa na uchaguzi wa kitaifa, kila mtu alikuwa bize na siasa, kama mnakumbuka mwaka huu nia halisi ya mgomo wa walimu ili wapandishiwe mshahara ilionekana.
4. Mwaka 2010 pia watoto walilipiwa ada ya mtihani na serikali, kwa hiyo ni lazima serikali ifanye kila linalo wezekana.
5. Mwaka 2011 hawa watoto pia hawakuwa na mtihani wa form two, na mgomo baridi wa walim uliendelea kushika kasi.
6. Mwaka 2012 mgomo wa walimu uliingia hadi vijijini na kuanza kuingia mioyoni mwa walimu na mwaka huo huo kulikuwa na mgomo dhahili wa walimu japokuwa ulikatizwa.
7. 2012 huu mwaka licha ya kuwa na mgomo dhahili wa walimu, pia mwaka huu kulikuwa na sensa iliyo chukua mwezi mzima, what do you expect from these two?
8. Mwaka 2013 up to date mgomo wa walimu (mgomo baridi) umeingia uvunguni mwa mioyo ya walimu, na hivi sasa nao wamefunga EFD/LUKU kwenye ufundishaji siku hizi walimu wanasema FUNDISHA KADRI UNAVYO LIPWA (FUKU).
9. Kuna sababu zingine nyingi, kama miundombinu mibovu, mazingira yasiyo rafiki katika ufundishaji, na nyingine nyingi.

10. Slogani mpya ya serikali ya "SIASA KWANZA ELIMU BAADAE" nayo imechangia kwa kiasi kikubwa, kusema kweli wakuu wa shule wanapata tabu sana na hawa watu waitwao madiwani.

Mie ni hayo tu wandugu, i stdand to be corrected.
 
nakataa kwani mitihani ya 2010 kushuka maswali yalikuwa yanarudiwa sana hata wewe shahidi hivyo aliye solve past papers ndiye aliefaulu,,1.7 zilikuwa za kumwaga na vijana wengi wa govn walikuwa wanakariri sana almaarufu kumeza,,,hivi sasa mtaala sio content based bali competence ka hujui kaulize necta,,na hii ndo ilifanya 2011 na 12 wafeli kwani waliikuta wakiwa form 3 na 4,,,vitabu vya sasa (kuanzia 2012) ni bora na competence based,,,masuala ya kukariri hayahitajikini tena bali uelewa wako wa mambo,,,
 
watu mmnatoa reason bila ya uzoefu ni hili swala,,,reason ni moja tu,,,elimu ya 2011 kuenfelea ni competence based,,na hawakujiandAa both students,necta and moe,,,elimu ya 2010 kushuka chini ilikuwa content based maswali yanarudiwa kama hawana akili,,wamezaji ndo walikuwa TO ,,,
 

Hata hivyo hakuna competence ambayo wanaitekeleza, huwa nnaangalia mitihani yao, labda kwa vile mie nmezoea sayansi ndio maana naona hali ni ile ile, pia maswali ya competence ni rahisi kwa sababu mtu yeyote alie elewa anauwezo wa kujibu.
 
Hata hivyo hakuna competence ambayo wanaitekeleza, huwa nnaangalia mitihani yao, labda kwa vile mie nmezoea sayansi ndio maana naona hali ni ile ile, pia maswali ya competence ni rahisi kwa sababu mtu yeyote alie elewa anauwezo wa kujibu.

its better na ya sasa kuliko zamani
 

kama nimfuatiliaji wa elimu hii ya tanzania vizuri utagundua wasomi ni wale walio maliza mwaka mmoja wa 2009 tu kwa sababu kuu mbili.

1.mitaala yote ilibadilika ghafla 2009 huku wanafunzi wakiwa karibu kabisa kufanya mtihani wa necta ..nakumbuka mwezi wanane wali pitisha mabadiliko hayo ..hali ambayo ili zikost sana shule za kata kutokana na kuchelewa kwa kufuatilia na kuingiza mitaaala hiyo.
Hivyo ilikuwa mwanafunzi aliye maliza sent kayumba akapata dv four ya 26 ...akiingia advance anakimbiza kinouma.

2.mabadiliko ya marks yalianzia hapo.
Mfano history; physics; math, na kadhalika section c ambayo unatakiwa kujibu maswali matatu miaka ya nyuma kuanzia 2008 kurudi nyuma maswali yote yalikuwa na marks 60 katika section hiyo lakiani kuanzia 2009 wakapunguza mpaka marks 45 kwa maswali hayo na sasa wameleta kitu kipya kabisa CA?
 
Waishukuru siasa ndo imewafaulisha japo ndo chanzo cha kupata madaktar feki
 
kwa elimu tulonayo sasa ni mbaya kwani wanafunzi hawaumizi kichwa sana ukipata tu point 30 unaenda zako advance wakati kipindi kileee unaumiza kichwa chuo gani niende.
 

kwa hiyo una maana kuwa waliomalza mwaka 2010 na kuendelea wako competent? mhh...lazima utakuwa miongoni mwao
 
Msomi ni mtu wa aje? Form 4 2005!am sure hata doctorate huna

Kwa kizazi cha sasa usomi ni kujua kuandika,kusoma,kuhesabu! iam sure kuanzia mwaka 2008-hasa mwaka 2013 hata wale wasojua kusoma,kuhesabu,na kuandika(3Rs) watakuwa wamefaulu kwa madaraja ya juu,au nadanganya wakuu?
 

hapo no2 sio kweli paper ya f2 imefutwa mwaka 2008, watu ambao hawakufanya ni hawa waliomaliza f4, 2010
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…