Wamiliki wa Hotel na Bar jijini Mwanza acheni Biashara za kizamani

Wamiliki wa Hotel na Bar jijini Mwanza acheni Biashara za kizamani

Miwatamu

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2012
Posts
1,450
Reaction score
489
Siku chache zilizopita nilikuwa Jijini Mwanza ambapo niliweza kupata burudani kadha wa kadha kutokana na hali ya hewa niliyoikuta huko ukilinganisha na joto la Jijini hapa Bongo. Lakini pamoja na raha zote hizo, kilichonikela zaidi ni jinsi wenye Bar na Hotel wanavyoendesha biashara zao kwa kuendesha biashara zao kizamani.
Niliweza kuzungukia Bar na Hotel zaidi ya kumi, lakini kila nilipoagiza soda aina ya PEPSI nilielezwa kuwa hawauzi kinywaji hicho ila COCA COLA tu. Nilipojaribu kufanya utafiti nikaambiwa kuwa wamiliki wa Kampuni ya Coca huwa wanagawa viti na ahadi za kuwapa ofa za kreti za soda kila mwezi wamiliki wa bar na hotel husika ili wasiuze soda za kampuni nyingine, Je, katika ulimwengu wa ushindani wa kibiashara tunashindana hivyo? Au ni kulazimisha wateja kunywa hata kile ambacho hawakitaki.
Acheni biashara za kizamani wajameni.
Huu ni ushauri usio na TOZO.
 
Ushauri huu ulitakiwa uwape SBL LTD pamoja na Bakhresa wauzaji wa bidhaa shindani,let them do their homework.Zoezi la kugawa vifaa ni marketing tool ya makampuni yote yenye bidhaa zinazofanana kama hao Pepsi wanagawana hivyo vifaa na maslahi yao basi hayo ndo malipo yake.
Kitu tunachoweza kushare hapa ni huduma za hoteli Mwanza bado ziko chini na hazina muendelezo kwa maana ya kuongeza ubora huwezi kuta mabadiliko.
 
Back
Top Bottom