HABARI KUTOKA BODI YA MKOPO
Muda wa kuomba
mkopo kwa wanafunzi wa vyuo vya
elimu ya juu imefikia mwisho wiki
iliyopita, Julai 30, huku wanafunzi 17,
406 kati ya wanafunzi 115,431
walioomba mikopo hiyo, wakiwa
hatarini kukosa.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Bodi ya
Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
(HESLB), Cosmas Mwaisobwa,
amefafanua kwamba mpaka wakati wa
kusitisha kupokea maombi kwa mwaka
huu, wanafunzi 54,370 ambao ni
waombaji mikopo wa mara ya kwanza
walikwishakamil isha maombi yao.
Mbali na hao wa mara ya kwanza,
Mwaisobwa aliyezungumza na gazeti hili
wiki iliyopita, alisema pia wanafunzi
61,061 wanaoendelea na masomo yao
katika vyuo vya elimu ya juu, walituma
maombi ya kutaka bodi hiyo kuendelea
kuwakopesha.
Kutokana na hali hiyo, Bodi imejikuta
ikipata maombi ya wanafunzi 115,431,
wakati ina bajeti ya kudhamini
wanafunzi 98,025 kwa mwaka wa
fedha 2013/14, ambayo hata hivyo ni
ongezeko la asilimia 2.4.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Dk Shukuru Kawambwa, aliposoma
bajeti ya wizara hiyo hivi karibuni,
alisema Serikali kupitia HESLB, itatoa
mikopo kwa wanafunzi 35,649 ambao
ni waombaji wapya na 62,376
wanaoendelea.
Kwa bajeti hiyo, inaonekana wanafunzi
wengi watakaokosa mikopo ni
waombaji wapya, kwa kuwa wakati
bajeti ya Serikali ilijielekeza kuwapa
mikopo wanafunzi wanaoendelea
62,376, walioomba ni pungufu ya hao
kwa kuwa wako 61,061.
Mwaka wa fedha uliopita, wanafunzi
98,773 waliwasilisha maombi na kati
yao, 95,594 ndiyo waliopata mikopo.
*Chanzo Habarileo Gazet tar 05/08/2013