waliowekwa ndani kwa ajili ya sensa waachiwe

waliowekwa ndani kwa ajili ya sensa waachiwe

nkisumuno

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2012
Posts
208
Reaction score
72
ushauri wangu wale wote waliowekwa ndani kwa sababu ya sensa naomba waachiwe huru kwani hata wangekuwepo mtaani wasingehesabiwa kwani vifaa vimeisha. wale wote waliohusika kukwamisha zoezi la sensa kwa kuchakachua vifaa hao ndo wawekwe ndani tukianzia na kamishna kwani haiwezekani maandalizi ya miaka mingi halafu ionekane kama ni ya siku moja.

Iundwe tume ya uchunguzi ikishirikisha vyombo huru itabainika uovo na ufisadi uliotumika. makarani tumekosa hata tshirt, kofia na hata ukiona vitambulisho hutaamini, mabegi ya kichina, kazi ngumu lakini malipo yake kidogo. Kwa vile muda Unaelekea ukingoni makarani tusikubali kuendelea na kazi muda utakavyoisha labda iwe kwa makubaliano mengine maana serikali ndiyo chanzo cha yote hayo.

Inakuwaje serikali inakosa madodoso imekuwaje? nani alipewa tenda hiyo? Mbona wanakula na kuiba pesa bila hata kufikiri nchi gani hii? Kujitapa eti kuna mafanikio sana. Labda mafanikio ninayoyaona nimwitikio wa wananchi lakini makarani tumekosa vifaa hizo ndo changamoto ndogo kama tunavyoaminishwa?
 
Hao waliokataa kuhesabiwa wakamatwe wote, wakaheshabiwe wakiwa mahabusu!
 
Hamna haja ya kuwaachia kwasababu wamefanya makosa chini ya sheria za sensa za mwaka 2002! Wawe fundisho kwa wengine katika sensa zijazo.
 
ushauri wangu wale wote waliowekwa ndani kwa sababu ya sensa naomba waachiwe huru kwani hata wangekuwepo mtaani wasingehesabiwa kwani vifaa vimeisha. wale wote waliohusika kukwamisha zoezi la sensa kwa kuchakachua vifaa hao ndo wawekwe ndani tukianzia na kamishna kwani haiwezekani maandalizi ya miaka mingi halafu ionekane kama ni ya siku moja.

Iundwe tume ya uchunguzi ikishirikisha vyombo huru itabainika uovo na ufisadi uliotumika. makarani tumekosa hata tshirt, kofia na hata ukiona vitambulisho hutaamini, mabegi ya kichina, kazi ngumu lakini malipo yake kidogo. Kwa vile muda Unaelekea ukingoni makarani tusikubali kuendelea na kazi muda utakavyoisha labda iwe kwa makubaliano mengine maana serikali ndiyo chanzo cha yote hayo.

Inakuwaje serikali inakosa madodoso imekuwaje? nani alipewa tenda hiyo? Mbona wanakula na kuiba pesa bila hata kufikiri nchi gani hii? Kujitapa eti kuna mafanikio sana. Labda mafanikio ninayoyaona nimwitikio wa wananchi lakini makarani tumekosa vifaa hizo ndo changamoto ndogo kama tunavyoaminishwa?
Ebwana nakuunga Mkono mi mwenyewe nimeyaona hayo: Serikali hakujipanga flesh swala hili maana kama inauwezo wa kusimia mambo mengine kama Vitambulisho kura n.k kwann hili lishindikane!!!? Makarani wanateseka pesa imechakachuliwa kuanzia ngazi juu mpaka kwa Watendaji!!
 
Back
Top Bottom