Wallace Karia aula, ashinda ujumbe wa kamati tendaji Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF)

Wallace Karia aula, ashinda ujumbe wa kamati tendaji Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia ameibuka mshindi wa kiti cha ujumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) katika uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo unaofanyika leo huko Cairo,Misri.

Karia ameshinda kwa kura nyingi za ndio kwa vile alikuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo kuwakilisha kanda ya soka ya Baraza la vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (Cecafa).

Katika hatua nyingine, Rais wa Caf, Patrice Motsepe amechaguliwa kuongoza tena shirikisho hilo kwa miaka mitano ijayo baada ya kupita bila kupingwa kama mgombea pekee wa nafasi hiyo.

Motsepe ataiongoza tena Caf kwa miaka minne hadi 2029 baada ya kumaliza awamu ya kwanza iliyoanza 2021.
 
Hakuna la maana ngoja kwanza tufungiwe kushiriki michuano ya kimataifa no itatusaidia.
 
Hakuna la maana ngoja kwanza tufungiwe kushiriki michuano ya kimataifa no itatusaidia.

Katika nchi ambazo ni ngumu kufungiwa ni Tanzania aisee.

Ni nchi kichocheo kukubwa cha mpira ukanda wa afrika mashariki.Mengi yatafumbiwa macho kwa mpira wa afrika
 
CCM oyeeeee!! Na Dabi ijayo mgeni wa heshima ni CHURA.
KAZI ni kipimo cha utu
 
Inaonekana hakukuwa na Uchaguzi huko

Yaani mtu anapita bila kupingwa, wakati Vijana wengi ni jobless 🙌
 
Vijana tumeshawaandaa kuwa mabaunsa na kuwapa kazi ya kuzuia mabasi ya timu pinzani yasiingie uwanjani
Hahaha............... hatari sana

Wakija kutahamaki, nafasi zote zimejazwa na Wazee 🤗
 
Inaonekana hakukuwa na Uchaguzi huko

Yaani mtu anapita bila kupingwa, wakati Vijana wengi ni jobless [emoji119]
Brother umenichekesha sana...mojawapo ya sehem ambazo hawajui neno ujobless ama kijana sijui anakuja kuomba kazi, ni huko ngazi ya CAF ..huko ni PESA YAKO na USHAWISHI ..au hata ukiwa na PESA tu ni silaha tosha. ...unamuona SAMUEL ETO .alivyopita kimasihara hata baada ya kufungiwa mara kesi, si unaona ghafla kaachiwa, ghafla Kawa nae mjumbe wa kamati kuu CAF ..PESA ...MONEY..CASH...na niwaibie Siri, baada ya BILIONEA Motsepe kuondoka ni yeye ETO.
 
Back
Top Bottom