waliomo kwenye Tume ya Katiba mpya

waliomo kwenye Tume ya Katiba mpya

friendsofjeykey

Senior Member
Joined
Aug 12, 2010
Posts
129
Reaction score
13
Hivi mnawajua waliopo kwenye hili jopo ni akina nani?

haya ndio matatizo ya kutokuwa na open Government
website ya Wizara ya Sheria haisemi kitu (infact iko down)
 
Hivi mnawajua waliopo kwenye hili jopo ni akina nani?

haya ndio matatizo ya kutokuwa na open Government
website ya Wizara ya Sheria haisemi kitu (infact iko down)
Watachaguliwa kutokana na ushauri utakaopendekezwa na Lowassa na Rostam! Mark my words... na niko serious!
 
Wanaoendesha nchi ni ra na el kwa hiyo lazima washirikishwe
 
Mkuu unatoka ndani ya system nini?
Ntajuaje aliyechaguliwa katokana na uliowataja?
Mkuu... hata hili suala la katiba mpya mratibu wa mambo yooooooote ni Lowassa. Lowassa aliongea na Kikwete akamwambia njia nzuri ya kushughulikia hili "tatizo" la katiba mpya ni kujihami. Wawahi mapema kushika usukani kwani wakichelewa na wananchi wakiongozwa na wapinzani wakiushika hawatakuwa tena na "control" ya chombo.
Na hii tume.. wewe fuatilia.. mambo yoooote yatapelekwa kimpangilio na kiakili.... ili yaifaidishe CCM (soma mafisadi). Na zimetengwa fedha nyingi sana kwa ajili ya ku-influence wajanja wachache watakaopiga kelele mchakato utakapoenda ndivyo sivyo... Tusibiri tuone kwani hizi info nimepewa na mtu "wa ndani" kabisa.
 
By the way si ulisikia siku Lowassa alipoongea kanisani na kusema anamshukuru Mungu kwa kumvusha vikwazo vigumu. Halafu akaenda mbali zaidi na kusema sasa ni wakati muafaka wa kuangalia katiba yetu? Sasa wewe inakujia akilini kweli Lowassa atake kujinyonga mwenyewe.... kwa kudai katiba nzuri? Kwa sababu kama leo itaandikwa katiba inayofaa, na ndoto zake za 2015 zitayeyuka moja kwa moja!
 
JK alisema ataunda kama nilimsikia vizuri sidhani kama alisema ameshaunda hiyo kamati maana najua akishaunda tu lazima majina yatakua hadharani sio jambo la siri hilo.
 
Prof issa shivji kusaidiana na dr slaa wanafaa kuongoza tume ya katiba mpya
Kama jk anataka kweli kuondoa fitina na kulitakia mema taifa hili-basi watu hawa wawili wanafaa kabisa kwa vyovyote na kwa maslahi ya umma kuongoza tume ya katiba mpya.

1. Prof issa shivji amekuwa katika mchakato wa kudai katiba mpya kabla na baada ya mfumo wa vyama vingi. Sio mnafiki, hanunuliki kama wasomi wetu wengi -anayetaka ukweli asome raia mwema la wiki ya jana atapata ukweli huu kutoka katika makala yake. Hayumbishwi. Nampendekeza awe mwenyekiti wa tume hiyo

2. Dr w. P. Slaa ni mtanzania mwenye msimamo aliyesababisha chachu ya katiba mpya, kama ilivyo kwa shivji slaa(phd) hanunuliki na hayumbishwi. Ni mtanzania aliyekuwa anagombea urais agenda yake kubwa ya kwanza ikiwa ni kuanzisha mchakato wa katiba mpya. Ni mtanzania anayeona mbali na anayeitakia mema nchi hii, mwenye kuchukizwa na umaskini, ufisadi, ujinga, na maradhi ya nchi. Huyu anafaa kuwa katibu wa tume hii -aombwe ashiriki hatakama yeye mwenyewe hakubaliani na approach ya serikali ya jk. Lakini kwa jk kumuomba na kumtumia katika tume hii wote wawili watakuwa wameweka historia ya aina yake kwa maslahi ya umma.

Tunao watanzania wengine kama jaji kisanga,ulimwengu, ayoub lioba, amiri maneto, bomani -hawa wanaweza kutumika kama wajumbe pamoja na mama nkya, ila hoja kubwa ni kutaka watanzania wazalendo wa kweli -nilisikitishwa na tume ya bomani ya madini ambayo mpaka leo bado wizi wa madini unaendelea -ndio maana slaa(phd) hataki tume hizi kwa kuwa zinakuwa hazipo huru.

Haya ni maoni yangu na ninaamini wapo wana jf watakubaliana na mimi kwa kupitia reference ya tume zilizowahi kuundwa huko nyuma na matunda yake.​
 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Frederick Werema, ambaye alihoji "Katiba mpya ya nini?" kwa mujibu wa cheo chake kama mshauri mkuu wa masuala ya sheria wa serikali lazima awe mjumbe wa Constitutional Review Commission ambayo Rais Kikwete anatarajia kuiunda.

“Tunapaswa kujiuliza Watanzania wanahitaji nini? Mimi binafsi ukiweka wadhifa wangu kando, bado sioni haja ya Katiba mpya, lakini kama ni Watanzania wanataka mpya sawa, wakitaka marekebisho pia sawa,” Werema alikaririwa akisema na gazeti la serikali, Habari Leo.

“Kila mtu anazungumza kama bata, watu wanazungumza kibatabata, lazima tujiulize Watanzania wanataka nini? Wakati fulani iliwekwa vifungu vya haki za binadamu kuanzia kifungu cha 12 hadi 29 kwa kuwa vilihitajika, tuzungumze si kutishana,” alisisitiza Jaji Werema huku akitolea mfano Katiba ya India ya mwaka 1948 iliyofanyiwa marekebisho mara 50.

Sasa kwa msimamo wake huu, sidhani kama mchango wa AG kwenye tume ya kupitia katiba kama utakuwa na tija.

Huko kwa jirani zetu kenya, wao waliunda Committee of Experts kuandaa katiba mpya. Bofya hapa ili kupata taarifa za uzoefu wa Kenya kwenye katiba mpya:

About us

Wajumbe wa kamati hiyo ya Kenya ya kupitia katiba walikuwa hawa hapa:

Profiles of members of the Committee of Experts

Nimevutiwa na kauli mbiu yao -- Katiba mpya ni SASA kama siyo SASA ni SASA HIVI!.

Katiba Mpya, Tanzania Moja
...
 
Rais kasema juzi tu katika hotuba yake ya kukaribisha Mwaka Mpya kuwa ataunda Tume itakayofuatilia Katiba Mpya. Alisema wadau wote, wakiwemo wanasiasa, wafanya biashara, viongozi wa dini na wananchi wengine watakuwepo. Tumpe muda, na papo hapo tuanze kujiandaa kuchangia wakati hiyo Tume itakapotutembelea.

Mimi naandaa Mada yangu ya Maboresho ya Katiba nitakayotoa kwa Tume.
 
Back
Top Bottom