wadau wa soka moja kati ya vitu ambavyo naona ligi yetu tanzania inakosa ni walpaper za kutumia kwenye simu au pc. nimeanzisha hii thread kwa muda wangu ambao nipo free nitatengeneza walpaper za vilabu mbali mbali hapa tanzania na kwa kuanza leo nitaeka ya azam halafu simba na yanga zitafuatia. challenge kubwa ninayopata hakuna picha za wachezaji zenye quality kubwa kama kuna mtu anafahamu source ninayoweza kuapata anaweza kunisaidia kwa kunipa link.
unatakiwa uwe na software ya kuedit picha kama photoshop au gimp, then ujifunze basics zote kama kukata picha, kuikuza, kuimove na kucheza na layers ndio utaweza kutengeneza kitu kama hicho hapo juu. ni vigumu kukuelekeza kwa maneno hapa ila kama una muda na internet nzuri youtube itakusaidia sana.
nenda youtube halafu search photoshop tutorial yatakuja mafundisho mbali mbali angalia ambayo unaona ni rahisi kwako jifundishe taratibu