Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
WAMANYEMA WA DAR ES SALAAM KATIKA TANU NA SIASA ZA KUDAI UHURU
Iddi Faiz Mafongo TANU Card No. 24 Iddi Tosiri TANU Card No. 25 Ndugu Wawili Katika Kupigania Uhuru wa Tanganyika, 1954
Wamanyema wanajulikana kama watu wenye harara na ya ushujaa.
Mmanyema anaweza kuulipia fedha ugomvi ili na yeye awemo, na kadri mpinzani anavyokuwa na nguvu na hodari, ndivyo Mmanyema anavyofaidi ugomvi wake.
Katika siku hizo Wamanyema walikuwa wameshikwa katika magomvi. Katika mwaka wa1941 ilibidi serikali, maimamu na masheikh wa msikiti mingine mjini Dar es Salaam kuingilia kati ili kuamua ugomvi uliowakumba Wamanyema kuhusu msikiti wa Manyema.
Msikiti huu Wamanyema waliujenga mwaka wa 1912.
Wamanyema hawakumstahi mtu yeyote, waligombana hata wenyewe kwa wenyewe.
Hamaki hizi zilipoelekezwa kwa serikali ya kikoloni zilikuja kuwa na manufaa sana.
Kwa kuwa walikuwa ni kabila la Waislam watupu, Wamanyema hawakuweza kufaidika na elimu iliyokuwa ipo mokononi mwa wamishionari.
Hata hivyo Wamanyema walipiga hatua kubwa katika elimu ya dini yao na hii ndiyo sababu kuwa hadi leo utamaduni wa Kiislamu umeenea katika kila familia ya Mmanyema iwe nyumbani Kigoma au huko pwani.
Mmanyema hayupo mbali sana na utamaduni wa Kiislam. Wamanyema, Warufiji na Wadigo ni katika makabila ambayo ni tabu sana kumpata Mkristo.
Iddi Faiz alikuwa Mmanyema.
Hadhi yake iliongezeka zaidi kwa kuwa alikuwa mweka hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na TANU.
Vilevile aliifanyia kampeni TANU, akifuatana na Nyerere katika safari za awali za kukitangaza chama, akihutubia mikutano jukwaa moja na Nyerere.
Ilikuwa ni Iddi Faiz na kaka yake Iddi Tosiri ndiyo waliompeleka na kumtambulisha Nyerere kwa binamu yao Sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo.
Ilikuwa ni baada ya utambulisho huu kwa Sheikh Ramia ndipo urafiki ukajengeka kati ya Sheikh Ramia na Nyerere na ndiyo Nyerere akakubalika Bagamoyo.
Sheikh Ramia akiwa khalifa wa tariqa ya Qadiriya alikuwa na murid wengi waliomfuata katika TANU kama kiongozi wao.
Juu ya hayo alikuwa miongoni mwa wanachuoni walioheshimiwa sana.
Hakuna kilichoweza kusimama na kuota mizizi Bagamoyo bila kupata ridhaa ya Sheikh Mohamed Ramia na hii ilikuwa toka wakati wa TAA.
Akiwa khalifa wa tariqa ya Qadiriya ambayo ilianzishwa na kustawishwa Bagamoya na baba yake, Sheikh Yahya Ramia, mwanzoni mwa karne ya ishirini, nguvu za Sheikh Ramia zilikuwa hazisemeki.
Alichosema sheikh ndicho hicho kilichofuatwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba IddI Faiz Mafongo alihudhuria mkutano wa uzinduzi wa TANU katika Ukumbi wa Arnautoglu mwezi Agosti 1954.
Haifahamiki kwa hakika hasa ni lini Iddi Faiz alijiunga na TANU kwa sababu kadi yake ya kwanza ya uanachama ilipotea na akapewa kadi nyingine iliyokuwa na namba 915 iliyotolewa tarehe 28 Agosti, 1954.
Lakini kwa kukisia tu kutokana na kadi ambayo Iddi Faiz mwenyewe aliitoa kwa kaka yake Iddi Tosiri ambayo ilikuwa kadi namba 25 na yenye saini yake kama afisa aliyetoa kadi hiyo, inaweza kuchukuliwa kwa uhakika kuwa Iddi Faiz alikuwa miongoni mwa wale watu wa mwanzo kabisa kuingia TANU na huenda akawa miongoni mwa wanachama ishirini wa mwanzo.
Ukichukua katika fikra ukweli kwamba Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa katibu wa Al Jamiatul Islamiyya aliingizwa TANU na Mtemvu katikati ya mwezi Agosti, 1955, huenda Ali Mwinyi kama katibu wa Al Jamiatul Islamiyya na Idd Faiz akiwa mweka hazina, wote wawili waliingia TANU wakati mmoja.
Iddi Faiz na nduguye Idd Tosiri, muasisi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, walikuwa Wakusu, moja ya makabila ya Kimanyema, kwa upande wa baba yao; na Wabwali kwa upande wa mama yao.
Wote wawili walikuwa katika Batetera Union (Congo Association), chama kilichokuwa kikiwaunganisha Wamanyema wa Tanganyika.
Mzee bin Sudi alikuwa rais muasisi wa chama hicho na baada ya kifo chake Sheikh Hussein Juma alichaguliwa kushika nafasi hiyo.
Batetera Union (Congo Association) kilikuwa chama kilichoshikamana na chenye nguvu sana miongoni mwa vyama vya kikabila vilivyokuwapo wakati wa ukoloni.
Wamanyema ni kabila la Waislam watupu na kwa sababu hii hakukuwa na pingamizi katika kuunga mkono TANU.
Batetera Union kilikuwa na nguvu sana kiuchumi kwa kuwa kilikuwa katika wafuasi wake, watu waliomiliki majumba na walihodhi takriban nusu ya nyumba zilizojengwa mjini Dar es Salaam kati ya vita kuu mbili za dunia.
Uwezo huu wa kiuchumu uliwafanya Wamanyema kuwa wapinzani wagumu wa serikali ya kikoloni na uliwanyanyua hadi kufikia kuwa mbele katika siasa mjini Dar es Salaam na katika miji mingine ya Tanganyika.
Umoja wa Wamanyema ndiyo uliojenga msikiti maarufu wa Wamanyema mwaka wa uliokuwa karibu na makao makuu ya African Association.
Mzee bin Sudi alikuwa rais muasisi wa chama hicho na baada ya kifo chake Sheikh Hussein Juma alichaguliwa kushika nafasi hiyo.
Mzee bin Sudi alikuwa pia ni muasisi wa African Association mwaka wa 1929 pamoja na Kleist Sykes.
Batetera Union kilikuwa chama kilichoshikamana na chenye nguvu sana miongoni mwa vyama vya kikabila.
Wamanyema ni kabila la Waislam watupu na kwa sababu hii hakukuwa na pingamizi katika kuunga mkono TANU.
Batetera Union kilikuwa na nguvu sana kiuchumi kwa kuwa kilikuwa katika wafuasi wake, watu waliomiliki majumba na walihodhi takriban nusu ya nyumba zilizojengwa mjini Dar es Salaam kati ya vita kuu mbili za dunia.
Uwezo huu wa kiuchumu uliwafanya Wamanyema kuwa wapinzani wagumu wa serikali ya kikoloni na uliwanyanyua hadi kufikia kuwa mbele katika siasa mjini Dar es Salaam na katika miji mingine ya Tanganyika.
Umoja wa Wamanyema ndiyo uliojenga msikiti maarufu wa Wamanyema mwaka wa 1912 uliokuwa karibu na makao makuu ya African Association.
Kubwa ambalo Iddi Faizi alifanya ni kule kuwa mratibu wa safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO mwaka wa 1955.
Iddi Faizi ndiye aliyekuwa musanyaji wa fedha za safari hii na kama Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya alitoa fedha za jumuiya hiyo na kuzitia katika mfuko wa safari ya Nyerere UNO.
Picha: Iddi Faizi Mafongo Aliyevaa Kanzu Koti na Tarabush Uwanja wa Ndege Dar es Salaam Akimsindikiza Nyerere Kwenda New York, UNO 1955 wengine kuanzia kushoto ni Rashid Sisso, Robert Makange, Iddi Faizi Mfongo Julius Nyerere, John Rupia na Bi. Titi Mohamed
Habari zaidi za Iddi Faiz Mafungo ingia hapa:
Iddi Faiz Mafongo TANU Card No. 24 Iddi Tosiri TANU Card No. 25 Ndugu Wawili Katika Kupigania Uhuru wa Tanganyika, 1954
Wamanyema wanajulikana kama watu wenye harara na ya ushujaa.
Mmanyema anaweza kuulipia fedha ugomvi ili na yeye awemo, na kadri mpinzani anavyokuwa na nguvu na hodari, ndivyo Mmanyema anavyofaidi ugomvi wake.
Katika siku hizo Wamanyema walikuwa wameshikwa katika magomvi. Katika mwaka wa1941 ilibidi serikali, maimamu na masheikh wa msikiti mingine mjini Dar es Salaam kuingilia kati ili kuamua ugomvi uliowakumba Wamanyema kuhusu msikiti wa Manyema.
Msikiti huu Wamanyema waliujenga mwaka wa 1912.
Wamanyema hawakumstahi mtu yeyote, waligombana hata wenyewe kwa wenyewe.
Hamaki hizi zilipoelekezwa kwa serikali ya kikoloni zilikuja kuwa na manufaa sana.
Kwa kuwa walikuwa ni kabila la Waislam watupu, Wamanyema hawakuweza kufaidika na elimu iliyokuwa ipo mokononi mwa wamishionari.
Hata hivyo Wamanyema walipiga hatua kubwa katika elimu ya dini yao na hii ndiyo sababu kuwa hadi leo utamaduni wa Kiislamu umeenea katika kila familia ya Mmanyema iwe nyumbani Kigoma au huko pwani.
Mmanyema hayupo mbali sana na utamaduni wa Kiislam. Wamanyema, Warufiji na Wadigo ni katika makabila ambayo ni tabu sana kumpata Mkristo.
Iddi Faiz alikuwa Mmanyema.
Hadhi yake iliongezeka zaidi kwa kuwa alikuwa mweka hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na TANU.
Vilevile aliifanyia kampeni TANU, akifuatana na Nyerere katika safari za awali za kukitangaza chama, akihutubia mikutano jukwaa moja na Nyerere.
Ilikuwa ni Iddi Faiz na kaka yake Iddi Tosiri ndiyo waliompeleka na kumtambulisha Nyerere kwa binamu yao Sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo.
Ilikuwa ni baada ya utambulisho huu kwa Sheikh Ramia ndipo urafiki ukajengeka kati ya Sheikh Ramia na Nyerere na ndiyo Nyerere akakubalika Bagamoyo.
Sheikh Ramia akiwa khalifa wa tariqa ya Qadiriya alikuwa na murid wengi waliomfuata katika TANU kama kiongozi wao.
Juu ya hayo alikuwa miongoni mwa wanachuoni walioheshimiwa sana.
Hakuna kilichoweza kusimama na kuota mizizi Bagamoyo bila kupata ridhaa ya Sheikh Mohamed Ramia na hii ilikuwa toka wakati wa TAA.
Akiwa khalifa wa tariqa ya Qadiriya ambayo ilianzishwa na kustawishwa Bagamoya na baba yake, Sheikh Yahya Ramia, mwanzoni mwa karne ya ishirini, nguvu za Sheikh Ramia zilikuwa hazisemeki.
Alichosema sheikh ndicho hicho kilichofuatwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba IddI Faiz Mafongo alihudhuria mkutano wa uzinduzi wa TANU katika Ukumbi wa Arnautoglu mwezi Agosti 1954.
Haifahamiki kwa hakika hasa ni lini Iddi Faiz alijiunga na TANU kwa sababu kadi yake ya kwanza ya uanachama ilipotea na akapewa kadi nyingine iliyokuwa na namba 915 iliyotolewa tarehe 28 Agosti, 1954.
Lakini kwa kukisia tu kutokana na kadi ambayo Iddi Faiz mwenyewe aliitoa kwa kaka yake Iddi Tosiri ambayo ilikuwa kadi namba 25 na yenye saini yake kama afisa aliyetoa kadi hiyo, inaweza kuchukuliwa kwa uhakika kuwa Iddi Faiz alikuwa miongoni mwa wale watu wa mwanzo kabisa kuingia TANU na huenda akawa miongoni mwa wanachama ishirini wa mwanzo.
Ukichukua katika fikra ukweli kwamba Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa katibu wa Al Jamiatul Islamiyya aliingizwa TANU na Mtemvu katikati ya mwezi Agosti, 1955, huenda Ali Mwinyi kama katibu wa Al Jamiatul Islamiyya na Idd Faiz akiwa mweka hazina, wote wawili waliingia TANU wakati mmoja.
Iddi Faiz na nduguye Idd Tosiri, muasisi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, walikuwa Wakusu, moja ya makabila ya Kimanyema, kwa upande wa baba yao; na Wabwali kwa upande wa mama yao.
Wote wawili walikuwa katika Batetera Union (Congo Association), chama kilichokuwa kikiwaunganisha Wamanyema wa Tanganyika.
Mzee bin Sudi alikuwa rais muasisi wa chama hicho na baada ya kifo chake Sheikh Hussein Juma alichaguliwa kushika nafasi hiyo.
Batetera Union (Congo Association) kilikuwa chama kilichoshikamana na chenye nguvu sana miongoni mwa vyama vya kikabila vilivyokuwapo wakati wa ukoloni.
Wamanyema ni kabila la Waislam watupu na kwa sababu hii hakukuwa na pingamizi katika kuunga mkono TANU.
Batetera Union kilikuwa na nguvu sana kiuchumi kwa kuwa kilikuwa katika wafuasi wake, watu waliomiliki majumba na walihodhi takriban nusu ya nyumba zilizojengwa mjini Dar es Salaam kati ya vita kuu mbili za dunia.
Uwezo huu wa kiuchumu uliwafanya Wamanyema kuwa wapinzani wagumu wa serikali ya kikoloni na uliwanyanyua hadi kufikia kuwa mbele katika siasa mjini Dar es Salaam na katika miji mingine ya Tanganyika.
Umoja wa Wamanyema ndiyo uliojenga msikiti maarufu wa Wamanyema mwaka wa uliokuwa karibu na makao makuu ya African Association.
Mzee bin Sudi alikuwa rais muasisi wa chama hicho na baada ya kifo chake Sheikh Hussein Juma alichaguliwa kushika nafasi hiyo.
Mzee bin Sudi alikuwa pia ni muasisi wa African Association mwaka wa 1929 pamoja na Kleist Sykes.
Batetera Union kilikuwa chama kilichoshikamana na chenye nguvu sana miongoni mwa vyama vya kikabila.
Wamanyema ni kabila la Waislam watupu na kwa sababu hii hakukuwa na pingamizi katika kuunga mkono TANU.
Batetera Union kilikuwa na nguvu sana kiuchumi kwa kuwa kilikuwa katika wafuasi wake, watu waliomiliki majumba na walihodhi takriban nusu ya nyumba zilizojengwa mjini Dar es Salaam kati ya vita kuu mbili za dunia.
Uwezo huu wa kiuchumu uliwafanya Wamanyema kuwa wapinzani wagumu wa serikali ya kikoloni na uliwanyanyua hadi kufikia kuwa mbele katika siasa mjini Dar es Salaam na katika miji mingine ya Tanganyika.
Umoja wa Wamanyema ndiyo uliojenga msikiti maarufu wa Wamanyema mwaka wa 1912 uliokuwa karibu na makao makuu ya African Association.
Kubwa ambalo Iddi Faizi alifanya ni kule kuwa mratibu wa safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO mwaka wa 1955.
Iddi Faizi ndiye aliyekuwa musanyaji wa fedha za safari hii na kama Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya alitoa fedha za jumuiya hiyo na kuzitia katika mfuko wa safari ya Nyerere UNO.
Picha: Iddi Faizi Mafongo Aliyevaa Kanzu Koti na Tarabush Uwanja wa Ndege Dar es Salaam Akimsindikiza Nyerere Kwenda New York, UNO 1955 wengine kuanzia kushoto ni Rashid Sisso, Robert Makange, Iddi Faizi Mfongo Julius Nyerere, John Rupia na Bi. Titi Mohamed
Habari zaidi za Iddi Faiz Mafungo ingia hapa: