Waliotegemea malipo ya uzeeni ujanani sasa tena basi! Ufafanuzi kutoka Mamlaka - SSRA

Zito kabwe, mnyika, nchemba, kingwangala etc najua mpo humu? Hili mlipitisha? Tunaomba majibu?
 
Duh watunga sheria wetu sijui wakoje. Life span yenyewe imepungua sana. Anyway ndo sheria zinazotungwa na watu kama nhemba, lusinde, maji marefu na kupigiwa chapuo na Werema. Tutegemee makubwa zaidi
 
hivi hnyama vya wafanyakazi vinatambua hili? Mbona avilizungumzii hiki? Kuna umuhimu wa kutokuchangia tena wakuu! Huu ni wizi wa waziwazi...
 
Wanakopa hela za kuwalipa wafanyakazi wa Serikali Mishahara kwenye hii mifuko hadi inafilisika.
 

Sijaona mtu akifariki inakuwaje au naye anasubiri 55 years? What a shame. Huu uwe mtaji kwa chadema kupata kura zaidi za wafanyakazi
 
Sijaona mtu akifariki inakuwaje au naye anasubiri 55 years? What a shame. Huu uwe mtaji kwa chadema kupata kura zaidi za wafanyakazi
Walisimamie kulipinga hili kwa nguvu zote,wafanyakazi wote tuwaunge mkono...lakini wap vyama vya wafanyakazi? Hawajalijua hili?
 
Bila kuwa na sheria ya Unemployment Benefits (au inayofanana na hiyo) hili sio wazo zuri hata kidogo.

Elimu ya umma kuhusu swala hili ni muhimu itolewe kwa haraka na kwa upana na uwazi sana haraka iwezekanavyo ili kuzuia taharuki na wasiwasi unaoweza kutokea kutokana na uelewa mdogo wa wananchi wa sera hii na athari za opportunists ambao watependa kupindisha ukweli kwa maslahi yao binafsi. Irene jenga imani kwa wananchi ili wakuamini; hili ni swala nyeti sana kwa sababu linagusa mafao ya wananchi hasa wale wa kipato cha chini. Historia haitakuonea huruma katika hili ikiwa utatumbukia katika mtego wa ujanja ujanja ambao kwa sasa it appears to be the practise rather than the exception in Tanzania, the public is watching!!
 
Jambo moja muhimu hapa ni kwamba sheria ni MKATABA. Utaratibu huu ni mpya hivyoi ni lazima uhusike na michango ya kuanzia pale ulipotangazwa onwards. Kisheria kuna hoja hapo.
Huwezi kuimpose new terms on existing contract UNILATERALLY. Wanasheria tutoeni kifungoni.
 
washaniaribia mipango yangu.......nasikia hasira mpaka basi,nachukia kuwa mtanzania kwa kweli....
 
Mi nashaang'aa hii nchi inavyoendeshwa...
Hapa itakuwa hawa jamaa wa serikari wamechota hela kwenye hizo fund wakashindwa kurudisha wkt watu wanadai hela zao ndo wakaona waitungie sheria.
Du!ama kweli hii nchi!
Ripoti ya CAG ilisema wazi Serikali imeshindwa kulipa mabilio ya pesa ilokopa kutoka NSSF au pale ilipodhamini mikopo kutoka NSSF. Ni NSSF wamejenga Udom, wamekopesha Gen Tyre, Daraja la Kigamboni nk.
Sasa mtu umeachishwa kazi, utasubiri 55 yrs
? Daini haki zenu.
 
Huu ni wizi wa mchana kweupee!!Yaani nikiacha kazi kabla ya miaka 55 hela mnayonikata kila mwezi mnaichukua nyie?Au labda sijaelewa vizuri?
Miaka michache iliopita niliamua kufanya maamuzi magumu. Nilichukua balance yangu NSSF nikakuta nina 8m, riba wameweka elfu 8! Yaani interst hairudishi hata kushuka thamani kwa shilingi! Baada ya 2yrs nikaacha kazi nikazoa milioni zangu nikaziwekeza mahali ambapo napata laki 8 kila mwezi, si haba.
 
Lakini kwa utaalam wangu wa sheria,hii sheria haipawi kuapply kwa wanyakazi waloajiriwa kabla ya kuanza kufanya kazi kwa sheria hii.

Hii itakuwa retrospective,na sheria yoyote haipaswi kuapply retrospective.

Hivyo basi,kwa maoni yangu tunaweza kuichallenge hii sheria mahakama kuu kwa ground kadhaa.kama ifuatavyo
1. Kwanza ni hiyo ya retrospective
2. Pili ni kuwa inahatarisha haki mbalimbali za msingi kikatiba,kwa mfano,right to life na hivyo ni unconstitutional.

Remedy yake ni kuwa declared unconstitutional na kuwa nullified.

Tundu lisu,LHRC mko wapi?
 
Jana kumetokea mtafaruku mkubwa sana Mgodini Nzega. Kwani wafanyakazi wa Kampuni ya Caspian woote waliamua kuachakazi, kwa kuandika resignation ya 24hrs, wakarudisha mashine toka site na kurudi ofisini kumkabidhi mkuu wao hizo barua. Hii yote imetokana na taarifa hizi za SSRA, imesababisha Management ichanganyikiwe na Production ilisimama kwa masaa 3 hivi, na sasa Kampuni ya Resolute na Caspian zimetuma wawakilishi Dar ili Kupata ukweli juu ya hali halisi.

Nasikia huko Nzega taarifa zinasema eti SSRA, itaanza kuitumia sheria hii kuanzia tarehe 1 Oktoba 2012 ndo maana wafanyakazi huko Mgodini wameamua kuacha kazi sasa na kwenda kuchukua mafao yao kabla ya Oktoba Mosi.
 
Basi wapunguze umri wa mtu kustaafu kwa hiari uwe miaka 35 manake life expectancy ya Mtanzania ni arround 40's..
 
hili nipigo kwangu na kwajamii kwa ujumla nilipanga kuacha kazi za kuajiriwa mwisho mwa mwaka huu ili vijisenti vyangu viniwezeshe kuendeleza kijikampuni changu..daah wabunge hili mlilipitisha kweli
 
 
hili nipigo kwangu na kwajamii kwa ujumla nilipanga kuacha kazi za kuajiriwa mwisho mwa mwaka huu ili vijisenti vyangu viniwezeshe kuendeleza kijikampuni changu..daah wabunge hili mlilipitisha kweli
Huu utakuwa ni ujinga. Unaacha kazi kwa kutegemea 20% ya contributions zako ndio uendelezee kampuni!!!

Hii sheria ya SSRA nimeipenda. Itasaidia sustainability ya mifuko yetu na pia wanaweza kuplan vizuri especially kwenye long term investmennts.
 
Nimejaribu kuipitia hiyo sheria, sijaona hicho kipengele maana kipengele cha 37 bado kinazungumzia kuwepo kwa mafao ya muda mfupi na muda mrefu. Last week mimi nimepeleka madai yangu nssf ila hawajaniambia hicho kitu mbali ya kusema wameipokea na wataifanyia kazi. Kesho asubuhi naenda kuwaona
 
Sheria tayari imeshaanza kutumika. Wasubiri tu mpaka wafike 55 yrs voluntary au 60 yrs compulsary!
 
Huu utakuwa ni ujinga. Unaacha kazi kwa kutegemea 20% ya contributions zako ndio uendelezee kampuni!!!

Hii sheria ya SSRA nimeipenda. Itasaidia sustainability ya mifuko yetu na pia wanaweza kuplan vizuri especially kwenye long term investmennts.

Aisee. Nimejaribu kama dakika 10 kutafuta maneno makali ya kukujibu nimekosa. Yote naona yatapelekea nilimwe kifungo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…