Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 753
- 1,812
Askari polisi watatu pamoja na raia sita akiwemo mfanyabiashara maarufu wa Madini a Tanzanite, Lucas Mdeme wanaotuhumiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi wamekiri makosa kwa kuandika barua kwa DPP.
Wameandika barua ya kukiri mashataka sita wanaokabiliwa nayo ikiwemo uhujumu uchumi, utakatishaji fedha haramu na kupanga njama za kujipatia fedha ya awali shilingi milioni 10 kati ya milioni 30 walizohitaji kutoka kwa Sammy Mollel
Watuhumiwa hao ambao walifikishwa mahakama hapo mapema leo kabla ya kuahirishwa, wakili wa utetezi Charles Kagirwa mara baada ya hakimu wa kesi hiyo kusema upelelezi wa kesi hiyo unaendelea ndipo wakili huyo alisema kuwa wateja wake tayari wameaandika barua ya kukiri mashtaka hayo.
Hata hivyo waendesha mashtaka wa serikali Adelaide Kassalay na Agnes Hyera walimweleza Hakimu Ngoka kuwa wanaomba tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwani upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.
Hakimu mkazi mfawidhi wa Arusha,Rose Ngoka amesema kuwa kesi hiyo namba 3/2021 imeahirishwa hadi February 24 mwaka huu kwaajili ya kutajwa hivyo watuhumiwa wataendelea kukaa rumande katika gereza la kisongo kwa kuwa kesi hiyo haina dhamana .
Januari Saba Mwaka huu Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu kushikiliwa kwa Askari polisi Watatu na Raia Sita kwa tuhuma za kushawishi na kupokea rushwa kutoka kwa Mmiliki wa Kampuni ya Germs and Rocks Ventures iliyopo Jijini humo.
Askari wanaotuhumiwa kujihusisha na tukio hilo ni Askari Polisi Intelijensia Mkoa wa kinondoni mwenye namba G.5134 DC Heavenlight Mushi,Askari Polisi Intelijensia Makao Makuu H.125 DC Gasper Paul na Askari Polisi Kazi za kawaida Mkoa wa Dodoma H.1021 PC Bryton Murumbe ambao wamefukuzwa kazi ndani ya Jeshi hilo.
Wameandika barua ya kukiri mashataka sita wanaokabiliwa nayo ikiwemo uhujumu uchumi, utakatishaji fedha haramu na kupanga njama za kujipatia fedha ya awali shilingi milioni 10 kati ya milioni 30 walizohitaji kutoka kwa Sammy Mollel
Watuhumiwa hao ambao walifikishwa mahakama hapo mapema leo kabla ya kuahirishwa, wakili wa utetezi Charles Kagirwa mara baada ya hakimu wa kesi hiyo kusema upelelezi wa kesi hiyo unaendelea ndipo wakili huyo alisema kuwa wateja wake tayari wameaandika barua ya kukiri mashtaka hayo.
Hata hivyo waendesha mashtaka wa serikali Adelaide Kassalay na Agnes Hyera walimweleza Hakimu Ngoka kuwa wanaomba tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwani upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.
Hakimu mkazi mfawidhi wa Arusha,Rose Ngoka amesema kuwa kesi hiyo namba 3/2021 imeahirishwa hadi February 24 mwaka huu kwaajili ya kutajwa hivyo watuhumiwa wataendelea kukaa rumande katika gereza la kisongo kwa kuwa kesi hiyo haina dhamana .
Januari Saba Mwaka huu Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu kushikiliwa kwa Askari polisi Watatu na Raia Sita kwa tuhuma za kushawishi na kupokea rushwa kutoka kwa Mmiliki wa Kampuni ya Germs and Rocks Ventures iliyopo Jijini humo.
Askari wanaotuhumiwa kujihusisha na tukio hilo ni Askari Polisi Intelijensia Mkoa wa kinondoni mwenye namba G.5134 DC Heavenlight Mushi,Askari Polisi Intelijensia Makao Makuu H.125 DC Gasper Paul na Askari Polisi Kazi za kawaida Mkoa wa Dodoma H.1021 PC Bryton Murumbe ambao wamefukuzwa kazi ndani ya Jeshi hilo.