Walivyo wajinga wamedanganywa wao ni bora kuliko Bingwa wa Super Cup USM Algers

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Najua ukiwa chizi huwezi kuona kweli nyingi zaidi ya kuwa na picha ya uongo kuhusu we mwenyewe. Kuna magonjwa ya akili yanasababisha kitu kinachoitwa "Delusion of grandeur", mtu kujisikia ni muhimu kuliko uhalisia ulivyo.

Habu fikiria timu ambayo zaidi ya miaka 20 haijatinga makundi club bingwa, walifanikiwa kucheza fainali ya CAF lakini eti ubora wao ni mkubwa kuliko aliyechukua kikombe. Aliyebeba kombe ni wa 10 huku wao ni wa 3.

USM Algers pia wamefanikiwa kubeba ndoo dhidi ya Al ahly lakini kwa mujibu wa waliodanganywa, hawa sio bora kama wao.

Wenye akili wawili bado hawajasema, huenda wakisema tutaelewa.
 
Wakati CCM wanaanzisha shule ya Katiba miaka 3 ni vema tutumie nafasi hiyo kutoa elimu ya ushabiki wa soka Kwa miaka 2.
 
Mmeumbuka mbwiga nyie, si mlisema Yanga alikutana na timu mbovu? Sasa mmeanza kujihami.
 
Kupata vichekesho zaidi tembelea mitaa ya twiga na jangwani kwamba Yanga ni ya 3 kwa ubora Afrika na wakati ni miaka zaidi ya 20 haijaingia makundi Club Bingwa!
 
Aahaaaa, inakuuumaa
 
Bado hamjasema, tunatarajia mtasema zaidi. Msimu huu unao anza wa mashindano ya Caf tunakwenda kukaa pale juu kabisa.
Wale mnao waona wababe tunakwenda kuwatia adabu wote.

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Aaaahaaa,kolo wanahofu kuwa tunaenda kuachieve kitu amabacho wao kimewashinda Kwa miaka nenda rudi
 
Mtaendelea kutoka mapangoni wote
Scars tayari keshatoka
Namsubiri Okwi Boban,popoma, na Kolo 1979magufuli
Bado hamjasema kilichomtoa kanga manyoya
Hahahahahaha, jamaa wamevaa mkenge wa kuanzisha Nyuzi za Yanga ,wakijua wanawaponda kumbe wanawapa AIRTIME

wameisahau kabisa Timu yao
 
Mtatoka Sana mapangoni safari hii, mlisema yanga kacheza na timu dhaifu sasa leo mnajitokeza kwa aibu kutafuta kichaka kingine cha kujificha? Mbumbumbu ni mbumbumbu tu mnakuwaga na akili za kuvukia barabara tu!
 
Zile kelele Yanga alikua anakutana na timu dhaifu huko kwenu bado unazisikia maana Yanga alimfunga huyo usm alger kwao na kama si uchawi wa mvua wa makolo Yanga angemfunga usm hapo taifa kama alivyofanya 2018
 
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… yanga aliposhinda Algeria ilikuwa USM Algers ni wabovu, saizi kamkanda mme wenu Al Ahly imekuwa wao ni Bora kuliko Yanga! Hii ni dalili za mashabiki wa Simba kuugua kichaa Cha mimba changa ya yanga!!, Ngoja tuwaletee limao maona mate yanawatoka Sana mdomoni.
 
Bado mnaweweseka na rank za IFFHS tu? wakati hao hao IFFHS walipoweka rank kuwa Simba ipo juu zaidi ya Sevilla mbona hamkufungua nyuzi nyingi za kuwaponda IFFHS?

IFFHS ina deal na namba tu ndio maana wanaitwa international federation of football history and statistics, wanachokifanya wao ni kupima performance za timu katika michezo yote ya kimashindano wanayocheza yaani ya kitaifa na kimataifa. Wao wana record kila aina ya data inayohusiana na performance za timu mfano idadi ya clean sheets, idadi ya mechi ilizoshinda, idadi ya magoli ya kufungwa, idadi ya magoli yakufunga, n k kila data inachukuliwa katika mechi za ligi kuu, FA na mashindano ya kimataifa.

Narudia tena IFFHS wanapima performance za timu kwa mashindano yote anayoshiriki kitaifa na kimataifa (kila mwanachama wa shirikisho la soka lazima awe na mashindano ya ligi kuu na FA) tofauti na ilivyo kwa shirikisho la CAF wao wana deal na mafanikio ya timu katika mashindano ya CAF
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…