Wamakonde tafadhalini sana, laana itawafuata na hata milele

Wamakonde tafadhalini sana, laana itawafuata na hata milele

NIMEONA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2019
Posts
3,862
Reaction score
5,693
Nawahusisha wamakonde wote wote katika mada hii na dharau anayoipata HALILA TONGOLANGA--FIELD MARSHAL TONGOLANGA (R.I.P)

1. Aliwatambulisha sana wamakonde Tanzania hii kupitia sanaa yake. 'kila munu ave na kwao' miaka ile ilifanya wamakonde mfuatwe majumbani kule dar na watu mbalimbali wa makabila mengine wakitaka kutafsiriwa maneno yaliyotumika mle.......kimakonde haikuwa lugha ya ajabu tena masikioni mwa watu.

2. Ngoma yenu ya asili, 'sindimba', nayo ikazidi kupaa kupitia yeye!

3. Ile kitu 'chilambo cha vene' nasikia mpaka pride fm ya huko mtwara wakaichukua na kuitumia katika kipindi flani. aisee huu wimbo hata mimi unanikosha sana.....bahati mbaya sijaupata

4. Miaka flani ya 2006 hivi nilipita maeneo mengi yanayokaliwa na wamakonde......tandahimba, newala, mtwara, baadhi ya maeneo ya lindi vijijini km vile mtama, litehu, chiuta, mandwanga, mnyambe, lindwandwali, namindondi, mbindo, madingo, malungo, nahukahuka, nyangamara, litipu, linoha, ngunja, mabeti, luagala n.k. sehemu zote hizo walikuwa wanajivunia na kuburudika sana nyimbo za Tongolanga.....nyingi tu (snura n.k)!

Ni mwaka wa nne sasa tangu huyu mwamba afariki 2017😭😭😭😭....wamakonde wote KIMYAAA, kama hakuna lolote lililotokea! nasikia alikuwa anapita vijijini mwenu hata na miguu kuburudisha.

YAANI HAMTAKI HATA KUITANA HAPO DAR (MLIPOJAA KIBAO) MKAANDAA SIKU YA KUMBUKIZI YAKE NA ANGALAU MKAMUONE TU HUYO MAMA YAKE AMBAYE NASIKIA ANA HALI NGUMU SANA MKAMFARIJI?!!!!

nyie wamakonde, nyie wamakonde...........shauri yenu!!!!!

nb:
mwenye chilambo cha vene atupie humu tafadhali
 
Ilo jina nalikumbuka, ila bahati mbaya hakuna kazi yake hata moja ambayo ipo katika kumbukumbuku yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
kweli mkuu?!!! huyo jamaa alitoa kibao matata mno, ndo hicho ambacho kinaitwa kila munu ave na kwao......tanzania nzima ilipata habari yake. hata huyu 'tozi' wa sasa, harmonize, alikirudia na kilibamba vizuri tu sababu kiliibua hisia ambayo tayari ilishatengenezwa na ile original ya tongolanga. harmonize amejinasua katika kumuenzi. nimekereka kuona harmonize anafanyiwa mpaka matambiko, yaani anaheshimika mno huku mmakonde original yule wakimtupia kapuni
 
Inategemeana n'tu na n'tu maana ukichimama n'chale ukikaa n'chale_,Baah!!,,hahah Wamakonde kila mtu akiongea kule ni Comedian lazima ucheke,,Naenda Ngaran'toni njinii,,hehehe hawa jamaa
wahaya na wasukuma walioumbwa kushika Hera..Wanyakyusa wazee wa "fiatu fyangu"...wanaokaa karibu na mukuki yao huwajui?.......
 
Njombaa unaiba Nazi zangu? Sasa chikia, ukishuka nchale, ukipanda nchale, ukiganda nchale, ukicheka nchale, ukinuna nchale, ukifumba macho nchale, ukifungua macho nchale, ukishika Nazi nchale, ukiachia Nazi nchale, ukipumua nchale, usipopumua nchale......
 
Laana anatoa baba ako..........?,,wazanaki wana muenzi nyerere kivyao?......we chimbwa nini... Tuache kama tulivyo
hivi nawe nipoteze muda kukujibu?!!! si nitakuwa c.h.i.t.o.k.o (hili neno nilijifunza huko kwenu ktk miaka 2 niliyokaa) kama wewe!
 
Back
Top Bottom